Naomba ushauri kudhurumiwa kiwanja

A.Ngindo

JF-Expert Member
Apr 6, 2012
276
98
Habarini wana jamvi,Nina shida kuhusiana na kichwa cha habari husika hapo juu.

Iko hivi Miezi 6 iliyo pita nilinunua kiwanja cha makazi maeneo ya Kinyerezi Dar es Salaam, Baada ya kua nimeonyeshwa mipaka ya eneo na michoro ya kiwanja katika ramani ya mipango miji na mhusika wiki moja badae nikaenda ofisi za serekali ya mtaa za eneo husika ili kujiridhisha na mmiliki wa eneo pamoja na uhalali wa kiwanja.

Nakukuta kua jamaa anatambulika kama mmiliki halali wa eneo kupitia hati ya serekali ya mitaa na eneo limerasimishwa kama eneo la makazi,nikampigia jamaa simu ilikesho yake tuka andikishane nilipie.

Kesho yake mimi na mashahidi wangu wawili ambao ni ndugu zangu pamoja na mmiliki wa kiwanja na shahidi wake mmoja tukaenda ofisi za mtendaji ili watuandikie hati ya mauziano mimi na mmiliki wa eneo pamoja na mashahidi wetu tuka sign ile document na ikapigwa mihuru na mtendaji.

Baada ya hapo tukatoa copy kadhaa za ile hati ya mauziano na kuacha copy mbili ofisi za mtendaji baada ya hapo tukaenda bank nikamlipa mmiliki wa kiwanja na akanipa ile hati ya mauziano,kila mtu akaendelea na maisha yake sasa shida imekuja juzi nimeenda sight nimekuta kuna jirani yangu mmoja kaweka uzio kwenye eneo ambalo ndio njia ya mimi kuingilia kiwanjani kwangu yani kama ni nyumba itajengwa basi njia ya mimi kuingia nyumbani kwangu itabidi iwe hapo sasa ikabidi nimfate na kumuuliza KULIKOONI na jamaa akanitolea ramani yake ya mpango miji ikionyesha kua kile kiwanja changu ni kiwanja kisicho kua na njia na kua ile ramani niliyopewa na jamaa aliyeniuzia ni fake japo inafanana asilimia 98 na ramani halisi ya eneo lile kwa kua kasoro iliyopo ni hicho kipande cha njia tu ndio kime editiwa kutoka kwenye ramani halisia.

Naombeni mnishauri nini naweza kufanya maana nilivyo enda serekali za mitaa nilionyeshwa ramani na nikapewa copy ikionyesha kua njia itafika mpaka ndani ya eneo langu kumbe sivyo huyu jamaa kanifanyia usanii.Naombeni kujua nini natakiwa kukifanya maana najaribu kumpigia jamaa kuhusu hili ila kila tukiongea ananiambia nipe muda kidogo walau wiki ntakuja tuta yamaliza lakini naona kila ifikapo hiyo wiki ninapo mtafuta ana leta usanii sanii tuu na sasahivi hapokei simu zangu kabisa ndugu na rafiki zangu wakaribu wananiambia nirudi kuwaeleza serekali ya mtaa kilicho tokea kupitia baraza la ardhi ili wamuite tujadili maana alipo niuzia kiwanja ramani aliyonipa na aliyotoa serekali yamtaa ilikua ikionyesha njia inafika mpka kwenye kiwanjani sasa sahivi nagundua ilikua ni mchezo ,jamaa nyumbani kwake ni meter 100 tu kutoka hapa kwenye kiwanja lakini kila nikija sight ananikwepa hatuonani na naambiwa huwa yupo tu kila siku saa 10 anakua kashatoka kazini yupo mtaani watu wanamuona,Naombeni mnishauri nifanyeje
 
Habarini wana jamvi,

Nina shida kuhusiana na kichwa cha habari husika hapo juu
Iko hivi Miezi 6 iliyo pita nilinunua kiwanja cha makazi maeneo ya Kinyerezi Dar es Salaam,

Baada ya kuwa nimeonyeshwa mipaka ya eneo na michoro ya kiwanja katika ramani ya mipango miji na mhusika wiki moja badae nikaenda ofisi za serekali ya mtaa za eneo husika ili kujiridhisha na mmiliki wa eneo pamoja na uhalali wa kiwanja.

Nakukuta kuwa jamaa anatambulika kama mmiliki halali wa eneo kupitia hati ya serikali ya mitaa na limerasimishwa kama eneo la makazi, nikampigia jamaa simu ilikesho yake tukaandikishane nilipie.

Kesho yake mimi na mashahidi wangu wawili ambao ni ndugu zangu pamoja na mmiliki wa kiwanja na shahidi wake mmoja tukaenda ofisi za mtendaji ili watuandikie hati ya mauziano mimi na mmiliki wa eneo pamoja na mashahidi wetu tuka sign ile document na ikapigwa mihuru na mtendaji.

Baada ya hapo tukatoa copy kadhaa za ile hati ya mauziano na kuacha copy mbili ofisi za mtendaji baada ya hapo tukaenda bank nikamlipa mmiliki wa kiwanja na akanipa ile hati ya mauziano, kila mtu akaendelea na maisha yake sasa shida imekuja juzi nimeenda sight nimekuta kuna jirani yangu mmoja kaweka uzio kwenye eneo ambalo ndio njia ya mimi kuingilia kiwanjani kwangu yani kama ni nyumba itajengwa basi njia ya mimi kuingia nyumbani kwangu itabidi iwe hapo sasa ikabidi nimfate na kumuuliza KULIKONI na jamaa akanitolea ramani yake ya mpango miji ikionyesha kuwa kile kiwanja changu ni kiwanja kisichokuwa na njia na kuwa ile ramani niliyopewa na jamaa aliyeniuzia ni fake japo inafanana asilimia 98 na ramani halisi ya eneo lile kwa kuwa kasoro iliyopo ni hicho kipande cha njia tu ndio kimeeditiwa kutoka kwenye ramani halisia.

Naombeni mnishauri nini naweza kufanya maana nilivyoenda serikali za mitaa nilionyeshwa ramani na nikapewa copy ikionyesha kuwa njia itafika mpaka ndani ya eneo langu kumbe sivyo huyu jamaa kanifanyia usanii.

Naombeni kujua nini natakiwa kukifanya maana najaribu kumpigia jamaa kuhusu hili ila kila tukiongea ananiambia nipe muda kidogo walau wiki nitakuja tutayamaliza lakini naona kila ifikapo hiyo wiki ninapo mtafuta ana leta usanii sanii tuu na sasahivi hapokei simu zangu kabisa ndugu na rafiki zangu wakaribu wananiambia nirudi kuwaeleza serikali ya mtaa kilichotokea kupitia baraza la ardhi ili wamuite tujadili maana aliponiuzia kiwanja ramani aliyonipa na aliyotoa serekali ya mtaa ilikuwa ikionyesha njia inafika mpaka kwenye kiwanja sasa sahivi nagundua ilikua ni mchezo,

Jamaa nyumbani kwake ni meter 100 tu kutoka hapa kwenye kiwanja lakini kila nikija sight ananikwepa hatuonani na naambiwa huwa yupo tu kila siku saa 10 anakuwa kashatoka kazini yupo mtaani watu wanamuona

Naombeni mnishauri nifanyeje
 
Kiwanja kipo vizuri shida ni njia ya kukifiki karibu kuzungumza na aliyeweka uzio akuuzie eneo kiasi ulifanye kuwa njia

Huyo mpuuzi hawezi kukusaidia lolote zaidi mbane akurudishie fedha kiasi ununue njia
 
Kila siku tunatoa ELIMU mitandaoni ya namna ya kununua kiwanja lakini hamfuatilii..

Kwa usalama wako siku nyingine hakikisha kiwanja unachotaka kununua kiwe na ramani ambayo ni surveyed na kwa kuhakikisha zaidi nenda hata wizarani kafanye search ya eneo unalonunua

Kwa stage uliyofikia cha kukusaidia hatuna zaidi ni kukuambia siku nyingine ukitaka kununua kiwanja fuata ushauri uliopewa hapo juu.

 
Pole mkuu kwa masaibu haya. Ramani iliyotumika kukuuzia ni hakali ambayo ukithibitisha kutoka mamlaka halali za mtaa. Kosa liko kwa muuzaji. Itisha kikao na serikali za mtaa huyo muuzaji anagakiwa kukulipa njia ya kupita.
 
Habarini wana jamvi,

Nina shida kuhusiana na kichwa cha habari husika hapo juu
Iko hivi Miezi 6 iliyo pita nilinunua kiwanja cha makazi maeneo ya Kinyerezi Dar es Salaam...
Nimecheka Sana uliposema hati ya serikali ya mtaa, hamna kitu ka hicho.
Uwe unawatumia wanasheria kwenye manunuzi ya ARDHI.
 
Usinunue njia kwanza fuatilia ramani ya eneo husika mipango miji kisha kama ni kweli eneo limerasimishwa lazima kuna njia halafu ukinunua ardhi iliyopimwa au kurasimishwa ni lazima ukaandikishane kwa mwana sheria anae tambulika tena ili kuthibitisha uhalali wa mwanasheria una google id yake!
 
Habarini wana jamvi,

Nina shida kuhusiana na kichwa cha habari husika hapo juu
Iko hivi Miezi 6 iliyo pita nilinunua kiwanja cha makazi maeneo ya Kinyerezi Dar es Salaam,

Baada ya kuwa nimeonyeshwa mipaka ya eneo na michoro ya kiwanja katika ramani ya mipango miji na mhusika wiki moja badae nikaenda ofisi za serekali ya mtaa za eneo husika ili kujiridhisha na mmiliki wa eneo pamoja na uhalali wa kiwanja.

Nakukuta kuwa jamaa anatambulika kama mmiliki halali wa eneo kupitia hati ya serikali ya mitaa na limerasimishwa kama eneo la makazi, nikampigia jamaa simu ilikesho yake tukaandikishane nilipie.

Kesho yake mimi na mashahidi wangu wawili ambao ni ndugu zangu pamoja na mmiliki wa kiwanja na shahidi wake mmoja tukaenda ofisi za mtendaji ili watuandikie hati ya mauziano mimi na mmiliki wa eneo pamoja na mashahidi wetu tuka sign ile document na ikapigwa mihuru na mtendaji.

Baada ya hapo tukatoa copy kadhaa za ile hati ya mauziano na kuacha copy mbili ofisi za mtendaji baada ya hapo tukaenda bank nikamlipa mmiliki wa kiwanja na akanipa ile hati ya mauziano, kila mtu akaendelea na maisha yake sasa shida imekuja juzi nimeenda sight nimekuta kuna jirani yangu mmoja kaweka uzio kwenye eneo ambalo ndio njia ya mimi kuingilia kiwanjani kwangu yani kama ni nyumba itajengwa basi njia ya mimi kuingia nyumbani kwangu itabidi iwe hapo sasa ikabidi nimfate na kumuuliza KULIKONI na jamaa akanitolea ramani yake ya mpango miji ikionyesha kuwa kile kiwanja changu ni kiwanja kisichokuwa na njia na kuwa ile ramani niliyopewa na jamaa aliyeniuzia ni fake japo inafanana asilimia 98 na ramani halisi ya eneo lile kwa kuwa kasoro iliyopo ni hicho kipande cha njia tu ndio kimeeditiwa kutoka kwenye ramani halisia.

Naombeni mnishauri nini naweza kufanya maana nilivyoenda serikali za mitaa nilionyeshwa ramani na nikapewa copy ikionyesha kuwa njia itafika mpaka ndani ya eneo langu kumbe sivyo huyu jamaa kanifanyia usanii.

Naombeni kujua nini natakiwa kukifanya maana najaribu kumpigia jamaa kuhusu hili ila kila tukiongea ananiambia nipe muda kidogo walau wiki nitakuja tutayamaliza lakini naona kila ifikapo hiyo wiki ninapo mtafuta ana leta usanii sanii tuu na sasahivi hapokei simu zangu kabisa ndugu na rafiki zangu wakaribu wananiambia nirudi kuwaeleza serikali ya mtaa kilichotokea kupitia baraza la ardhi ili wamuite tujadili maana aliponiuzia kiwanja ramani aliyonipa na aliyotoa serekali ya mtaa ilikuwa ikionyesha njia inafika mpaka kwenye kiwanja sasa sahivi nagundua ilikua ni mchezo,

Jamaa nyumbani kwake ni meter 100 tu kutoka hapa kwenye kiwanja lakini kila nikija sight ananikwepa hatuonani na naambiwa huwa yupo tu kila siku saa 10 anakuwa kashatoka kazini yupo mtaani watu wanamuona

Naombeni mnishauri nifanyeje
Ninyi wanunuzi wa viwanja mnatusumbua sana, sasa hivi hapa nilipo nahangaika na kesi mahakamani! Jitu limejipeleka tu kwa mwenyekiti wa mtaa kulipia kiwanja bila kujiridhisha kwa ofisi ya ardhi Manispaa likajikuta linauziwa kiwanja ambacho tayari kina hati kwa jina langu. Sasa na wewe ilikuwaje ukatumia ramani ya mwuzaji wa kiwanja? Kwa nini hukuenda kupata ramani halisi kule mipango miji? Kosa umelifanya wewe mwenyewe, ulitakiwa ukawachukue mipango miji waje wachukue coordinates za eneo hilo halafu wakakuangalizie kwenye ramani yao ambayo imetokana na survey ya eneo husika. Sasa nenda Manispaa ukawaone maafisa mipango miji watakusaidia (ila lazima hapo wakupige hela kidogo za usumbufu) kama kweli hakuna njia ya kuingia uwanjani kwako! Ukikuta kweli hakuna njia itakuwa imekula kwako! Ukikuta kuna njia itabidi ufungue kesi mahakamani na mashahidi wako watakuwa hao hao serikali ya mtaa pamoja na watu wa ardhi!
 
Back
Top Bottom