Naomba ushauri kuhusu dini

Hawa watu wa namna hii wako wengi sana, wanajidai Waislamu kumbe si Waislamu, lengo lao ni kuichafua dini ya Allah, ila hili haliwezkani.


Hii mada nawaachia nyinyi ndugu zangu mmalizane, mimi naona kama anmtanipotezea muda. Nasoma maoni yenu nipate faida.
 
Mkuu dini zote tunamuabudu Mungu na sio kwamba kwa sababu mtu ni dini flani basi ataenda mbinguni isipokuwa matendo yako yatakupeleka na uamini wako,dini zote zinahubiri mambo yaleyale hivyo kama una amani zaidi kwenye ukristo basi fata moyo wako.
 
Hata Catholic bado hujafika bado
Tafuta mahali Kristo anahubiriwa na Mungu anajifunua. Uokoke umpokee Yesu maji ya baraka yanakupotezea muda tu
 
You are just a Scammer.

Wewe ni mkristo pure, tena mgonga kengele kanisani.

Acha ulaghai, kwa jifanya eti..... Blah .. blah.. blah.

Dini zinyewe za kuja tu...
Amini chochote tu... Acha ulaghai.

Ila

Hakuna moto wala pepo.
 
Njoo atheism huku hakuna viingilio vyenye kupewa majina kupunguza ukali kama sadaka au swadaka
 

Hebu pumzika dada huendi popote na hamna aliyeenda akarudi ebooh
 
Nakupenda sana
 
Kwa upande wangu sidhani kama kuna ulazima wa kutumia neno lenye utata na kuliacha neno lisilo utata ili hali maneno yote hayo yana maana moja.
 
Namna pekee ya kuepuka hivyo vitisho ni kuwa atheist tu

Huku tunaogopa umasikini sio mythical hell
 
Hivi hili fundisho la UTATU nani aliliweka kwa mara ya kwanza ? Maana najua kabisa Yesu hawezi kusema haya, sababu alikuwa ni nabii wa Allah.
Mfano familia fulani inamiliki gari moja.
Sentesi A. Tunalo gari jeusi, zuri linalotumia petroli na linakimbia kwa kasi sana.
Sentensi B. Tuna gari linalokimbia
Kutete ushirikina kazi sana. Natamani ungekielewa hiko ulichokiandika. Kanuni ya utoaji mifano umeiitupilia na hili nina uhakika kabisa kwamba huijui. Usilete falsafa na logic katika uhalisia. Mfano wako ulio utoa hauingii katika mfano wa utatu au kupitia mfano huo ukahalalisha utatu, hapo umedhibirisha wazi ni kwa namna gani Wakristo mnauwezo mdogo sana wa kuhoji.

Kwanza ulitakiwa utuambie Mungu ni nani hasa ? Sifa zake na tabia zake.

Mfano ulio utoa una leta maswali mengi sana miongoni mwa maswali hayo ni lazima tumjue nani mmiliki hasa wa hilo gari ? Kama wanamiliki wote ushirika wao uko sawa ? Lakini je hawapingani katika maamuzi juu ya gari hilo ? Sasa unapo toa mfano mambo hay unatakiwa kuyatilia maanani.
Kingine siyo unachosema "mnalo" basi wewe ni mmiliki au wewe una miliki, bali una muwakilisha yule mwenye kumiliki ambaye katika huo umiliki hamuwezi kuwa sawa.
Tunaruhusiwa kusema sentensi B na sentensi A ni moja.
Hakuna ruhusa hii katika lugha yoyote hata kimantiki inakataa sababu kikubwa hakiwezi kwa sawa na kidogo, yaani "Subset" haiwezi kuwa sawa na "Universal set" mpaka uanishe baadhi ya mambo na kuyatoa mengine.
Tunaruhusiwa pia kusema sentensi B ni mwana wa sentensi A na wakati tulisha sema ni moja na hatujachanganyikiwa! Kosoa hii logic kwanza kama iko na makosa. Kama haifai niambie nitumie miduara[cocentric circles labda tutaelewana
Hapa ndipo mlipoharibu dini yenu kuruhusu mawazo ya watu yaamue juu ya maandiko na cha ajabu mawazo yao hayakuweza kung'amua maandiko.

Hili jambo linakosolewa kwa uhalisia sababu hiyo logic imekwepa uhalisia. Hakuna nafsi tatu muda huo huo zikawa moja, huko ni kuikosea adabu akili mliyo pewa bure kwa kuipuuza na kuifanyia kazi.
 
Kwa upande wangu sidhani kama kuna ulazima wa kutumia neno lenye utata na kuliacha neno lisilo utata ili hali maneno yote hayo yana maana moja.
Hapa ndipo Wakristo mlipo angukia pua, ukisoma maelezo ya mwenzako anaonyesha wazi hicho alichokiandika hakijui na hawezi kukitetea, anawezaje kuelezea maandiko ya dini kwa kutumia falsafa na logic ? Elimu dhaifu namna hii ?

Hapa alitakiwa aende na maana za maandiko na uhalisia ila huko alipoenada hapakidhi haja.
 
Swadakta. Yaani islam ingekuwa dini ya haki kama wanavodai ingekuwa inatawala dunia, na mungu asingeruhusu dini nyingine itawale
Mwenyezi Mungu humpa nguvu amtakaye na umnyima amtakaye na vyote(kunyimwa na kupewa) sio kiashiria cha kupendwa au kuchukiwa bali ni mtihani .

Mbona Wana Israel kipindi cha mateso ya firauni Mwenyezi Mungu aliruhusu wateseke huku firauni akiwatawala je hapo firauni alikuwa kipenzi cha Mwenyezi Mungu kwa vile alikuwa super power kwa wakati ule ? na vipi mwisho wake ukikuwaje ?
 
Uzima wa milele, Wakati tunaona makaburi ya Wakristo yamejaa, sawa tu na wasiyo Wakristo, unachekesha wewe.
Hebu nenda Mburahati ukaone, angalau mngedanya, kuwa wakristo mtafufuliwa baada ya kufa, maana kufa lazima ufe hivyo hakuna uzima wa milele.
.
Mkuu!Hivi hata kiswahili ni kigumu kwako?.Ni wapi andiko limeongelea kufa mwili?Na niwapi nimekuambia kuwa mimi mkristo?
Usipoelewa kinachoelezwa na mtu ni bora zaidi ukikaa kimya kuliko kujidharirisha hivi.
 
We una amini jiwe ni kiumbe hai?
 
huyu amepatwa na shambulizi la shetani na limempata akiwa hana kinga hata 0.00000 so ni suala la muda tu atahamia huko anapotamani, aaamyn atuepushe sote kaka.
 
Kwenye Biblia Yona aliitwa na Mungu akaokoe watu wa Ninawi lakini hakutaka kufuata sauti ya Mungu badala yake akapanda Meli kwenda Tarshishi ili asitii agizo lq Mungu lakini meli aliyopanda ilipata mawimbi sana hadi alipojitokeza akajisalimisha walivyomtupa baharini meli ikatulia na akamezwa na samaki akakaa kwa siku 3 tumboni kwa samaki akisali hadi samaki akamtapika kwenye ufukwe wa mji ule ule aliokua hautaki.....akafanya kazi aliyotumwa na kusudi la Mungu kikatimia.
Nimejikuta na relate habari yako na kisa cha Yona, inawezekana msukumo ulionao ni Mungu ameweka ndani yako ili akutumie kwa jambo fulani kudhihirisha ukuu wake, Inawezekana Mungu anataka akakutumie maisha yako yawe ushuhuda kwa wengine. Kuna maneno yanasema "God does not call the qualified but he qualifies the called " ....Mimi nakuombea kusudi la Mungu litimie kwako na akutumie vile anavyotaka.
Natamani sana sana uje utupe ushuhuda siku moja Empress_sheila
 
Mkuu!Kwanza mimi siyo mkristo.
Lakini pia ni vema ungenifuatilia huko juu ili kujua mimi nafundisha nini na kwa aina gani ya mafundisho.
Asante.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…