Brother kaongeza mke wa pili, nimefurahi sana

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,321
Nina brother wangu, tunachangia mzee ila kila mtu yuko na mama yake. Brother ananizidi kama miaka 6.

Miaka ile nakuja kusoma chuo kikuu, nilifikia kwa brother kwa sababu yeye tayari alikua anafanya kazi hapa Dar ila immediately baada ya mimi kuja akahamishiwa mkoa mwingine hivyo akaniacha na mke wake nyumbani kwake.

Kwa miaka yote ile nasoma nilikua naishi kwa brother, tuseme nyumbani kwetu. Jamaa alikua akija Dar once in a while.

Sasa baada ya kumaliza masomo tu hata kabla ya graduation shemeji akamshawishi brother anitimiue nyumbani kwake, yaani sina hili wala lile, nikaomba muda kidogo nijipange lakini ikashindikana, nikatimuliwa.

Nikahamia kwa brother mwingine mtoto wa baba mdogo, yeye alikua well off zaidi kuliko brother wangu. Nikakaa pale kama mwezi, kisha nikaunganishiwa kazi moja mkoani nikaenda huko baadae nikarudi Dar hadi leo.

Sasa, shemeji yetu bwana yeye hakutaka kabisa mahusiano yangu na brother, alihakikisha anatufarakanisha, alifanikiwa mwanzoni ila nadhani baadae bro akili zikamrudia akaona alifanya ujinga, tukaendelea vizuri ila sio kama zamani.

Sasa kwa kua shemeji alishalikoroga kwa ndugu zake na mume wake, mambo yalipoanza kumuendea kombo kwa mumewe akakosa msaada.

Hivi karibuni bro kaongeza mke wa pili, actually alifanya ndoa ya kimila kwani tayari alishakua amemzalisha huyo mwanamke watoto 3, sisi tundu tunajua long time, mke mkubwa kajua jana, amechanganyikiwa, presha imepanda amelazwa, hana wa kumpa faraja kwa upande wa mume. Mimi nasema atulie dawa imuingie.

Mimi binafsi nimefurahi sana. Sasa hivi mimi shemeji mdogo ndio mshikaji wangu, yule kimeo namuangalia tu.

Wanawake msijisahau sana, unaweza kufanikiwa kufarakanisha ndugu ila hutaweza kufuta undugu wao.

Ni hayo tu wakuu.
 
Sema wote hamna akili tu hapo,

Sasa wew unaanza kujihusisha na ndoa za br ako za kazi gani?

Ulikuwa na uwezo wa kumzuia br ako kumzalisha huyo mdada?

Au kama huyo sister angekutreat vizuri kaka ako asinhechepuka?

Wote wangese niny
 
Mara nyingi msimuliaji hueleza mabaya ya mlengwa na kuacha mabaya yake kana kwamba yeye yuko sahihi kwa kila alitendalo.

Ndugu saa zngne jau sana ukute wewe ndo ulikuwa unawavuruga hapo home..Unakuta unaishi kiboss hutaki hata kusafisha choo au kazi ndogondogo ukiamka tu ni mguu na Njia na kujiona msomi uchwara wakikutimua unawaona wabayaaa na kuanza kuwaombea shida kumbe wewe ndo mpuzi namba moya. Aisee kuishi na watu kazi. Ubinadamu kazi

Siba guvu moya
BY MO
 
Mtoto wa kiume kushangilia matatizo ya ndoa za wengine ni dalili mbaya sana ya urijali wako.

Kupitia uzi huu naona ni halali kabisa huyo shemeji yako kutaka ufukuzwe kwao inaelekea una tabia za kike kike kiasi cha dada wa watu kuhisi kama anaishi na wifi yake.

Unaonaje hata huyo mke wa pili ushauri aachwe halafu wewe uhamie kwa kaka yako uwe unamhudumia, maana inaelekea una wivu sana na shemeji zako kwa kile wanachopata toka kwa kaka yako.

Na ukitaka kujua upumbavu wako, angalia hakuna comment hata moja inayo kusupport. Kila mtu anakuona mduwanzi. Hapo hatukujui, tumesoma upupu wako tu, imagine dada watu alikuwa anapitia mangapi kuishi na mpuuzi kama wewe.
 
Hili la wanawake kutaka kuwamiliki ndugu wa ukoo mmoja linawacost sana.
Ukitaka kumshika mmeo kamata ndugu zake kamata mama mkwe kamata mawifi kaka apindui akileta chochote ndugu wanasimama na mke.
Sasa we watibue mashemeji, mawifi,wakwe ndoa huna hapo
 
Inaonesha Tundu lisu unamwandika Sana ,magroup wasap huko

Aya ya nane ,Tundu isomeke ndugu


Hatujui dadazetu watakuelewa kweli
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom