Naombeni msaada nimechanganyikiwa

Naombeni msaada nimechanganyikiwa

Wasalaam wana JF, mimi binti Nina tarajia kuwa tabibu hivi karibuni. Ila Nina tatizo Fulani, nina mchumba muislam na mimi ni mlokole, tunapendana sana lakini wachungaji wangu hawamtaki kabisaaa.

Nachanganyikiwa wanadai nimuache, tutafanya maombi nitapata mlokole mwenzangu wananiambia biblia inasema "msifungiwe NIRA na MTU asiyeamini" na MTU asiyeamini ni yule ambaye hajampokea YESU kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake na haamini kifo cha msalaba, ila wazazi wetu wote hawanashida sasa nifanyeje niko njia panda.

Kama nimekosea undishi mnisamehe sana naombeni mchango wenu

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
NB. Huyu mtu nimeanza mahusiano nae kabla sijaokoka na nimeokoka ukubwani
Kwangu Dini na Dhehebu ndiyo kigezo cha Kwanza
Siyo lazma wewe ubadili dini au wewe ubadili dini kama mmoja hajaridhia mwenyewe
Nina imani hata mkiachana Huko kanisani utapata Mme na Yeye huko Msikitini atapata Mke
Haya Makanisa ya Kilokole na Jamii husika huwa Wanatowa adhabu ya Kumtenga Mfuasi wao kama tu
i.akipata mimba kabla ya ndoa
ii.akiolewa uislamu
iii.wanaingilia sana familiya yako ,yani kama wewe binti umeolewa na Mme wa dhehebu kama RCC ,AC na KKKT .

Lakini Pia ktk upande wetu wa pili sisi Muslim's tunamini asiye amini na kuwa Muslim basi yeye si Msafi na ni Khafiri
Sasa ikitokea umeowa binti wa kilokole lazma jamii yako husika itakupa maana umeowa Khafiri , kwa hiyo lazma aslimishwe ili maadili ya Uislam yakamilike
Je Yule binti alikotoka ktk jamii yake mwanamchukuliaje ?

Mimi binafsi naona tusijiendekeze sana kusema dini siyo kigezo , kiukweli kuishi dini tofauti kuna changamoto kubwa japo hata mkiwa dini moja napo kuna changamoto ila naomba uhamini zimetofautiana .

( ni mawazo yangu na si mawazo ya kiitikadi ya udini )

Sent from my itel it1556 Plus using JamiiForums mobile app
 
Nyie walokole kuoa ama kuolewa si mpaka uoteshwe na bwana!?

Sent from my TECNO_W4 using JamiiForums mobile app
 
Sasa kama wazazi hawana shida.. Huyo mchungaji inamuuma nin?

Sent from my TECNO-C5 using JamiiForums mobile app
Mchungaji anataka apewe kondoo yake, aichinje mwenyewe

Hii Simu Sio Ile, Hii Ni Hii
 
Wasalaam wana JF, mimi binti Nina tarajia kuwa tabibu hivi karibuni. Ila Nina tatizo Fulani, nina mchumba muislam na mimi ni mlokole, tunapendana sana lakini wachungaji wangu hawamtaki kabisaaa.

Nachanganyikiwa wanadai nimuache, tutafanya maombi nitapata mlokole mwenzangu wananiambia biblia inasema "msifungiwe NIRA na MTU asiyeamini" na MTU asiyeamini ni yule ambaye hajampokea YESU kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake na haamini kifo cha msalaba, ila wazazi wetu wote hawanashida sasa nifanyeje niko njia panda.

Kama nimekosea undishi mnisamehe sana naombeni mchango wenu

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
NB. Huyu mtu nimeanza mahusiano nae kabla sijaokoka na nimeokoka ukubwani

See my comment in RED BELOW:

Wasalaam wana JF, mimi binti Nina tarajia kuwa tabibu hivi karibuni. Ila Nina tatizo Fulani, nina mchumba muislam na mimi ni mlokole, tunapendana sana lakini wachungaji wangu hawamtaki kabisaaa.

SIKU ZOTE UMEKUWA MLOKOLE, WACHUNGAJI WAKO NI WALOKOLE, MMESHIRIKIANA NAO KWA MTAZAMO WA KILOKOLE, LEO UNATAKA WAKU SUPPORT KUOLEWA NA MUISLAM? HISIA ZIMEKUZIDI UMEACHA AKILI MAHALI KWINGINE DADA YANGU.

Nachanganyikiwa wanadai nimuache, tutafanya maombi nitapata mlokole mwenzangu wananiambia biblia inasema "msifungiwe NIRA na MTU asiyeamini" na MTU asiyeamini ni yule ambaye hajampokea YESU kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake na haamini kifo cha msalaba, ila wazazi wetu wote hawanashida sasa nifanyeje niko njia panda.

WAZAZI WAKO SIJUI NI DINI GANIA NA SITAKI KUJUA, ILA WEWE UMEKUWA WAENDA KWA WALOKOLE, INA MAANA ULIAMINI ULOKOLE, WEWE NDIO UTAISHI NA HUYO MWISLAMU, NA SIO WAZAZI WAKO, MI NINAKUHAKIKISHIA KITU KIMOJA KWAMBA: FURAHA YA NDOA IPO ZAIDI KWENYE KUISHI, SIO HISIA YA KUOLEWA ..... HAPO MUNGU NA IMANI SIO KIPAUMBELE TENA, KIPAUMBELE CHAKO NI KUOLEWA, MAISHA YA NDOA NDUGU YANGU KWA IMANI TOFAUTI WATOTO MWAWALEAJE?

Kama nimekosea undishi mnisamehe sana naombeni mchango wenu

MIMI NISINGEOLEWA NA MWISLAMU HATA SIKU MOJA KAMA NI WEWE, ILA NA WEWE MPAKA MNA DATE MWAANZA UHUSIANO SIJUI IMETOKEAJE, MIMI NAKUPA 95% YA KUTOFURAHIA NDOA YAKO, UTANISAMEHE LAKINI MIMI NDO MTAZAMO WANGU, JIPANGE UPYA, WASIKILIZE VIONGOZI WAKO WA IMANI.

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
NB. Huyu mtu nimeanza mahusiano nae kabla sijaokoka na nimeokoka ukubwani

OH, NDO NIMEIONA HII, KAMA UNAAMUA KUACHA IMANI NA KUOLEWA NAYE, NI SAWA, ILA USIJIDANGANYE KUOLEWA NAYE NA KUSEMA BADO UMEOKOKA, WAWEZA JIRUDI BAADAYE, BUT NOTE: NDOA NI VERY SERIOUS COMMITMENT, SIO KITU CHA MAJARIBIO DADA YANGU.
 
Funga na kuomba kwa imani thabiti katika roho na kweli kwaajili ya hilo Mungu atakuoneshea njia iliyosahihi

Sent from my TECNO-J8 using JamiiForums mobile app
Asante sana

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
 
See my comment in RED BELOW:
Thanks alot those words are so useful to me. Ubarikiwe sana

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
 
Nilitamani sana kuja inbox but kwa kua umenielewa then sina sababu ya kuja. Nakutakia maisha mema ya maamuzi.
Karibu mkuu kama unalolote Niko tayar kupokea usihofu

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
 
Karibu mkuu kama unalolote Niko tayar kupokea usihofu

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
Nitakuja, ngoja nitulie cause baadhi ya mambo hushauliana na mtu ANA kwa ANA kuliko jukwaani humu.
 
  • Thanks
Reactions: THT
swali jepesi cyo wachungaji wako coz wachungaji wako hawatakuja ku solve matatizo ya ndoa yako hapo badaye ishu ni kuwa wewe mwenyewe umeridhia kubadili dini maana ucje jidanganya mvulana eti atabadili akufuate kama atafanya hivyo atafanya kwa kipindi kifupi tu cha kufunga ndoa yenu baada ya ndoa sahau hiyo kitu swala gumu litbaki pale mtakapo zaa watoto maana mtawachanganya kwenye imani wasali/ waswali hapo ndo ndoa za hivyo zinakuwa ngumu ndo maana watu wanashauri ufanya maanzi kbla ya kukurupuka kwa kuangaria mihemko ya moyo tumia akili sana kuliko kuckiliza moyo.
 
  • Thanks
Reactions: THT
Asante sana

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app

Napinga issue ya kuomba hapa, it is so clearly kwamba ulipookoka na kuamua kumfuata Yesu ulipaswa kuacha vitu vyote nakumfuata, including of Mchumba, usiombe kuonywesha njia na Mungu, this is sooooooooooooooo open .... don't even waste you time, kama ni kuomba, OMBA MUNGU akupe Neema muachane kwa amani bila maumivu .... KUMWACHA NI LAZIMA kama unaamini unataka kuwa bado kwenye imani, huitaji kuomba.
 
Mambo mengine bana .
Sa upo tayari kuwa mwislamu, je mpenz wako yupo tayari kuwa mkristo? Hapa utachukulia poa tu ila ugumu utauona badae. Kama uliamua kuokoka waislamu kwako ni sawa n waovu pia kwa iman y mchumba wako we ni kafiri ,ili kuyaepuka hayo nin nyie wawil kuwa katik njia moja. Mwisho niseme tu kuwa Maamuz unayo ww

Sent from my Halotel H8401 using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: THT
Msichana aliyeokoka hawezi hata kumuangalia muislam? acha uongo bhana mbona mi nawakaza sana watoto wa kilokole ss we kwa akili yko unadhani namkazaje bila kuniangalia usoni?

Sent from my TECNO-C7 using JamiiForums mobile app

Mkuu;
Hivi ukiambiwa kuwa kuna msichana mjahidina anakazwa hovyo chooni kila mwanamume anajitwalia utaonaje? Nadhani wazo lako la kwanza ni kuwa; Tumtangazie 'Fatwah". Hivyo msichana wa kilokole unaye mkaza kama ulivyosema, huyo kwetu tushamtangazia fatwah.
 
Kwangu Dini na Dhehebu ndiyo kigezo cha Kwanza
Siyo lazma wewe ubadili dini au wewe ubadili dini kama mmoja hajaridhia mwenyewe
Nina imani hata mkiachana Huko kanisani utapata Mme na Yeye huko Msikitini atapata Mke
Haya Makanisa ya Kilokole na Jamii husika huwa Wanatowa adhabu ya Kumtenga Mfuasi wao kama tu
i.akipata mimba kabla ya ndoa
ii.akiolewa uislamu
iii.wanaingilia sana familiya yako ,yani kama wewe binti umeolewa na Mme wa dhehebu kama RCC ,AC na KKKT .

Lakini Pia ktk upande wetu wa pili sisi Muslim's tunamini asiye amini na kuwa Muslim basi yeye si Msafi na ni Khafiri
Sasa ikitokea umeowa binti wa kilokole lazma jamii yako husika itakupa maana umeowa Khafiri , kwa hiyo lazma aslimishwe ili maadili ya Uislam yakamilike
Je Yule binti alikotoka ktk jamii yake mwanamchukuliaje ?

Mimi binafsi naona tusijiendekeze sana kusema dini siyo kigezo , kiukweli kuishi dini tofauti kuna changamoto kubwa japo hata mkiwa dini moja napo kuna changamoto ila naomba uhamini zimetofautiana .

( ni mawazo yangu na si mawazo ya kiitikadi ya udini )

Sent from my itel it1556 Plus using JamiiForums mobile app
Hiyo ni kweli kabisa, mnaweza ishi vizuri siku mkigombana kila mtu anawaza imani yake ya zamani usiombe ukahama RC kisha ukarudi utapigishwa magoni mlangoni kila jpili tena mlangoni mwanzo wa ibada mpaka mwisho bado kuongea mle ndani

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Kweli mkuu sometimes usipotumia hekima unaeeza kupotea

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
Asante kwa kunielewa mambo kama hayo yanawapata wengi san kabla kuchukua hatua omba Mungu utapata amani, vishawishi huja wakati umesimama na Bwana kwanini asingekuja wakati hujamjua Mungu kwa undani omba amani na rehema utaponywa.

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Dada yangu alidondoka hapo ! Mambo yakuendekeza Moyo kuliko facts. Maisha ya kiislam ili uyaweze lazima uukubali uislam! Bila kuukubali hutaweza kuendana nao.
Ni hivi dada alikacha familia akaslim sio kwamba aliukubali uislam ila alifanya ili asitengane na ampendaye! Akaolewa, Maisha yanaanza mama wa kiislam! Mziki hauchezeki, masharti hayabebeki, Shemeji mstaarabu ila ndio anasisitiza mkewe lazima aishi kiislam, Dada anajitahidi lakini kwa sababu sivyo alivyokuzwa ni mateso!
Hapo hakuongezewa mke -angezimia kabisa. Alivumilia lakini alishindwa.
Kama unadhani unaweza kuvaa viatu vya mke kwa maadili ya kiislam sawa. Kama huwezi wakati ni sasa ! Chukua hatua

Sent from my SM-J200H using JamiiForums mobile app
Nimekuelewa sanaa

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
This happened to relative. After more than 4 years they demand him to convert to be muslim. He refused, they took their daughter and the baby off the went. Kuwa makini sana na haya mambo kama ni mlokole. Na ujue kikitoka kibali from both parents huyo ni mke/mume mpka kifo kiwatenganishe hata akioa wake wangapi au akikutaliki bado imani yako inamtambua mmoja tuu mpka afe.
 
Nachelea kuseme ww sio MLOKOLE kabisa ila unasali na sisi.

~Dada Mungu hadhihakiwi hata kidogo na sisemi umemdhihaki hapana maana biblia inasema viache ngano na magugu vikue pamoja ndio km hivi.

~Narudia hujaokoka huijui kweli ww!! tena ungeijua gharama ya msalaba na damu ya YESU y ungetubu mapema sana dhambii haianzii nje huanzia ndani.

~Natamani km nikuhubirie yani kuna kitu kinachemka ndani yangu si cha kawaida.najiuliza una ROHO MTAKATIFU kweli?

~Mimi ni mlokole tena kwa chimbuko dada Mungu anajibu,usisingizie wachungaji ww biblia husomi au zipo tofauti yakwako inaruhusu??

Yeremia 17:5 inajieleza wazi.panda mlimani,hata siku 3 kavu,lia kwa Mungu majibu hayapo Jf yapo magotini mama.Ita jina lipitalo majina yote.

~dada iambie damu inenayo mema kuliko damu ya habiri inene mema juu ya hilo,ingia patakatifu pa patakatifu,kisogelee kiti cha rehema kwa ujasiri.amuru mbingu iachie majibu,fungua madirisha ya hazina iliyo sitirika ohooo jamani kwa YESU raha saaana.

~Nb;MUNGU HAWI RADHI NA WAPUMBAVU.

Sent from my SHV-E250S using JamiiForums mobile app
We kweli mlokole kwa chimbuko...hasa pale nilipoanza kusikia mambo ya mlimani, siku tatu kavu
Umenena vema kama muinjilisti

Lakini nadhani ni vema hata tungejua level yake ya kiroho badala ya kumshauri kimashambulizi kama ambavyo wengi wamemwagika hapa...

Mtume Paulo mwenyewe kuna wakati alinena akijua hapa naongea na watoto wachanga...kuna wakati aliongea mambo magumu akijua anaongea na matured

Unaweza kukuta dada wa watu hana hata mwezi huko wokovuni, sauti ya roho mtakatifu ataijuaje, neno atakuwa amesoma saa ngapi, huko kufunga siku 3 si itakuwa jaribu lingine kwake ikiwa walokole magwiji 24 hrs ni shida

Ebu tumshauri kwa upole jamani

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
Hata simuelewi,natakamani ningemuona face to face nna maswali mengii,haingiii akilini kua wewe mlokole na from day one uko na huyo jamaa am sure jina lake haitwi John wala Hillary umeshindwaje kujua mapema? haya tumuache ajiongeze mwenyewe..
Sio kwamba alisema amekutana naye kabla hajaokoka, aliedit bandiko hakuwa amesema mwanzoni?

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom