Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
kaka umeniwahi kupost mada hii. Mimi mwenyewe nimemsikia Nape kupitia habari ya ITV. Nimeguswa sana ukizingatia mimi sio mwanachama wa ccm na wala sitegemei kuwa mwanachama wa chama hicho. Kwa kauli hiyo ya Nape anamaanisha wale wote wasio wana ccm nchi hii si yao na hivyo wanapaswa kutafuta mahali pengine pa kuishi. Nape amechoka mapema sana wakati umri wake bado mdogo. Nape atwambie tusio wanachama wa ccm twende wapi kama nchi hii ni ya ccm!!!!!! Vinginevyo ajitokeze hadharani nakufuta kauli yake na akiri kwamba ulimi ulitereza.
Mkuu anza sasa maandalizi ya kuirudisha nchi mikononi mwako.
Mwaka 2015 tunatakiwa kupiga kura ya restoration of our beloved country. Muda wa maandalizi ni sasa, andaa na vijana wenzako.