Nape: Lowassa kapoteza sifa ya kugombea

Nape: Lowassa kapoteza sifa ya kugombea

Crashwise

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
22,227
Reaction score
8,760
sakata la Nape na lowasa limeendelea baada ya Nape jana kumwambia kwa kutangaza nia kabla ya wakati wake amepoteza sifa ya kuteuliwa kupitia chama cha mapibduzi.
maoni yangu: Nabe acha kushindana na Lowasa au umesahau ulivyobanwa kule dodoma ukitakiwa kupeleka ushahidi wa ufisadi wa lowasa vinginevyo umuombe msamaha, ukakomea kumpigia magoti, umesahau ulishatangaza siku 90 vinginevyo ungemg'o mpaka leo Siku 90 imegeuka miaka 90..

source: Mwananchi/RFA


Dar es Salaam.
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesema mwanachama yeyote anayetangaza nia ya kuwania nafasi ya urais kabla ya muda mwafaka kutangazwa, anapoteza sifa ya kuwa mgombea.


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema Dar es Salaam jana kwamba chama hicho kinaamini katika umoja na mshikamano na kwamba wanaotangaza nia ya kugombea urais kabla ya muda wamepoteza sifa kwa kuwa ni kama wanakigawa.

Juzi, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa alitangaza nia ‘kimtindo' akisema anaanza rasmi safari aliyoiita ya matumani ya ndoto zake, ambayo pia itatimiza ndoto za Watanzania za kupata elimu bure, maji safi na maendeleo ya uhakika.

Lowassa ambaye amekuwa akitajwa kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais kupitia CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, alitangaza hayo katika ibada ya shukrani ya kuupokea mwaka mpya, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Monduli.

Nape alisema wanaotangaza nia ya kuwania urais hivi sasa wanafahamu kwamba hawana sifa za kuwa wagombea wa nafasi hizo kwa sababu mbalimbali.

Alisema wanafahamu wazi kwamba vikao vya chama havitawapitisha kutokana na kutuhumiwa kwa rekodi zao pia ni mbaya.

"Suala hili liko wazi katika chama chetu, viongozi wenye sifa waliowahi kuongoza nchi hii hawakujitangaza mapema. Walisubiri na muda ulipofika wakatangaza nia ya kuwania," alisema Nape.

Alisema kwa hao wanaojitangaza hivi sasa kabla muda, wanakigawa chama na kwamba vikao havitawapitisha labda wafanye hivyo kupitia vyama vingine.

"Labda wagombee urais kupitia vyama vingine lakini si CCM, chama hiki kina misingi na taratibu zake, wanachama wanashikamana hadi muda utakapofika," alisema.

Alisema viongozi bora hawapatikani kwa kujiandaa wao wenyewe kuchukua nafasi hizo, bali kwa kuombwa na wanachama wenzao katika hatua mbalimbali zinazokubalika.

Urais CCM

Oktoba mwaka jana, Rais wa Zanzibar, Dk Mohamed Ali Shein alielezea kushangazwa na tabia ya baadhi ya wanachama wa CCM kutangaza nia ya kuwania nafasi za uongozi kwa uchaguzi wa 2015 ikiwamo nafasi ya urais wakati wahusika wa nyadhifa hizo bado hawajamaliza muda wao.

Akifungua Mkutano wa Makatibu wa CCM wa Mikoa, Dk Shein aliwataka watu hao kusubiri hadi chama kitakapotoa mwongozo.

Katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwenye mikoa ya Kusini na Nyanda za Juu Kusini, mwishoni mwa mwaka jana, alisema wanaotangaza nia mapema, wanajitengenezea mazingira magumu ndani ya chama.

Mbali na Lowassa, wengine wanaotajwa kuwania nafasi hiyo ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Mbunge wa Songea Mjini, Dk Emmanuel Nchimbi na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba.

Source: Mwananchi.

====================
Ufafanuzi wa Nape
====================
Acha kupotosha watu weka chote nilichosema. Nilichosema ni kuwa yeyote anayekiuka taratibu za chama katika mchakato ANAJIONDELEA SIFA za kuwa mgombea wa chama hichi!(Labda Chama kiamue kutofuata taratibu zake chenyewe, na kikiziacha hakina namna ya kuendelea kuaminiwa)!

Sasa si swala la Lowassa ni swala la KILA ANAYEKIUKA TARATIBU!kama naye anakiuka anaingia kwenye mkumbo huo, sio kwasababu ni Lowassa ila kwasababu ni mwana CCM na taratibu za CCM haziruhusu! Sio swala la Nape ni swala la taratibu,kanuni na sheria zilizowekwa kabla hata Nape hajazaliwa!

Haiwezekani watu wagawe rushwa hovyo tukae kimya tu kisa anayegawa flani!!!! Hivi kuna uwezekano wa kuingia na kiti moto msikitini ukapigiwa makofi?!! Unaweza kupigiwa makofi na kupewa uongozi wa kanisa wakati humwamini Yesu Kristo?!! Watanzania tusiogope kusema ukweli maana ndio utakaoiponya nchi yetu.

Kama mnamgombea ana sifa atachaguliwa tu huna haja ya kuongezea sifa zake kwa rushwa! Haya si yangu ya CCM, na ni kwa madiwani, wabunge na hata urais!

HERI YA MWAKA MPYA 2014!
 
Nape ni kiongozi wa CCM lakini mwenzake ana kundi kubwa na chama ni watu.Sasa siijui atashindana na huyo jamaa kivipi.Pili Lowassa hakutamka wazi kuwa anataka kugombea ila aliongea kwa mafumbo.

Nape kazi ya kutumika itakuumbua!
 
Nape alisema wote wanaotangaza nia wamepoteza sifa ya kuteuliwa.
Kwa juu nawaona lowasa january makamba sitta sumaye na membe hawa wanatumia lugha ya matendo kutangaza nia.
 
sakata la Nape na lowasa limeendelea baada ya Nape jana kumwambia kwa kutangaza nia kabla ya wakati wake amepoteza sifa ya kuteuliwa kupitia chama cha mapibduzi.
maoni yangu: Nabe acha kushindana na Lowasa au umesahau ulivyobanwa kule dodoma ukitakiwa kupeleka ushahidi wa ufisadi wa lowasa vinginevyo umuombe msamaha, ukakomea kumpigia magoti, umesahau ulishatangaza siku 90 vinginevyo ungemg'o mpaka leo Siku 90 imegeuka miaka 90..

source: mwananchi/rfa

Mkuu mbona sikuelewi?! uko upande wa nani?! ushajikatia tamaa au unakula kotekote?
Je ushauri wako ni ili ccm iendelee kutawala au unajipendekeza kwa lowasa?
 
Acha kupotosha watu weka chote nilichosema. Nilichosema ni kuwa yeyote anayekiuka taratibu za chama katika mchakato ANAJIONDELEA SIFA za kuwa mgombea wa chama hichi!(Labda Chama kiamue kutofuata taratibu zake chenyewe, na kikiziacha hakina namna ya kuendelea kuaminiwa)!

Sasa si swala la Lowassa ni swala la KILA ANAYEKIUKA TARATIBU!kama naye anakiuka anaingia kwenye mkumbo huo, sio kwasababu ni Lowassa ila kwasababu ni mwana CCM na taratibu za CCM haziruhusu! Sio swala la Nape ni swala la taratibu,kanuni na sheria zilizowekwa kabla hata Nape hajazaliwa!

Haiwezekani watu wagawe rushwa hovyo tukae kimya tu kisa anayegawa flani!!!! Hivi kuna uwezekano wa kuingia na kiti moto msikitini ukapigiwa makofi?!! Unaweza kupigiwa makofi na kupewa uongozi wa kanisa wakati humwamini Yesu Kristo?!! Watanzania tusiogope kusema ukweli maana ndio utakaoiponya nchi yetu.

Kama mnamgombea ana sifa atachaguliwa tu huna haja ya kuongezea sifa zake kwa rushwa! Haya si yangu ya CCM, na ni kwa madiwani, wabunge na hata urais!

HERI YA MWAKA MPYA 2014!
 
Nilini lowasa aliwahi kuwa nasifa za kuwa mgombea...
 
Nadhani Lowassa alisema anaanza na Mungu na kwa Jina la Yesu Kristo atatimiza ndoto yake. Imani hiyo ni juu ya yote na ni juu ya mawazo na mipango na taratibu tunazozijua. Mhimu sasa Mungu mwenyewe aweke mtenda kazi wake.
 
Nape Nnauye na wewe unaamin kwamba ukweli ndio utaiponya nchi???!!
 
Last edited by a moderator:
Nape yuko ccm kimaslahi tu, lakini kimtazamo yuko upinzani kabisa! Lowassa akiukwaa urais nape ahame nchi.

siyo kwamba ni kambi tofauti tu ndiyo maana anatofautina na lowasa na vijana wake kama nchemba, january....wakati kambi yake ni Sitta, mwakyembe...
 
Nape punguza mdomo usijifanye mungu mtu,mimi naunga mkono lowasa kuwa mgombea kwasababu uweza anawo sababu anayo mwisho anamaamuzi magumu nchi itanyooka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom