Imenilazimu kufungua akaunti mpya kwa sababu nyingi kidogo. Moja kwa moja kwenye matatizo yanayonisibu, huyu bwana niko naye muda wa miaka karibu minne sasa ila tunakaa mikoa tofauti mimi niko Dar na yeye yuko mkoa mmoja Kusini Mangaribi, naendaga kumtembelea nikipata nafasi na nikiwa huko tunaishi kama mke na mume kabisa.
Yeye kuja mjini mpaka alazimishwe anasema ni kazi inambana yaani nikiangalia maisha yangu na plan zangu za miaka ijayo naona kabisa hapa hakuna cha maana ninachofanya.
Mbali na kutokuwa na imani nae kwenye mahusiano simwoni kama ni mtu mwenye uelekeo wa kufanikiwa, chochote anachopata ni pombe tu. Ananiambiaga plani zake nyingi za maendeleo napata matumaini labda ameanza kupata hamu ya kufanikiwa ila hakuna kitu.
Kila nikamuuliza analalamika kuwa wanawake tuna tamaa, sina tamaa ila nataka na sisi tufike mbali. Marafiki zake wengi wanajielewa na wana kazi nzuri tu, yeye kutwa ni kujisifia tu kuwa anafahamiana na huyu au huyu na kwamba amesoma Dar chuo cha mabrazameni na masistadu ila nikimwambia aniconnect nipate kazi huku Dar anaanza kulalamika nirudi mkoani atanilipa hiyo hela ambayo ningepata nikiajiriwa.
Nikiangalia kweli amejenga hapo mkoani ila pia kuna opportunity nyingi zaidi Dar kwanini anang’ang’ania mkoani? Na ameshawahi kusoma na kuishi Dar muda mrefu kwahiyo sio mgeni.
Lingine nikiangalia umri wangu unaenda na yeye wala haeleweki, tayari ana mtoto na mwanamke mwingine na hana interest ya responsibility na huyo mtoto. Nahisi ndiyo alivyo yaani wale wanaume wa kuzalisha watu tu bila mbele wala nyuma.
Kwenye kutomuamini kimapenzi ni kwasababu kila mara anaongea na maex wake nakusema flani bado ananipenda au flani anajuta kuachana na mimi. Yaani ananiboa sana kama wanampenda si aende kwa wao asinipotezee muda. Kuna wakati rafiki yangu aliajiriwa kwenye ofisi flani hapo mkoani nilitaka nimtume kwa siri baa jamaa anazoenda nione kama atamtongoza ila nikaona ni ujinga. Hii ingekuwa njia nzuri ya kumkamata na kuachana nae ila pia nahisi sitakuwa nimetenda haki, nakosa amani jamani sijui nifanyeje?
Na mambo mengi sana nayofikiria ila niishie hapa kwa leo.
Yeye kuja mjini mpaka alazimishwe anasema ni kazi inambana yaani nikiangalia maisha yangu na plan zangu za miaka ijayo naona kabisa hapa hakuna cha maana ninachofanya.
Mbali na kutokuwa na imani nae kwenye mahusiano simwoni kama ni mtu mwenye uelekeo wa kufanikiwa, chochote anachopata ni pombe tu. Ananiambiaga plani zake nyingi za maendeleo napata matumaini labda ameanza kupata hamu ya kufanikiwa ila hakuna kitu.
Kila nikamuuliza analalamika kuwa wanawake tuna tamaa, sina tamaa ila nataka na sisi tufike mbali. Marafiki zake wengi wanajielewa na wana kazi nzuri tu, yeye kutwa ni kujisifia tu kuwa anafahamiana na huyu au huyu na kwamba amesoma Dar chuo cha mabrazameni na masistadu ila nikimwambia aniconnect nipate kazi huku Dar anaanza kulalamika nirudi mkoani atanilipa hiyo hela ambayo ningepata nikiajiriwa.
Nikiangalia kweli amejenga hapo mkoani ila pia kuna opportunity nyingi zaidi Dar kwanini anang’ang’ania mkoani? Na ameshawahi kusoma na kuishi Dar muda mrefu kwahiyo sio mgeni.
Lingine nikiangalia umri wangu unaenda na yeye wala haeleweki, tayari ana mtoto na mwanamke mwingine na hana interest ya responsibility na huyo mtoto. Nahisi ndiyo alivyo yaani wale wanaume wa kuzalisha watu tu bila mbele wala nyuma.
Kwenye kutomuamini kimapenzi ni kwasababu kila mara anaongea na maex wake nakusema flani bado ananipenda au flani anajuta kuachana na mimi. Yaani ananiboa sana kama wanampenda si aende kwa wao asinipotezee muda. Kuna wakati rafiki yangu aliajiriwa kwenye ofisi flani hapo mkoani nilitaka nimtume kwa siri baa jamaa anazoenda nione kama atamtongoza ila nikaona ni ujinga. Hii ingekuwa njia nzuri ya kumkamata na kuachana nae ila pia nahisi sitakuwa nimetenda haki, nakosa amani jamani sijui nifanyeje?
Na mambo mengi sana nayofikiria ila niishie hapa kwa leo.