Nape na madai ya uchagga ndani ya CHADEMA

hapana kuna mambo ya ajabu CCM
mara utasikia tunatekeleza mpango wa kaskazini
mimi mngoni sipo CCM kwa akilizangu leo naambiwa na hawa ccm kuwa CDM wachagga
Pumba tupuuuuuuuuuuu ndio maana nasema bora kieleweke nadhani watanzania hawakumwelewa JK kuwa CCM waislam,CDM wakristo tutengane na tufanyaziane in case habari za kubembelezana sitaki

Acha uzushi wa UDINI MKUU. Hatari hiyo. Mungu aepushie mbali.
 
Nakumbuka ile staili ya Rais Obama wakati huo akiwa mgombea, kila uongo Republican waliojaribu kuutumia dhidi ya seneta Obama; Obama ali-rebut huo uwongo kwa nguvu zote na kwa uthibitisho. Twajua CHADEMA wana mambo muhimu ya kufanya zaidi ya kulumbana na Nape, hata hivyo ni busara ku-rebut uongo wa aina yoyote ile dhidi ya CHADEMA kwa uthibitisho. CCM sasa hivi watasema lolote lile as long wakihisi kuwa wanaweza kunusurika kwa njia moja au nyingine na adhabu ya watanzania.

CCM wanajaribu kuwaondoa CDM kwenye reli.CDM wakikosea ku deal na kauli kama hizi zitawagharimu kama CUF mwaka 2005.Waalitwa mjahidina,badala ya kujibu hoja wakawa wanapanga maandamano kuanzia misikitini.
 
Jana kwenye thread nyingine kuna bwana mmoja alionekana waziwazi akinyanyapaa na kudharau eneo/watu wa eneo yalipo makao makuu ya CHADEMA huku akitumia maneno kama 'uswahilini'

Leo tunasoma kwenye vyombo vya habari kuwa Nape anasema hawezi kujiunga na chadema kwa kile anchodai cha wachaga! Hivi wachaga ni watanzania? wako Tanzania kihalali? na kama sio kwa nini waruhusiwe kuwepo na mbaya zaidi kwa nini waruhusiwe kufanya siasa Tanzania?
Tendwa naye aneweza kutoa maelezo kwa nini amesajili chama cha watu wa jamii/kabila moja kinyume na sheria/kanuni za kuanzisha vyama vya siasa?

Mwisho, Nape, ccm ndio wameshika dola kwa maana wanaongoza serikali hivyo wanatakiwa wasimamie sheria za nchi. Na kumbuka viongozi wote wa serikali (rais, mawaziri etc) waliapa kulinda na kutetea katiba ya nchi pamoja na kusimamia sheria. Sasa, kama chadema ni chama wa wachaga basi ni wazi wameenda kinyume na sheria za nchi hivyo Nape na viongozi wenzake wanatakiwa wachukue hatua za kisheria na sio kulalamika mitaani.
 
Ameonyesha Chuki ya Wazi dhidi ya Wachagga anavyowachukia. Huyu Dogo hapa hajapata madaraka. Huenda ametumwa ili kukijengea chama chuki dhidi ya wachagga ili wakichukie na kikose support ya wachagga.

Anaingizwa mkenge na watu wasiokitakia mema chama, ili kichukiwe zaidi na hatimae ionekane chama kimemfia JK mikononi.

Amechokoza mziki mkubwa, je ataweza kuucheza! Akina RACHEL bado wanamsubiri, hawajamalizana nae, sasa anapanua wigo wa maadui!

Dogo hapo unalo!
 
Hebu nielewesheni Nape alizungumzia wapi hili? Lini na katika jukwaa lipi?? Kama ni kweli huyu hatufai na mimi nasema nitaenda Moshi kumlaki na aeleze umma wa Wachaga alikuwa anamaanisha nini
 
huyu dogo kama anataka akomae kisiasa namshauri asiikimbie JF kwani hapa ndio kuna watanzania wasomi wengi na sio kwenda kuongea mitaani na vijijini huku akishangiliwa na watu ambao hata huyo nnape mwenyewe ndio wanamuona kwa mara ya kwanza, yeye hajui kuwa wale wanamshangilia pale kwa sababu wamepewa buku moja moja au mbili mbili lakini hawachanganui kitu chochote so NNAPE amka dogo kabla hujaumia zaidi , nna ukija hapa kujibu hoja hakuna mtu atakaye kutukana
 
Teh teh teh Albedo....... ama kweli wewe unawafahamu CCM vizuri maana hawafanyi jambo bila kuwa wametafiti.......nakubaliana na wewe kuwa sasa CCM wamekosa muelekeo....Kolomba uko wapi uwakumbushe ulichowaambia.
 
Ninependa kujua maneno haya Nape aliyatoa wapi na lini kabla ya kusema lolote?

Angalia mwananchi la leo

Ramadhan Semtawa na Elias Msuya
CCM na Chadema, vimeendeleza siasa za jino kwa jino kufuatia viongozi wake kuzidi kurushiana makombora yaliyobeba tuhuma ndani yake.Jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alimtaka Dk Willibrod Slaa ambaye ni Katibu Mkuu wa Chadema aliombe radhi Bunge, huku Chadema nayo ikimtaja Nape kwamba ni mtuhumiwa wa ufisadi wa EPA uliofanyika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambapo Sh133 bilioni zilikwapuliwa.

Tuhuma hizo kutoka kila upande, ambazo sawa na siasa za jino kwa jino, zimekuja baada ya Nape kutaja alichokiita unafiki wa Dk Slaa kwa kushinikiza kulipwa mshahara wa Sh7.5 milioni na Chadema, wakati alikataa mshahara wa Sh7 milioni alipokuwa mbunge akidai ni mkubwa na uliwanyonya Watanzania.

Vyama hivyo jana kwa nyakati tofauti, kila kimoja kiliongeza mashambulizi dhidi ya kingine, ambapo Nape alikwenda mbali zaidi akimtaka Dk Slaa aliombe radhi Bunge na wabunge kwa alichoeleza kuwa Dk Slaa alipokuwa Mbunge wa Karatu, alichochea chuki kwa wananchi dhidi ya taasisi hiyo.

"Najua Chadema watakuwa wanajibu, lakini nasema msimamo wangu uko mbele zaidi kwamba Dk Slaa aliombe radhi Bunge na wabunge, kwani alichochea chuki kwa wananchi dhidi ya Bunge, halafu yeye anakuja kuchukua mshahara zaidi ya ule aliojidai kuukataa. Huu ni unafiki," alisisitiza Nape.Nape alisema Dk Slaa ni Padre hivyo pia alipaswa kuungama kwa Mungu kwa kutokuwa mkweli ndani ya dhamira yake."Bahati nzuri Dk Slaa ni Padre, namshauri pia amuombe radhi Mungu, kwani amekuwa akipita mitaani kupandikiza chuki miongoni mwa Watanzania kumbe naye hana maadili yoyote," aliongeza Nape.

Alifafanua kwamba mshahara anaolipwa Dk Slaa ni kodi ya wananchi inayotokana na ruzuku, hivyo ni matumizi mabaya kumpa mshahara mkubwa kama huo wakati aliukataa akiwa mbunge.Kama alivyofanya katika mkutano wa kwanza aliofanya Kata ya Ulugu jimboni Iramba, Nape alisema ataendeleza mashambulizi dhidi ya Dk Slaa katika mikutano yake yote itakayofanyika mkoani Singida ili kuweka wazi maovu ya kiongozi huyo kwa kile alichokiita uchonganishi.

"Hapa naelekea Iramba Mashariki, lakini ninachosema ni kwamba, nitaendelea kuwaeleza Watanzania unafiki wa Dk Slaa. Hatutaki viongozi wanaoeneza chuki wakati wao wenyewe hawana maadili yoyote,"aliongeza.
Alisema ndani ya Chadema wapo baadhi ya watu wanalipwa kiasi cha fedha ambacho ni kidogo na wanaishi kwa shida kubwa hivyo, kama Dk Slaa ni mwadilifu awaangalie hao.


MJumbe wa kamati kuu ya Chadema Mabere Marando akionyesha ripoti ya fedha ya chama hicho kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana

Chadema waja juu
Lakini mkutano na waandishi wa habari jana, licha ya kufafanua kuhusu mshahara wa Katibu Mkuu wake, Dk Slaa na ununuzi wa magari, Chadema jana ilimuita Nape kuwa ni 'Vuvuzela' na kwamba hana sifa ya kuinyooshea kidole Chadema.

"Tuna ushahidi wa kutosha kuwa mmoja wa watu walionufaika na fedha za EPA kupitia kwa Jeetu Patel ambaye ameeleza vizuri jambo hili katika maelezo yake mbele ya kamati ya Rais," alisema Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Chadema, Anthony Komu.

Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Mabere Marando alidai kuwa Nape aliwahi kuomba kugombea ubunge kupitia Chadema baada ya kushindwa kupata nafasi hiyo kupitia CCM, lakini wakamtosa kwa kuwa hakuwa na sifa.

"Nilikuwapo kwenye kikao cha kumjadili Nape, tukaona kuwa hana sifa kumzidi John Mnyika ambaye sasa ni mbunge" alisema Marando. Lakini akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu, Nape aliwataka Chadema kutoa ushahidi unaoonyesha kuwa alihusika na ufisadi wa EPA.

"Atoe ushahidi hadharani, unajua hawa watu ni waongo, hata Watanzania watawashangaa," alisema Nape.
Kuhusu suala la kuhamia katika chama hicho, Nape alisema: "Tena uandike kabisa, mimi ndiyo ninao ushahidi wa wao kunitaka nikagombee kupitia chama chao nikakataa, kwa sababu siwezi kuhamia kwenye chama cha Wachagga, kile ni chama cha ukoo," alisema Nape.

Mishahara ya Makatibu Wakuu
Akifafanua mshahara wa Dk Slaa, Komu alisema kuwa Katibu wake hawajawahi kuomba, kushinikiza wala kuchagiza kulipwa kiasi cha Sh 7.5 milioni kama inavyodaiwa bali analipwa Sh 1,725,000 milioni wakati mbunge analipwa Sh 2,305,000 kabla ya kukatwa kodi.

Alifafanua kuwa Dk Slaa pia hulipwa Sh900,000 za mafuta kwa ajili ya kwenda na kurudi ofisini. Vingine ni malipo ya nyumba, mawasiliano na uwajibikaji na hivyo kuufanya mshahara wake kufikia Sh7,174,000 kwa mwezi.

"Sekretarieti ya Kamati Kuu ilipeleka pendekezo hilo katika vikao vyake vya Kamati Kuu na Baraza Kuu na pendekezo hilo likapitishwa kwa njia ya uwazi na likaingizwa katika mpango kazi wa chama," alisema Komu.

Naye Mabere Marando alikituhumu CCM kuwa kinamlipa Katibu Mkuu wao Sh 11 milioni akisema: "CCM wanapigia kelele mshahara wa Dk Slaa, mbona Mukama (Wilson) analipwa Sh11 milioni?. Mbona Rais Jakaya Kikwete analipwa posho nyingi tu? Ofisi yake iko Dodoma, lakini akienda huko analipwa posho, akirudi Dar es Salaam analipwa," alisema Marando.

Alipoulizwa na Mwananchi kuhusu madai ya Marando, Mukama alikataa kutaja mshahara wake akisema kuwa ni siri yake.

"Mimi leo ndiyo natimiza mwezi mmoja tangu niingine ofisini, hata mshahara wenyewe sijauona. Mshahara ni siri yangu mwenyewe, nimeingia hapa baada ya kustaafu kwa hiyo ndiyo hivyo, naomba msiniingize kwenye hizo ‘debate' (malumbano)" alisema Mukama.

Lakini akijibu hoja hiyo, Nape alisema kuwa Mukama analipwa mshahara kulingana na daraja la viongozi na hurekebishwa kama watendaji wengine serikalini.

"Katibu Mkuu wetu analipwa Sh1.5 milioni na hukatwa kodi. Vilevile hulipwa posho isiyokatwa kodi ya Sh300,000. Hayo mengine ya usafiri ni mambo ya kawaida tu. Usafiri anao na hulipiwa umeme wa LUKU na nyumba. Siyo suala la kificho hilo," alisema Nape.

Mafuso ya Chadema
Wakijibu hoja ya Nape kuwa Chadema kimenunua magari chakavu, walikanusha wakisema kuwa magari hayo licha ya kutokuwa chakavu, siyo magari ya kawaida bali ni mitambo maalumu ya uenezi.

"Katika magari hayo kuna vipaza sauti (Public addressing system 3 sets) zenye thamani ya dola za Marekani 148,000 (Sh 222 milioni), jenereta tatu kila moja Sh15.5 milioni sawa na Sh47,000,000," alifafanua Komu.

Naye Marando alisema kuwa chama ndiyo kilimwomba Mwenyekiti Freeman Mbowe awauzie magari hayo ndipo akakubali. "Mimi mwenyewe nilihusika kumwomba Mbowe atupe magari yale, akakubali. Baada ya hapo Kamati Kuu iliunda kamati ya watu wanne chini ya makamu mwenyekiti Zanzibar Mohamed Issa kumwomba mwenyekiti akiachie chama magari hayo.

Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Profesa Abdallah Safari alisema kuwa CCM inatumia ujinga wa Watanzania kama mtaji wake na kuwataka Watanzania kutoyumbishwa na propaganda za CCM.
 
Hivi kweli haya yote yanatokana na hii sentensi moja, au I'm i missing something?

"Tena uandike kabisa, mimi ndiyo ninao ushahidi wa wao kunitaka nikagombee kupitia chama chao nikakataa, kwa sababu siwezi kuhamia kwenye chama cha Wachagga, kile ni chama cha ukoo"
 
Huu upuuzi wa NApe usiachwe nyinyi CDM ni lazima uongozi wa njuu uitishe mkutano wa waandishi wa habari kulaani hii simu inayoenezwa na huyu kijana


Not at all,Viongozi wetu hawawezi kujibishana na Nape.Wapo kikazi zaidi kuhakikisha ukombozi unapatikana Nape ni Mbwayuwayu tu a guy after money.
 
Nape hivi umewahi kusikia CDM wakilalamikia kuhusu CCM kuwa chama cha Kisultani? Hawaoni sababu ya kufanya hivyo kwa kuwa hiyo sio agenda yenye kuleta tija kwa Watanzania........Dogo soma alama za nyakati Nyoka akijivua gamba hawi Mjusi......huyo EL si mlitaka kumtosa akaibukia kwenye uenyekiti wa kamati ile ya Bunge.........Sasa subiri akutokee akiwa mwenyekiti wa chama chako utalamba viatu vyake.....huyo jamaa CCM hamumuwezi hata kidogo.......Mwalimu JK aliwaambia huyu kijana MHUNI hamkutaka awafafanulie mkaishia kukenua meno tu sasa atawafundisha.......
 
Hivi kweli haya yote yanatokana na hii sentensi moja, au I'm i missing something?

"Tena uandike kabisa, mimi ndiyo ninao ushahidi wa wao kunitaka nikagombee kupitia chama chao nikakataa, kwa sababu siwezi kuhamia kwenye chama cha Wachagga, kile ni chama cha ukoo"

Huu ni ushahidi tosha dhidi ya tuhuma za Nape kwenda kinyume cha maadili ya uongozi, kwa kukishushia tuhuma nzito za ukoo na ukabila chama kilichosajiliwa kwa kufuata utaratibu na sheria za nchi kwa kupata wadhamini toka kanda mbalimbali za Tanzania ikiwemo Zanzibar.

CCM imeruka jivu na kukanyaga moto kwa kumweka huyu dogo ambaye bado bongo lake halijakomaa na folders bado layers hazijapanga vuzuri. Kazi kama hiyo anayofanya inahitaji mtu mkomavu, mvumilivu, mpambanuzi na mwenye kufanya upembuzi yakinifu kabla ya kumwaga mtama kwenye kuku wengi.

Makamba ametulia anachekelea walivyomtoa mkumku pale Dodoma, afadhali mgosi wa kaya licha ya kuropoka alikuwa mwangalifu katika utoaji wa kauli zinazogusa umoja wa kitaifa. Mnauye sijui atakapofika Kilimanjaro atawajibu nini anaowaita Wachaga ambao ni watanzania wenzetu.

Bora lawama kuliko fedheha​
 
Alipoulizwa na Mwananchi kuhusu madai ya Marando, Mukama alikataa kutaja mshahara wake akisema kuwa ni siri yake. "Mimi leo ndiyo natimiza mwezi mmoja tangu niingine ofisini, hata mshahara wenyewe sijauona. Mshahara ni siri yangu mwenyewe, nimeingia hapa baada ya kustaafu kwa hiyo ndiyo hivyo, naomba msiniingize kwenye hizo ‘debate' (malumbano)" alisema Mukama.

Unaweza kupambanua na jibu la Katibu mkuu wa CCM ambaye anatumia busara badala ya kuropoko tu kama vuvuzela, anachofanya ni kujifunza kwanza kazi mpya aliyopewa badala ya kuanza kujiingiza kwenye malumbano. Hapo nimejifunza kitu kwake, ana busara, lakini huyu dogo Nape,mmmmmmmmmmmmmmmm! Kazi kweli kweli vandugu zangu.
 
naona mzee wa gamba unakariri maisha, kumbuka maisha hayana formular i.e. to say sio kila mweupe au mwenye jina Mnyika ni mchaga. kuna cku utasikia kimaro ametokea Mbeya vilevle so usishangae

Kaka mnyika ni msukuma wa magu, wala siyo mchaga baba yake anatokea magu na ndiyo chimbuko lake asante

wazee nawashukuru sana sikufahamu kbs kama mnyika ni mtu nyumbani lkn mlikuwa wapi siku zote kuweka mambo sawa?? mimi nilikuwa najua ni mchaga, nadhani tunamuhitaji kijana wetu 2015 maana magu wamepeleka mganga wa kienyeji mjengoni.

sina gamba jamani, someni signature
 
Labda Nape amefanya tathmini hii kwamba katika Orodha hii ya watu 19 tu, kaskazini ni wajumbe watano 5 ambao ni sawa na asilimia 26 ya wajumbe wote.Vile vile nafasi muhimu kwa maana ulaji na utawala ni ile ya KOMU(FEDHA) na Mrema kule kwenye utawala wa bunge na halmashauri.Hawa wote ni eneo moja aisee.Mkoa wa kilimanjaro ni sawa na asilimia 3 ya mikoa yote Tanzania.Hii ni sekretariet tu bado KAMATI YENYEWE na Mkutano Mkuu akiwemo Mtei.
 
Ndiyo tatizo la kufanya kazi kwa kufuata "ZIDUMU FIKRA ZA MWNYEKITI" Nnape kila afanyala anafikiria ampendezeshe mwenyekiti, na si awapendezeshe watanzania wapenda CCM,
 
CCM hawana hoja za msingi maana kuna kipindi walisema CHADEMA ya wakatoliki baadae mara ya wakristu then wanakuja kuwaomba kura wakristo haohao tabu tupu

mwenyekiti wake aliwahikuwatukana wafanyakazi baadae akarudi kuwaomba kura na kuwaongeza mishahara kimyakimya sijui Nape atawafanyia nini kuwapoza wachagga...Nape kazi unayo....
 
Nimekuwa nikifuatilia mambo mbalimbali katika magazeti na naweza kusema kuwa inaonekana kuna kawaida ya watu/viongozi wa CCM kuchukua kila aina ya silaha wanayoiona itawasaidia kumwangusha mpinzani wao.

Wakati wa kampeni nilisoma Beno Malisa (ambaye naye nafikiri ni Mchagga) akisema "Kule Kenya fisadi ni mtu aliyepora mke wa mtu". Sina haja ya kueleza alikuwa anakusudia kusema nini au kumsema nani ambaye wakati huo waliichukua hiyo kama silaha yao. Nikasoma comments za spika A. Makinda akilisema hilo hilo mara tu baada ya kuchaguliwa. Naye alikuwa akilenga lile lile.

Vijana wa mkoa wa Pwani walidai Uraisi hautakwenda kwa watu wa kaskazini. Hapo walikuwa na aina mbili za watu waliowaleng, Mh. Sumaye waliyekuwa wakumrudi na wanowaita viongozi wa CHADEMA.

Pamoja na mbao mengi niliyoyasoma na kyafuatilia, suala la CHADEMA kuwa chama cha Wachagga au watu wa Kilimanjaro na Arusha nimelisoma mara nyingi kutoka kwa watu wa cadre ya chini ya wapinzani wao. Sasa limechukuliwa na viongozi wenyewe. Hivi kweli ahadi za CCM za kusema kweli daima ... bado ipo? Watanzania tuliangalie kwa makini kuitambu CCM ya "KISASA">
 
Back
Top Bottom