- Thread starter
- #61
Nimekuelewa, bahati nzuri,Unafikira simple ila siyo hivyo.
Una mke kwenye uzee huwezi kuwa huyu huku huyu huku.
Mi nilihamia huku na mtoto tu kivulana cha jirani hata wanangu walikataa, baadaye kidogo binti yangu kanifuata.
Nyumba mjini zipo ila huku niliwahi let say five years before retirement, nikawa naenda job kutoka huku shamba, kila siku nauli ilikuwa elfu kumi, ila nilipenda nizoee mazingira.
Wakati huo niko na separation ya more than fifteen years, ila ndoa ya kikristo ndo hivyo.
Wale vijana wakasema kwa baba yao mama anaishi maporini anariski maisha.
He called me, nikamwambia nipe hela nirudishe mizigo mjini, alishtuka tu hata angenipa nisingerudi mjini.
Anyways ni mambo mengi sana,
Nilishaandaa hayo mazingira ni kipindi sasa toka miaka ishirini iliyopita,
Ni mambo tu ya kusomesha watoto, ila nilikuwa sikauki kijijini, nimezoeleka sana na ninasifiwa kwamba sijapasahau nyumbani kama vijana wengine,
Najua kuna changamoto, lakini nimejipanga kuzikabiri,
Mzee mmoja wa mjini aliwahi kuniambia yeye hawezi kwenda kijijini kwa sababu kuwa ataonewa wivu anamaisha mazuri watamroga,
Halafu msiba ukitokea lazima aende, Hana excuse, hata vijiji ya mbali huko, kwa hiyo akaona hayo hayawezi, Nadhani na changimoto nyingine zipo
