Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,488
- 13,608
Kuna mtu mmoja shombe shombe (chotara/zero point five), yeye ni mmoja wa watu wenye ushawishi ndani ya klabu ambayo zamani iliitwa Sunderland. Huyu mtu ni mmoja wa wadau muhimu wa sekta ya usafirishaji, ni mmoja wa wamiliki wa magari makubwa yanayopeleka mizigo katika nchi jirani.
Wakati wa awamu ya nne aliingia kwenye mzozo na aliyekuwa waziri wa barabara, akafikia hatua ya kuongea kwa dharau akisema kwamba yeye haongei na mbwa bali anaongea na mmiliki wa mbwa, ilibidi aliyekuwa waziri mkuu aingilie kati na kuutatua ugomvi ule.
Mungu si athumani siku za kuishi huwa zinakwenda kasi sana, leo hii yule aliyeitwa mbwa ndiye mwenye mbwa, na ana sauti ya juu kabisa na yenye mamlaka.
Shombe shombe yupo kwenye wakati mgumu, kwani huyu mwenye mbwa wa sasa, anafahamu fika dharau aliyokutana nayo wakati akiwa kazini katika wizara ya barabara.
Nyeti zinahabarisha kwamba mwenye mbwa yupo njiani kuandaa mapigo yatakayorudisha heshima aliyoipoteza baada ya kudharauliwa mpaka kufananishwa na dogi.
Somo muhimu kwa shombe shombe na wengine wote wenye kupenda kuropoka hovyo bila ya kuitazama kesho inafananaje, ni kwamba mdomo ulikiponza kichwa.
Wakati wa awamu ya nne aliingia kwenye mzozo na aliyekuwa waziri wa barabara, akafikia hatua ya kuongea kwa dharau akisema kwamba yeye haongei na mbwa bali anaongea na mmiliki wa mbwa, ilibidi aliyekuwa waziri mkuu aingilie kati na kuutatua ugomvi ule.
Mungu si athumani siku za kuishi huwa zinakwenda kasi sana, leo hii yule aliyeitwa mbwa ndiye mwenye mbwa, na ana sauti ya juu kabisa na yenye mamlaka.
Shombe shombe yupo kwenye wakati mgumu, kwani huyu mwenye mbwa wa sasa, anafahamu fika dharau aliyokutana nayo wakati akiwa kazini katika wizara ya barabara.
Nyeti zinahabarisha kwamba mwenye mbwa yupo njiani kuandaa mapigo yatakayorudisha heshima aliyoipoteza baada ya kudharauliwa mpaka kufananishwa na dogi.
Somo muhimu kwa shombe shombe na wengine wote wenye kupenda kuropoka hovyo bila ya kuitazama kesho inafananaje, ni kwamba mdomo ulikiponza kichwa.