SEMBE WA LUSANGA
Member
- Apr 6, 2012
- 97
- 34
Hongera bi mdada kwakufikia umri huo ukiwa bado huyajui mambo ya kikubwa, hapo cha msingi kama unajiaminisha hujawahi kunanihii hata siku moja, mwambie kwa kumbembeleza huku umerembua, '' Honey nimekutunzia TUNU ambayo utaifaidi mara tu baada ya ndoa kufungwa, nakuahidi kuwa kama nilivyojitunza na sijui mwanaume mpaka leo, katu sitamruhusu mwingine aonje TUNU yako, vumilia kwani subira huvuta heri mpenzi, nakupenda sana, pia nionyeshe upendo kwa kuvumilia mpaka siku ile ikifika'' Kisha mbusu kwenye paji la uso halafu akuthibitishie kwamba atavuta subira. Akikubali, mbusu tena kwenye paji la uso kisha muage urudi nyumbani kwani ukikaa sana mizuka itamsumbua, pia mara nyingi jenga mazoea ya kumtembelea ukiwa na eidha rafiki yako au mdogo wako ili pasiwepo mwanya wa ahadi kuvunjwa.:cheer2: