Napenda kwenda nchini Marekani

Napenda kwenda nchini Marekani

kishamawe

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2020
Posts
267
Reaction score
363
Mie ni mtumishi wa serikali (halmashauri ya wilaya) umri wangu umesonga mbele natarajia kustaafu, hivyo basi kabla sijastaafu napenda kutembelea nchini Marekani maarfu USA.

Naombeni mnijuze Kwa kifupi hasa nikifika ubalozi hapo Dar es Salaam maafisa wa ubalozi wataniuliza maswali yapi?

Naombeni mwenye uzoefu anijuze tafadhalini sana
 
Mimi nikutakie tu maandalizi mema, na pia safari njema iwapo utafanikiwa kusafiri.

Binafsi nawaza tu siku moja kwenda Urusi, au Korea ya Kaskazini kwa ajili ya kutalii na pia kuonana na jamaa zangu Vladimir Putin, na mwenzake Kim Jong Un.
 
Mie ni mtumishi wa local government umri umesonga kiasi muda si mwingi ujao nitastaafu , ndoto yangu ni kwenda Nchini Marekani japo hata Kwa wiki moja . Sasa naombeni munijuze ABC.. za hapo US Embassy nitakazo kutana nazo niendapo kuomba VISA .
 
Ukifika Kremlin kata kushoto kuelekea Karlingrad mpa Moscow.

Kumbuka Biden siyo mtu ni nyonya damu.

Chuki hapana kwani ni kidding.

Wanakuja
 
Twende wote Uingereza, nimpata mwaliko na nimepewa fursa ya kwenda rafiki kama yupo,so nitakuwa nimekurahisishia kupata visa. Ila hata marekani siyo ngumu kupata visa ya kwenda kutembea cha msingi kwenye akaunti yako iwe vizuri.
 
Mie ni mtumishi wa serikali (halmashauri ya wilaya) umri wangu umesonga mbele natarajia kustaafu, hivyo basi kabla sijastaafu napenda kutembelea nchini Marekani maarfu USA.

Naombeni mnijuze Kwa kifupi hasa nikifika ubalozi hapo Dar es Salaam maafisa wa ubalozi wataniuliza maswali yapi?

Naombeni mwenye uzoefu anijuze tafadhalini sana
karibu inbox nikujuze
 
Ok. Shida yako ni kwenda kutalii. Ukienda kichwa kichwa hupati. Tafuta kampuni ya kutembeza watalii iliyoko usa. Wasiliana nao. Wakikubali watakupa mwaliko na hoteli ya kufikia. Mwaliko huo ukikamilika nenda nao ubalozini. Uende pia na bank statement iliyonona, hati za viwanja kuonyesha kuwa una uwezo wa kujilisha kule usa na pia una mali hapa nchini ambazo huwezi kuziacha. Barua ya mwajiri itafaa poa. Unaweza kupata. Usiwe mwanachama wa kikundi cha kigaidi. Wanavijua
 
Back
Top Bottom