Nape: Lowassa kapoteza sifa ya kugombea

Nape: Lowassa kapoteza sifa ya kugombea

Hii imesemwa na Na Nape hapo jana baada ya Lowasa kutangaza nia kanisani Monduli
 
Nadhani Lowassa alisema anaanza na Mungu na kwa Jina la Yesu Kristo atatimiza ndoto yake. Imani hiyo ni juu ya yote na ni juu ya mawazo na mipango na taratibu tunazozijua. Mhimu sasa Mungu mwenyewe aweke mtenda kazi wake.

Mungu na jizi la raslimali za watu wake wapi na wapi? Mwambieni huyo lowasa atupe msimamo wake juu ya haya maswala makubwa yanayolitesa taifa; RUSHWA,UFISADI,BIASHARA YA UNGA,MIKATABA MIBOVU,UTOROSHAJI WA PESA NJE,WIZI WA RASLIMALI NA VIWANDA VYETU KUFA AU KUTOFANYA KAZI! Kama hawezi kuyaongelea haya basi hafai hata kuwa diwani.
 
Nape mwache mzee wa watu. Mbona JK alitangaza miaka 9 kabla na hakupoteza sifa? Naanza kuhisi Kwa EL anajambo kubwa linalo watisha huko. Mwacheni mzee wa watu.
To EL; songa mbele baba miiba;milima na mabonde utavivuka. Ziba masikio yako Angalia kuitimiza Ndoto yako tu.
 
  • Thanks
Reactions: Sal
Japo Nape ni Mropokaji lakini kwa mara ya kwanza nakubaliana na Kauli hii yake. Ni kweli Lowassa kapoteza sifa ya kuwa Rais wa tano wa Tanzania.
 
Acha kupotosha watu weka chote nilichosema. Nilichosema ni kuwa yeyote anayekiuka taratibu za chama katika mchakato ANAJIONDELEA SIFA za kuwa mgombea wa chama hichi!(Labda Chama kiamue kutofuata taratibu zake chenyewe, na kikiziacha hakina namna ya kuendelea kuaminiwa)! Sasa si swala la Lowassa ni swala la KILA ANAYEKIUKA TARATIBU!kama naye anakiuka anaingia kwenye mkumbo huo, sio kwasababu ni Lowassa ila kwasababu ni mwana CCM na taratibu za CCM haziruhusu! Sio swala la Nape ni swala la taratibu,kanuni na sheria zilizowekwa kabla hata Nape hajazaliwa!

Haiwezekani watu wagawe rushwa hovyo tukae kimya tu kisa anayegawa flani!!!! Hivi kuna uwezekano wa kuingia na kiti moto msikitini ukapigiwa makofi?!! Unaweza kupigiwa makofi na kupewa uongozi wa kanisa wakati humwamini Yesu Kristo?!! Watanzania tusiogope kusema ukweli maana ndio utakaoiponya nchi yetu.
Kama mnamgombea ana sifa atachaguliwa tu huna haja ya kuongezea sifa zake kwa rushwa! Haya si yangu ya CCM, na ni kwa madiwani, wabunge na hata urais!
HERI YA MWAKA MPYA 2014!

Nape kuhusu Kanuni na taratibu za chama umeeleweka kabisa na uko sahihi ila suala la rushwa sijakuelewa unataka kumaanisha nini. Kama kuna watoa rushwa CCM ina taratibu nzuri kabisa za kuwashughulikia, kwa nini usiwashitaki kwenye vikao ili Chama kiwachukulie hatua?
 
Elewa kuwa kutoa sadaka na zaka sio sifa ya kuweza kuongoza nchi ila anapalilia njia ya kwenda mbiguni .



J
 
  • Thanks
Reactions: Sal
Kwani lowasa ni wapi amesema anataka kugombea urais???? kasema ana ndoto hamna ushahidi wowooooteee ni porojooo tuuuu
 
Huyu Lowassa hata rasimu ya katiba mpya inamkataa. Kwa sifa za anayepashwa kugombea uraisi, Lowassa yuko nje kabisa.

Tiba
 
Nape ni mtoto mdoga sana kwa lowasa hagusi hata chembe ya harufu yake. Jamaa ndo katangaza nia Akiwa mbele ya wadau wote anaowaamini. Nape lawashindwa akina Kawambwa atamuweza Papaaaaaa Mihela> akaoge.
 
Acha kupotosha watu weka chote nilichosema. Nilichosema ni kuwa yeyote anayekiuka taratibu za chama katika mchakato ANAJIONDELEA SIFA za kuwa mgombea wa chama hichi!(Labda Chama kiamue kutofuata taratibu zake chenyewe, na kikiziacha hakina namna ya kuendelea kuaminiwa)! Sasa si swala la Lowassa ni swala la KILA ANAYEKIUKA TARATIBU!kama naye anakiuka anaingia kwenye mkumbo huo, sio kwasababu ni Lowassa ila kwasababu ni mwana CCM na taratibu za CCM haziruhusu! Sio swala la Nape ni swala la taratibu,kanuni na sheria zilizowekwa kabla hata Nape hajazaliwa!

Haiwezekani watu wagawe rushwa hovyo tukae kimya tu kisa anayegawa flani!!!! Hivi kuna uwezekano wa kuingia na kiti moto msikitini ukapigiwa makofi?!! Unaweza kupigiwa makofi na kupewa uongozi wa kanisa wakati humwamini Yesu Kristo?!! Watanzania tusiogope kusema ukweli maana ndio utakaoiponya nchi yetu.
Kama mnamgombea ana sifa atachaguliwa tu huna haja ya kuongezea sifa zake kwa rushwa! Haya si yangu ya CCM, na ni kwa madiwani, wabunge na hata urais!
HERI YA MWAKA MPYA 2014!

Ni ufaanuzi mzuri, ujumbe umefika. kanuni, taratibu, sharia pamoja na misingi iliyowekwa lazima ifuatwe.Zaidi ya hapo haliwezi kuwa kudi lenye nia moja.
 
Kwani lowasa ni wapi amesema anataka kugombea urais???? kasema ana ndoto hamna ushahidi wowooooteee ni porojooo tuuuu

Yuo must be dellusional if you can't read between the lines!!!
Unataka ushahidi gani??
Kujifanya mlokole kanisani na "ndoto" za safari ya kupitia mabonde, milima na makorongo ni safari ipi hiyo? Ya kwenda mbinguni???
C'mon man usijitie hamnazo.
Uroho wa pesa na sasa cheo cha urais kutamfikisha pabaya Lowassa. Angetulia aangalie afya yake tete badala kulilia urais kama mtoto mdogo analilia andazi....
Siku Lowassa akipata uraisi, kama niko hai, nitahama hii nchi.
Maana nitajuwa kiukweli WATANZANIA wote tuko majnoon!
 
Nappe na Lowasa vita yao bado haijaisha?
 
nape anaota...kauli zake kama za zitto hakamilishi kusudio la kauli
 
Anatishia ili wasijiingize wengine wakamchafua mzee mamvi. Anamzia EL ile mbaya kwani anajua atamkumbuka kwenye huo ufalme wake.
Huenda EL akamtosa Mangula akampa Nape
 
Hii imesemwa na Na Nape hapo jana baada ya Lowasa kutangaza nia kanisani Monduli
haileti taswira nzuri hata kidogo. yeye kama anataka kuwa kiongozi wa kitaifa. we will see at the end.
 
Nyambaf!

Hicho chama si mali yako au babayako, kila mtanzania ana haki ya kutoa maoni yake ilimradi asivunje sheria ya nchi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom