NAOMBENI MBINU YA KUPATA WAGONJWA.

NAOMBENI MBINU YA KUPATA WAGONJWA.

ydalnorI

Member
Joined
Mar 21, 2019
Posts
37
Reaction score
26
Wana jamvi wenzangu mimi ni muajiriwa ktk clinic fulani kama meneja fedha wa kituo.
Ninaomba mawazo yenu wakuu kwamba ni njia gani naweza kuitumia kuvuta wateja waje kuhitaji huduma ktk kituo chetu? Je wagonjwa ambao ni wateja wanapendelea kuhudumiwa vipi? Mawazo yenu yatanisaidia kuboresha. Natamani kufanya kwa moyo wangu wote kwa mafanikio ya ustawi wa kituo.
Naomba kuwakilisha , nishauri chochote cha kujenga.
 
daaa, kwa hiyo mkuu mim nikiumwa we we ndio unafurahiaa.daaa dunia haiko fair hii,badala ya kuomba magonjwa yatuepuke wew ndio shavuu.hayaa ngoja wajee
 
Zingatia usafi wa jengo nje na ndani pia usafi wa watoa huduma..

Pili kauli safi zenye kutoa faraja kwa wagonjwa kupitia watoa huduma wako..

Tatu hakikisha maabara yako inatoa majibu sahihi sio kubambikia watu ugonjwa ili upige pesa kupitia vipimo na dawa..

Nne anzisha clinic ya magojwa ya uzazi hasa akina mama coz wana mattzo sana nw days na ukiwapata hao umezipata familia zao pia..

Mengine wataongezea wataalam.
 
Wana jamvi wenzangu mimi ni muajiriwa ktk clinic fulani kama meneja fedha wa kituo.
Ninaomba mawazo yenu wakuu kwamba ni njia gani naweza kuitumia kuvuta wateja waje kuhitaji huduma ktk kituo chetu? Je wagonjwa ambao ni wateja wanapendelea kuhudumiwa vipi? Mawazo yenu yatanisaidia kuboresha. Natamani kufanya kwa moyo wangu wote kwa mafanikio ya ustawi wa kituo.
Naomba kuwakilisha , nishauri chochote cha kujenga.
Afadhali umeongea ya moyoni!
Pharmaceutical industry wanatamani hata kuweka sumu ya kuleta magonjwa ili watu waumwe!
Na ndo sababu pia ukienda hospitali huambiwi sababu ya ugonjwa hata kama ugonjwa wenyewe hupona kwa kunywa maji mengi.
 
Afadhali umeongea ya moyoni!
Pharmaceutical industry wanatamani hata kuweka sumu ya kuleta magonjwa ili watu waumwe!
Na ndo sababu pia ukienda hospitali huambiwi sababu ya ugonjwa hata kama ugonjwa wenyewe hupona kwa kunywa maji mengi.
Pharmaceutical industry ipo kibiashara zaidi..na huo ndo ukweli mchungu.
 
Mgonjwa akija kwako mpe dawa isiyoendana na ugonjwa wake.
Nakuhakikishia wagonjwa wataongezeka
 
binafsi yangu kuni win lazima uwe na DR. sio ma clinical officer namanisha M.D kama hao hawapo kuja kwenye clinic yako ni big No labda niletwe nimebebwa sijitambui.
 
Unatamani kufanya kwa moyo wako wote kwa ustawi wa kituo sio jamii kwa kuisaidia? Uko vizuri mkuu.
Fanya hivi, tengeneza ugonjwa kisha tengeneza dawa yake baada ya hapo ambukiza watu ili wafuate dawa kwako tu kwa ustawi wa kituo.
 
binafsi yangu kuni win lazima uwe na DR. sio ma clinical officer namanisha M.D kama hao hawapo kuja kwenye clinic yako ni big No labda niletwe nimebebwa sijitambui.
Kwa hyo unataka kusema kwamba clinical officers hawana competence hata ya kutibu malaria?
 
Mwenye link ya thread ya wafanyabiashara wa mikoani wanaochukua vitu kariakoo naomba anitag
 
daaa, kwa hiyo mkuu mim nikiumwa we we ndio unafurahiaa.daaa dunia haiko fair hii,badala ya kuomba magonjwa yatuepuke wew ndio shavuu.hayaa ngoja wajee

Mkuu wagonjwa wapo tu hata wasipo kuja hospitalini kwangu. Na nia ya vituo vya afya ni japo tunaugua tukienda kutibiwa tupone.
Pole sana naona umenielewa tofauti.
 
Zingatia usafi wa jengo nje na ndani pia usafi wa watoa huduma..

Pili kauli safi zenye kutoa faraja kwa wagonjwa kupitia watoa huduma wako..

Tatu hakikisha maabara yako inatoa majibu sahihi sio kubambikia watu ugonjwa ili upige pesa kupitia vipimo na dawa..

Nne anzisha clinic ya magojwa ya uzazi hasa akina mama coz wana mattzo sana nw days na ukiwapata hao umezipata familia zao pia..

Mengine wataongezea wataalam.

Mungu akujalie ndugu yangu asante kwa ushauri wako mzuri sana , nitautekeleza.
 
binafsi yangu kuni win lazima uwe na DR. sio ma clinical officer namanisha M.D kama hao hawapo kuja kwenye clinic yako ni big No labda niletwe nimebebwa sijitambui.

Umeongea jambo usilo lijua tena ni wazuri sana huwezi amini sometime kuliko hata hao MD maana wao wako huku ground they meet many and consult many. Sijui nikwambie kwa mfano upi unielewe.
 
Mgonjwa akija kwako mpe dawa isiyoendana na ugonjwa wake.
Nakuhakikishia wagonjwa wataongezeka

Ndugu yangu jiangalie kesho usije ukawa wewe unaletwa msobe msobe hujitambui. Lolote mtakalo mtendewe na nyie watendeeni wengine vivyo hivyo.
 
Wana jamvi wenzangu mimi ni muajiriwa ktk clinic fulani kama meneja fedha wa kituo.
Ninaomba mawazo yenu wakuu kwamba ni njia gani naweza kuitumia kuvuta wateja waje kuhitaji huduma ktk kituo chetu? Je wagonjwa ambao ni wateja wanapendelea kuhudumiwa vipi? Mawazo yenu yatanisaidia kuboresha. Natamani kufanya kwa moyo wangu wote kwa mafanikio ya ustawi wa kituo.
Naomba kuwakilisha , nishauri chochote cha kujenga.
Toa huduma bure wateja watakuja kwa wingi...
 
Back
Top Bottom