Amiliki
JF-Expert Member
- May 6, 2011
- 2,085
- 1,004
Ulipoteuliwa tu katika nafasi uliyonayo, ulianza kwa mkwara mzito, ukijidai eti unataka kukirudishia "mvuto" chama uliopotea miongoni mwa jamii (sijui ni nani aliyekwambia kama CCM wamapoteza mvuto!). Kutekeleza mpango wako, ukawa unapita kila mahali na kelele za kujivua gamba huku ukirusha makombora ya kashfa kwa Edward Lowasa (bila hata kuheshimu mchango wake kwa chama ukiachilia mbali umri wake na kuulinganisha na wako). Ukatupa matumaini makubwa kwamba wale uliowaita mapacha watatu ambao ni Lowasa, Chenge na Rostam, ndio ulikuwa mwisho wao kwenye ulingo wa siasa. Ukiacha Rostam aliyeamua kuondoka mwenyewe kwa kuondokana na Siasa za majitaka, waliobakia wanaendelea kuwepo tena kama haitoshi wameendelea kupata nyadhifa mbalimbali kupitia kwa wanachama wengine wa CCM. Je Nape kule kujivua gamba kumeishia wapi? Au umekuwa Staaring wa kihindi ambaye umekufa kabla ya movie kwisha!