Naombeni mwongozo


exactly! that's a very decent solution.
 
pole mwaya kwa mdada wa kwanza wa kazi hapo home
ninachoomba cha kufanya mketishe chini muelezee kinagaubaga wa
wewe unapomwachia hela ya voucher kuwa ni matumizi ya kinyumbani
na si kibinafsi yake , muelezee kuwa unapo;pigia ujue kuna kitu unataka
kufahamu happo nyumbani pakoje na mambo ya dharula kiujumla akufaahamishe

vilevile mtengenezee jedwari au ratiba kamili ya mzungumko wa voucher zako
uzitoazo hapo home kuanzia tarehe 1-30 ili ujue unatoaga voucher ngapi na za
shilingi ngapi kwa matumizi ya home kwako

labda ratiba hii ambayo ni demo itakusaidia namna ya kuweza kumpangia bajeti za voucher
hapo home kwako bestito

HUU NI MFANO TU KAMA WAWEZA KUCHUKUA CHUKUA AU VYYOVYOTE BEST

Na Matumizi ya Voucher siku mwezi jumla ya mwezi
1 VOUCHER NGAPI KWA SIKU MWEZI YOTE

 
Rafiki baadhi ya Wababa wako tofauti. Wanajua fika kwamba Mama mwenye hawezi kufuatilia mambo ya pale nyumbani 24/7 hivyo nao husaidia ili kuhakikisha huyo msaidizi waliyemfungulia milango na kumkaribisha nyumbani kwao ni mtu salama na anafuata taratibu zote za pale nyumbani na kama Baba mwenye nyumba ataliona lolote ambalo halitamfurahisha basi anaweza kujadiliana na mwenzie ama lirekebishwe au kuamua kuachana naye.

Msaidizi wa nyumbani tajiri wake anaweza kuona anamthamini sana kwa vitu mbali mbali ambavyo humfanyia ikiwemo kula chakula kizuri cha pale nyumbani, kupewa pesa, kulala mahali pazuri n.k. lakini kwa huyo msaidizi jambo kama la kuzuwiwa kuongea na nduguzake akaliona kubwa sana na kusahau mengine yote hivyo kuwaambia watu "Yule mama ana roho mbaya sana hataki niongee na ndugu zangu."

Ubahatike uwe na yule ambaye ataamua kufunga virago kwa kutokubaliana yeye kutoongea na ndugu zake, lakini mwingine anaweza kusema "Huyu mama mwenye nyumba yake na roho mbaya yake ngoja nimkomoe." Akaenda kununua gudulia la mafuta ya taa akasubiri watoto wamelala ndani akatia kiberiti nyumba yote au akatayarisha msosi na kutia sumu ya panya (Mungu apishilie mbali)

Hawa watu wengi wao wana matatizo mbali mbali lakini tunapoamua kuwafungulia milango ya majumbani mwetu basi tuwe karibu nao sana na kuwaona kama ni ndugu zetu hivyo kutowawekea sheria nyingi ambazo hatuwezi kuwawekea ndugu zetu kwa usalama wa wenye nyumba, watoto wao na mali zao.

Good day 🙂🙂🙂
 

Hujaelewa bado. hiyo 1000 ni kwa ajili ya emergency tu. kama akitaka kupiga simu kwa ndugu zake atawekewa airtime atapiga. hakuna mtu aliyesema kwamba anamnyima beki 3 kupiga cm kwa ndugu na jamaa zake.

na kama 1000 ikitumika ikaisha leo ataongezewa nyingine papo hapo--1000 haiko FIXED!
 

hakuna mtu anayetaka kuwanyanyasa hawa beki 3 hata kidogo--sote tunaishi nao kiundugu na kirafiki. tunachojaribu kuongelea hapa ni JINSI GANI YA KUWA-SHAPE ILI WAWE NA MATUMIZI SAHIHI YA RASILIMALI ZA WAAJIRI WAO--hii ndiyo point and there's no one claiming to look baby sitters down his/her nose!!!
 
Asante sana tpaul kwa kunisaidia kuelezea na kujibu hoja, kweli mada imekuingia kisawasawa, nimejifunza mengi toka kwako
 
Last edited by a moderator:
Rafiki yangu BAK, hakuna sehemu nimesema sitaki aongee na ndugu zake..... aongee nao tu any time, sina shida na hilo.
Sijui naeleweka hapa au la; huyu mtu nampa 1000 kwa wiki kwa ajili ya kunipigia endapo dharura itatokea nyumbani, ni kiasi cha kutoa taarifa tu. Siku hizi bongo simu ni very cheap kupiga, yaani mimi hata sms naonaga uvivu kutuma. napiga kwenye mtandao wowote, muda wowote, ni cheap sana. huyu mdada anaweza kaa mwezi mzima asinipigie simu ya dharura, inawezekana hata miezi mi3 au mi4, kila siku huwa anapokea tu simu zangu. lakini sasa ikija tokea kumetokea dharura na anahitaji kuwasiliana nami anasema hana airtime, unadhani hiyo ni fair?
Kuhusu wababa kusaidia kuangalia wadada endapo mama hayupo hilo halina mjadala, wababa wote wanafanya hilo. Ila naweza kukushangaa sana rafiki mkeo yupo sitting room wewe upo busy kumwelekeza dada jinsi ya kufanya kazi pale nyumbani, utakuwa unafanya kazi si yako.
Have a good day as well:smile-big::smile-big:
 
Last edited by a moderator:
Reactions: BAK
natamani hii pia ionwe na BAK na Eiyer
Asante sana kwa ufafanuzi huu
 
Last edited by a moderator:
Reactions: BAK
Hahahahaha lol!!!! Rafiki kwenye hili bado msimamo wangu haubadiliki. Tunazungumzia usalama wa familia kwa jambo dogo sana ambalo msaidizi anaweza kabisa kuamua kuipoteza familia nzima au kuiacha na majonzi makubwa sana. Pia simaanishi msaidizi atumie tu financial resources za familia hovyo hovyo kitu ambacho hata ndugu hatuwezi kumruhusu. Ninachosema ni kuwa flexible ili hawa wenzetu wasijione wanabaguliwa na hivyo kuhatarisha uhai na mali za familia au kutafuta mwingine kila baada ya miezi michache baada ya kushindana.

natamani hii pia ionwe na BAK na Eiyer
Asante sana kwa ufafanuzi huu
 
mfundishe huduma ya tafadhali nipigie...mpe mazoezi ya kufanya hivyo angalau mara moja kwa siku....

hata mi nilitaka kumshauri hivi huyu bi dada--na badala ya kumfundisha formula hiyo asevu jina lake kwa kabisa ili kwamba beki 3 akipiga jina lake apokee ujumbe wa pls call me.
 
ukimuunganishia hv ndio ataacha kazi zote atakaa kupiga cm cku nzima! wewe beki 3 huwajui vzr eeh?

Kwani beki 3 hawafai kuwa na social lives? Kuwa na marafiki?

Utamfungia hadi lini?
 

simu la MKONGE? hahaha! mkuu umenichekesha sana! hata mi nalitamani.
 
Rafiki umeshamjua huyu tabia yake kwamba hakupigii hata kuwe na dharura, hivyo kila saa moja tafuta dakika tano tu za kumpigia ili kujua hali nyumbani iko shwari. Mama mwenye nyumba hawezi kuwepo nyumbani 24/7 anaweza kuwa amesafiri kikazi, kwa dharura kama msiba, ugonjwa n.k. Hapo baadhi ya Baba wenye nyumba huamua kufuatilia shughuli za msaidizi ili kujua kila kitu kiko shwari wakati mama mwenye nyumba yuko mbali na nyumbani. Hili la wasaidizi kuikomoa familia limetokea mara nyingi tu sehemu mbali mbali nchini na hata duniani. Hivyo ni vizuri kuhakikisha kila siku iendayo kwa Mungu familia iko salama. Nimeliona dongo lako Hahahahaha lol! Nikabaki natabasamu tu 🙂🙂🙂

 
Kwani huzijui? corporate organisations wanatumia mobile lines za voda, tigo na airtel kama simu za mezani. Si unajua ttcl ilishazimia?
simu la MKONGE? hahaha! mkuu umenichekesha sana! hata mi nalitamani.
 
Bahati mbaya hata ujui mada ipi ya kutoa povu ila kwa kuwa umejua kusema neno hilo basi unalitumia hata mahali ambapo halina haja,mfano wako ulioutoa mbona haulingani na mada iliyopo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…