Just Distinctions
JF-Expert Member
- May 5, 2016
- 2,701
- 5,329
Pole sana kwa kumpoteza ndugu yako na pongezi kwenu kwani sio wengi wanaoweza ama walioweza kushibana na ndugu zao wa damu kwa upendo mkubwa.
ni jambo la heri kupata nafasi hiyo ya kumuota nduguyo na kujumuika naye njozini, japo binafsi yangu bila kuathiriwa na mitazamo ya kidini wala mila naamini kuwa ndoto hazina maana yoyote hivyo sijawahi kutilia maanani juu ya chochote kile ninachokiota.
ila kwa hii simulizi yako I wish japo walau kwa sekunde chache tu Marehemu Baba yangu angekuja hata ndotoni ili nimuambie kuwa yale aliyoniusia kwa hakika sasa nayashuhudia.
hii dunia ni tofauti na nilivyoitarajia, nimshukuru kwa malezi aliyonipa, upendo, ushauri, miongozo, maonyo na kila kitu, nampenda sana na anisamehe kwa yote ambayo nilimkosea na nimuahidi kuwa yale yote aliyoyaacha au kupanga kuyafanya, nitayatimiza na ulimwengu ipo siku utayashuhudia, na iwe hivyo.
ni jambo la heri kupata nafasi hiyo ya kumuota nduguyo na kujumuika naye njozini, japo binafsi yangu bila kuathiriwa na mitazamo ya kidini wala mila naamini kuwa ndoto hazina maana yoyote hivyo sijawahi kutilia maanani juu ya chochote kile ninachokiota.
ila kwa hii simulizi yako I wish japo walau kwa sekunde chache tu Marehemu Baba yangu angekuja hata ndotoni ili nimuambie kuwa yale aliyoniusia kwa hakika sasa nayashuhudia.
hii dunia ni tofauti na nilivyoitarajia, nimshukuru kwa malezi aliyonipa, upendo, ushauri, miongozo, maonyo na kila kitu, nampenda sana na anisamehe kwa yote ambayo nilimkosea na nimuahidi kuwa yale yote aliyoyaacha au kupanga kuyafanya, nitayatimiza na ulimwengu ipo siku utayashuhudia, na iwe hivyo.