Naona aibu

Naona aibu

Nyamuleha jr

Senior Member
Joined
Feb 20, 2013
Posts
185
Reaction score
65
Nimemaliza digri 2013 Baada ya kukaa dar mda mrefu kusaka ajira bila mafanikio nimeamua kurudi home, nimewakuta wale tulio soma nao lasaba wametoka kimaisha wamejenga, wanauhakika wa maisha tofauti na mimi ambaye sinahata ela ya vocha, nimekuta watu wamejiingiza sana kwenye biashara ndogo ndogo mbao, ufugaji wakuku, mwezi sasa umekatika watu wananishauri jiingize kwenye hizi biashara ndogo sasa naona noma kweli inshu ambazo ningefanya nikiwa la saba sasa nizifanye nikiwa nimemaliza chuo kikuu, kwanza nahisi nitawakatisha hawa madogo tamaa ya kusoma, nikama nilisha kuwa juu sasa nimerudishwa chini kwenye matope kabisa. Hapa naona bora niende mbali ambapo sijulikani nikafanye izo inshu, au nifanyaje?
 
Kusoma ni kusoma na kuna tofauti kubwa ya aliyesoma na siyesoma
Ufugaji utakaoufanya wewe utakuwa tofauti na ufugaji wa mwengine,
Usivunjike moyo hayo ni maamuzi tu, na wala usidharau kazi ya halali, elimu yako sio elimu kama hutotumia maarifa kujiendeleza kutokana na elimu yako
 
Acha kujistukia wewe.
Achana na mawazo mgando hayo,chagua mradi mmojawapo hapo uanze nao ASAP tena usipuuze ushauri wa hao wenzio wazoefu kisa tu wewe una degree.
Elimu ulionayo itakusaidia kuifanya hiyo shughuli kwa ufanisi,utatunza vizuri mahesabu yako na utashangaa baada ya muda mfupi watakufata kukuomba ushauri.
 
elimu ya tanzania sio kazi za kujitegemea ni ya kukariri ndo maana umekasirika sana mpaka umechanganjikiwa but by the way fanya maamuzi ya kitu kimoja kama ni kufuga kuku au ni chochote plus your degree mambo swafi sana ..... tuko pamoja mkuu
 
Usiache elimu uliyopata ikakutumia, ITUMIE!
 
Pole sana kijana!
livue kwanza koti la inferiority then haraka sana daka fursa hizo. Wenzio tulikataa utumwa ktambo na sijivungi kupga kazi yoyote ila naitendea haki elimu yangu ktk kila nifanyalo.
 
Chasha wherever you are tafadhali naomba uje umsaidie kijana mwenzetu huku.
Mimi nahisi nitaandika hapa hadi vidole vitauma sidhani kama mdau atanielewa.
 
Last edited by a moderator:
Chasha wherever you are tafadhali naomba uje umsaidie kijana mwenzetu huku.
Mimi nahisi nitaandika hapa hadi vidole vitauma sidhani kama mdau atanielewa.

pamoja na kumaliza degree ila nilirudi shambani kulima na sahv naanza kutoka
 
Yaani umenisikitisha sana. Itakuwa elimu yako haijakusaidia kujikomboa kifikra...huku tuliko serikalini hakuna kitu kabisaaaa..chukua fursa hiyo
 
You are in an opportunity you must not loose.
Jiandae kisaikolojia kutumia wako wote kutengeneza hela badala ya kuhangaika kutafuta mteja atakayenunua muda wako halafu akulipe laki 5 kwa mwezi.
Nakushauri tumia hiyo fursa
 
Nyoote mmempa moyo,mia nampongeza kwa kuwa muwazi namna hii.
Watu kama hawa wapo wengi sana mitaani,wengine na masters zao kisa aibu.
Ningeomba pia kutambua kwamba mradi au biashara yoyote pia ni kipaji.

Kwanza tambua kwamba mfumo wa ujana wa zamani na sasa ni tofauti sana.Degree hizi haziogopwi tena,maana vijana wameisha zi challenge na kuona tija yake ni ndogo sana kwa wenzao wakija katika maisha ya kawaida.

Pili kama unaanzisha na unaingia kwenye hiyo biashara au mradi wowote lazima ukubali kwamba hao vijana ndio wawe waalim wako.
Wengi wamesema kwamba Elim yako itakusaidia sana kwenye hizo kazi mie sikubaliani nao kabisaaa.
Ni kwamba Elim yako na wao zitakuwa sawa na wanaweza kukuacha kitaaluma pia hata kama wameishia Darasa la saba.
Miradi mingi ya vijana wa sasa sio kama ile ya zamani kwamba miaka inaenda watu wapo na akili na uzalishaji uleule.
Siku hizi kuna Taasisi nyingi sana binafsi na za kiserikali na nyingine kutoka nje ya nchi zimewesha vijana hawa,na nyingi kila mwaka wanatoa mafunzo kwa vijana na wengine mpaka kusafirishwa nje ya nchi na hilohilo Standard seven lao.
Sasa hapo unakuta mfano taaluma ya ufugaji ya chuo kikuu mtu anayo mtaani kulingnana na mazingira na mafunzo ya kila mwaka,sasa wewe utakuja najipya lipi ?
Wakati wanapewa mafunzo ya kuanzisha miradi,kuundeleza kutafuta masoko na chanmgamoto zote za biashara husika.

Hapa kubali matokeo kwamba wewe jione kama wao tu,kisha upate ujuzi kutoka kwao uendeleze maisha,na sio kwamba wewe ndio utafanya miujiza mikubwa sana kupita wao hilo usijidanganye kwa elim yako.

Utakuta Darasa la saba huyohuyo kapata mafunzo anakupa somo mpaka unabakia umeganda,na kila mwaka kichwa kinangiza mapya.

Badilika na chukua Hatua
 
ni wakati sasa serikali iweke somo la economics, finance and entrepreneurship liwe la lazima kuanzia ngazi ya advanced level mpaka degree ya kwanza...

hapa angalau vijana watasaidiwa kujikwamua na tatizo kama hili!

wengi wetu tunapata government loans lakini tunazitumia vibaya vibaya tu, at the end ukihitimu elimu yako unaishia kutanga tanga na kuomba misaada ya nauli...

hata kuwaza namna ya kujiajiri kwa mtu wa undergraduate kweli unashindwa???... hmm!
 
Hii yote imetokana na mitaala mibaya ya elimu yetu ya tanzania.
Mwanafunzi anafundishwa kukariri majibu ya mtihani ili apete 'A'.
Matokeo yake wasomi wana graduate wakiwa hawaja elimika.

Kila nikisoma posts za wasomi wetu waliomaliza vyuo mbali mbali wanavyolalamika kusota miaka kadhaa wakisaka kuajiriwa huwa nasikitika sana.
 
Chasha wherever you are tafadhali naomba uje umsaidie kijana mwenzetu huku.
Mimi nahisi nitaandika hapa hadi vidole vitauma sidhani kama mdau atanielewa.

Mkuu hilo ni tatizo kubwa sana na inauma sana, ndo elimu ya Tanzania hii, kweli ni Tatizo sana na si kwa jamaa tu bali ni kwa vijana wote.

Bwana mdogo anatakiwa yeye mwenyewe kuchagua kunyoa au kusuka, ni lazima achukue maamuzi magumu kwa faida yake nisi kubakia kusema o watanicheka,

Kama anaona ni aibu kwake basi aondoke huko au aendelee kusaka kazi ambazo yeye anaona ndo heshima kwake, kwa sasa tunaelekea kwenye wakati mbaya sana ambapo itatubidi tu tuingie kwenye ajira binafisi make ndo optional pekee iliyo bakia.

So Bwana mdogo anatakiwa achukue uamuzi mgumu sana, anatakiwa kuweka pamba masikioni, anatakiuwa kuvaa miwani ya mbao, na hapo atafanikiwa kusonga mbele.

Kuhusu biashara, huwa tunazani biashara ya heshima ni kuuza magari used kutoka Japani, biashara zote zilianza ndogo Bwana mdogo anatakiwa kusoma historia za wakina Aliko Dangote, Muguku na wengineo, Mtu kama Muguku alianza na kuku 6 but alikuja kuibuka na kuwa kati ya bilionare 5 wakubwa kabisa nchini Kenya.

Aina ya biashara si tatizo ila tatizo ni kwamba anayo spriti, yuko willing? yuko commited, bila kuwa na haya hata tungetoa ushauri wa aina gani ni kazi bure
 
Nimemaliza digri 2013 Baada ya kukaa dar mda mrefu kusaka ajira bila mafanikio nimeamua kurudi home, nimewakuta wale tulio soma nao lasaba wametoka kimaisha wamejenga, wanauhakika wa maisha tofauti na mimi ambaye sinahata ela ya vocha, nimekuta watu wamejiingiza sana kwenye biashara ndogo ndogo mbao, ufugaji wakuku, mwezi sasa umekatika watu wananishauri jiingize kwenye hizi biashara ndogo sasa naona noma kweli inshu ambazo ningefanya nikiwa la saba sasa nizifanye nikiwa nimemaliza chuo kikuu, kwanza nahisi nitawakatisha hawa madogo tamaa ya kusoma, nikama nilisha kuwa juu sasa nimerudishwa chini kwenye matope kabisa. Hapa naona bora niende mbali ambapo sijulikani nikafanye izo inshu, au nifanyaje?
kijana mbona hata ujamaliza mwaka tokea umalize,,suala la ajira rasmi linahitaji uvumilivu,,na kusoma siyo kigezo cha wew kuchagua kazi wakati kazi unayoichagua wenzako wanalelea nayo familia,,kua na subira na uvumilifu,,na usichague kazi alimradi tu unajua unafanya kwa madhumuni gani,,
 
Usiogope kukaa hapo nyumbani na ukafanya wanayofanya wengine. Hakuna utakayemkatisha tamaa, you have your own life hapo kijijini mwenye vision ya kusoma ataifanikisha bila hata ya kumwangilia mtu mwingine. Wewe mwenyewe ni circumstance tu ndiyo iliyokufikisha hapo sidhani kama kuna mtu hapo kwenu ndiye aliyekufanya upate nguvu ya kusoma degree. Pia sidhani kama wewe hapo kwenu ndio mwenye degree pekee na kwamba watu wataidharau degree yako kwa kufuga kuku. Actually ukikaa bila kufanya chochote ndipo watakudharau zaidi. Ingia kazini kama unaweza kufuga kuku, fuga. Mimi nilitafuta kazi kama wewe kwa miaka miwili, na kuku ndio walionifanya sasa nisipende kazi ya kinyangarika chochote. Utatoka tu. hata kama sio kuku. fanya chochote kwa juhudi, usomi ubakie kuwa chachandu tu. vingine vyote nguvu zako. Acha unyonge.
 
Kaka elimu c kigezo bt plan yako ya maisha ndo msing wako wa kutoka!ukiweka plan mbovu utakuwa wa kulalamika kila cku cha msingi jifunze toka kwa wenzako waliofanikiwa changanya na ujuz wa chuo kikuu Mungu atakuongoza!
 
Naona hii post watu wameipenda kweli na ushauri wenu umenipeleka level nyingine, bora zaidi.
Nataka ni wambie hii ni day one yakuanza kutekeleza.:-
kwanzia nifike home nimekuwa mtu wa kujificha tu home nikitoka naenda town tu mara moja nachukuwa gazeti narudi home, ila bado kuna changamoto ya maneno hasa sisi tulio soma social sciences, utasikia sasa umesoma kozi gani hiyo, sosholoji, pltc science, ndiyo maana hupati ajira . Kuna wadau wameniambia fahari ndiyo baba waujinga watafute haohao walasaba ambao wamefanikiwa ukubali wawe walimu wako, nasema asante kwahilo., ngoja nianze kutafuta slide za enterprenueship nipate elimu zaidi.
 
Naona hii post watu wameipenda kweli na ushauri wenu umenipeleka level nyingine, bora zaidi.
Nataka ni wambie hii ni day one yakuanza kutekeleza.:-
kwanzia nifike home nimekuwa mtu wa kujificha tu home nikitoka naenda town tu mara moja nachukuwa gazeti narudi home, ila bado kuna changamoto ya maneno hasa sisi tulio soma social sciences, utasikia sasa umesoma kozi gani hiyo, sosholoji, pltc science, ndiyo maana hupati ajira . Kuna wadau wameniambia fahari ndiyo baba waujinga watafute haohao walasaba ambao wamefanikiwa ukubali wawe walimu wako, nasema asante kwahilo., ngoja nianze kutafuta slide za enterprenueship nipate elimu zaidi.
mkuu, ushapata initial capital...?
 
Back
Top Bottom