Naomba ushauri jamani

Naomba ushauri jamani

alichokiunganisha MUNGU mwanadamu asikitenganishe so mwombe MUNGU sana atakusaidia "kamwe MUNGU hawez kukuacha bila msaada"
 
ndugu pole sana...hichi kisa kinasikitisha kiukweli....ushauri wangu ni kwamba kwa sasa fanya mambo yako wewe kama ww...yaani ingefaa ujipange upya bila kumtegemea coz kwa hali nilivyoielewa hatajenga hiyo nyumba bali huenda ana mipango yake.

ukifanikiwa kutimiza malengo yako ndipo utakapoelewa majibu ya maswali mengi uliyonayo...

nakutakia afya njema na mafanikio.
 
Kwa ushauri wangu mngepeana nafas kidogo,yan umrudshe kwao kwa mda hata 4mnths huku ujpanga kufanya mambo yako yakae sawa.Kwa sasa sidhan kwamba kutakuwa na suluhsho ambalo litaweza kuondoa uchungu ulioko nao sasa akiwa bado yupo ndani.Mrudshe kwao kwa mda ila n vzr asjue ni kwa mda,alafu ufanye mambo yako kwa uhuru.Pole sana kaka.
 
Pole sana , tatizo hapo ni wewe kushindwa kusimama kama mwanaume ndani na kusimamia maendeleo ya familia. Siku zote unapoingia kwenye mahusiano au ndoa usiweke dhana ya kuona furan ni sahihi kwa kila jambo. Ulitakiwa masuala ya maendeleo usimamie wqewe kwa vile unaujua mwenendo halisi yeye alitakiwa afuate maagizo. Lkn pia ulimpenda sana kiasi ukamwachia mamlaka yote kiasi akakupanda kichwan hasa suala la maamuzi
 
Nadhani ukichwa wa familia ni uwezo wa kutafuta pesa, huo uwezo ninao mkubwa sana na unaongezeka kila siku,
kwa bandiko lako hili, nimeweza "kukuona" na kukufahamu!, ni vyema ku accumulate mali kwa haki kama ufanyavo, lakini si sahihi hata kidogo kuiachia pesa isimame ktk nafasi yako kama baba wa familia! rudi usimame kny nafasi yako uiongoze familia yako na siyo kuachia pesa iongoze. Mkeo usimwache labda kwa uzinzi tu,
 
unaweza kuendesha biashara ila ukashindwa kuendesha familia...sometimes moneys isn't everything...
 
ndio maana huko kukaya wanaogopaga wakiona kijana ameoa mkoa huo uliooa wewe... japo huwa sikubaliani nao, lkn....

back 2 the topic, huyo hana sifa ya kuwa mke. kuna wanawake wanagangamala wenyewe kwa ajili ya families zao hawajui hata 1% ya mishahara ya waume zao ikoje. sasa yeye 80% ya salary anapata, na mihela mingine anailalia ndani halafu bado hawezi kufanya kitu chochote.

huyo mwanamke ni limbukeni na mshamba (amepita hata vidato vile vinne?). kwa nini akae na 5M ndani atembee na 2M kwenye gari wkt banks na mitandao ya simu ipo.

simama kama mwanaume, ndani ya nyumba. umesema baba yako alikuwa akimpa mama yako hela yote. unasahau kwamba unapoanza maisha ya ndoa unaenda kuishi ndoa yako na si ndoa za watu wengine. hakuna formula kwenye marriage life, don't copy your parents life style, tengeneza ya kwako
natamani nikwambie umrudishe kwao hata kwa miezi mi3 akapate kitchen party mara ya pili
 
Biashara alianzisha nikiwa safarini, mawasiliano huvunjika pale anaposhindwa kutoa accounting ya pesa, nimeishamkaliza zaidi ya mara mia moja, mpaka nimempleka nje ya nchi kupumzika, na huko nikalianzisha, in a friendly and lovely manner, kwamba pesa zinatumika vipi, biashara fulani inaendeleaje, imekufakufaje, nikakuta baadhi ya partiners ni family members wake, kwa pesa alizokili watu wamekataa kumlipa ama kwa kutokuonekana au kwa kudai hawana nikamuomba anipe details zao za kutosha ili niwachukulie hatua za kisheria hata kwa ubabe sababu i have networks hakutoa ushirikiano mpaka leo.

Leo jioni naondoka moshi (nyumbani kwao),
kakataa kwenda Mwanza kwamba atakuja baada ya mwaka mpya, bado hili sio tatizo sababu as long as atakuja na anabaki kwa wazazi wake natambua damu ni nzito, sio issue.

bado hapo ninatatizo la mawasiliano?

Ni majanga.
 
Pole sana mkuu @Sangarara kutokana na maelezo uliyoweka inaonyesha fika kuwa kwenye ndoa yako kuna tatizo kubwa.

  • Uaminifu kwenye pesa: hili ni tatizo kubwa sana hasa mwanandoa mmoja anapokua sio muwazi kwenye matumizi yake na namna anavyopata pesa kwani inajenga hisia hasi.
  • Kushindwa kwa mke kusimamia mambo ya msingi kama vile ujenzi hii ni shida
  • Mashaka juu ya uaminifu wake kwenye ndoa mara baada ya kubamba picha akituma kwa wanaume na kufanya mawasiliano na hao wanaume . Mkuu kwangu mimi hili ndio naliona kuwa ni tatizo kubwa na pengine ndilo linalochangia yote yanayoendelea kwenye ndoa yenu. Halafu mwanamke kukataa kwenda na wewe kwenu kisa abaki moshi na wazazi wake atakufuata baadae mmmh hii nayo ni shida mkuu.

Ushauri wangu fanya uchunguzi ujue hizo pesa zinapelekwa wapi na jitahidi ujue uhusiano wake na hao aliowatumia picha . Uchunguzi huu utakusaidia kupata ushahidi au vielelezo vya kutosha ktk kufanya maamuzi magumu. Si ajabu mwenzio kesha jenga na ana mpango wa kuolewa au kuishi peke yake na hivi anajua afya yako imeanza mgogoro be careful.
 
ndio maana huko kukaya wanaogopaga wakiona kijana ameoa mkoa huo uliooa wewe... japo huwa sikubaliani nao, lkn....

back 2 the topic, huyo hana sifa ya kuwa mke. kuna wanawake wanagangamala wenyewe kwa ajili ya families zao hawajui hata 1% ya mishahara ya waume zao ikoje. sasa yeye 80% ya salary anapata, na mihela mingine anailalia ndani halafu bado hawezi kufanya kitu chochote.

huyo mwanamke ni limbukeni na mshamba (amepita hata vidato vile vinne?). kwa nini akae na 5M ndani atembee na 2M kwenye gari wkt banks na mitandao ya simu ipo.

simama kama mwanaume, ndani ya nyumba. umesema baba yako alikuwa akimpa mama yako hela yote. unasahau kwamba unapoanza maisha ya ndoa unaenda kuishi ndoa yako na si ndoa za watu wengine. hakuna formula kwenye marriage life, don't copy your parents life style, tengeneza ya kwako
natamani nikwambie umrudishe kwao hata kwa miezi mi3 akapate kitchen party mara ya pili
Tatizo la hawa kaka zetu ni kusema "sawa do, ndoho mhayo" inawaumiza sana.
 
Pole ndugu,pesa anazo na akimaliza mipango yake anakumaliza.muombe Mungu akunusuru
 
Dah..I feel so sad about this, you sound so frustrated, kama unaamin maandiko basi soma zaburi 32:8 "Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea, nitakushauri, jicho langu likikutizama", Muombe Mungu huwezi amini atakupa amani na jinsi ya kusimama tena na kukuondolea maumivu, usiweke imani sana katika uwezo wako ulionao.

Pia, Unaonekana umekulia familia yenye furaha sana na amani ukajifunza kitu kwa baba yako ukatamani utumie mfumo huohuo kwenye ndoa yako, and it has failed terribly..hukua na nia mbaya..na wala mkeo hakua na nia mbaya nadhani hakuwahi kushika pesa kama ile sasa alipoiona kwa nia njema na ile tabia yake ya kupenda kutafta akajenga picha kichwani ya jinsi akifanya ile biashara mtaendelea zaidi..na njiani of course vikaingia vitabia vya kiburi (humjui mtu mpaka amiliki pesa) na pia management ya pesa ikamshinda na labda watu wakaanza kutake advantage of her etc etc..alikua na tabia nzuri, all she needed was your strict management and guidance..haimaniishi eti ukiwa unamuongoza basi humpendi au yeye hafanyi nafasi yake..noooo..kwa sisi wanafunzi..tunajua kua tupo aina nyingi..kuna wanafunzi wanafanya vizuri bila supervision, yaani ni very independent na anakuletea product nzuri, ila kuna wale lazima umcheki kila wakati, umhimize, umchallenge, na yeye anafanya vizuri kwa mazingira hayo..hapo hamna mbaya wapo tu tofauti

Mungu akusaidie/awasaidie sana maana kuachana sio suluhisho, pia huyo mkeo anahitaji apate wakati mgum kiaina..yaani mda wa kujutia..afunguke macho..kama akiweza kujirudi itasaidia sana, ila kama hatayaona makosa yake..mmmhhh..Mimi na mpenzi wangu tumefanya vitu vingi sana vya maendeleo pamoja na hua ananiamin sana hata bado hatujaoana najua ana sh ngapi na pesa za savings amehamishia zote kwenye account yangu ili kwa urahisi wa mambo yetu, kabaki na mshahara wake tu ndo unaingia kwake, yaani yuko kama wewe kabisaaa..sasa hua nawaza yaani tukioana tutafika mbali sana..sasa nimesoma hapa nimesikitika sana, naomba Mungu mpate mlango wa kutokea.
 
Pole Mkuu,i hope things will get better!Sina experience na ndoa,sina cha kukushauri wengi wamejaribu kutoa Ushauri!just do what is best for you and maybe her.
 
Full kuchanganyikiwa hata kueleza tatizo shida....,au ndo visa visivyoelezeka mpaka kuona?
 
Haiwezekani wewe uwe una tatizo la kiafya badala ya mkeo aende na wewe mza mfikilie jinsi gani mpate pesa za matibabu yako yeye anasema anabaki kwao.

je yy ni mke wa nani?ina maana hana uchungu na wewe sasa na ndio maana ata anasita kuuza gari yake kwa sababu ya kutibiwa wewe.

Hakuna kitu muhimu kama afya yako kwanza.
Mwisho akili ku mkichwa mkeo hawezi kutumia mipicha ya utupu wanaume wengine kama hana mahusiano nao ya kingono.
Cha msingi fight utibiwe kwa pesa zako tu manake huyu mkeo inaonekana anasubiri uhumie (ufe) ili abaki anatanua na pesa ulizompatia mwenyewe.
 
Hii ni serious sana.

Nina Mke na mtoto mmoja, ndoa yenu inamiaka mitano sasa, katika swala la uaminifu katika ndoa sijawahi kumhisi mke wangu kutokuwa mwanaminifu, inawezekana ni kwa sababu nimeamua hivyo au inawezekana ni sahihi kabisa kwamba ni mwaminifu mpaka nilipokutana na kitu cha ajabu majuzi.

Naposema namuamini inajumuisha ukweli kwamba,sijawahi kupata kusikia wala kuhisi juu ya tabia mbaya juu yake,kiasi kwamba sikuwahi kufikiria kumfanyia uchunguzi wa namna yoyote ile.

Kwa upande wake, naweza kusema ama haniamini au anawivu sana na mimi, hataki hata nikae na rafiki zangu, ikitokea nimefanya hivyo atanisumbua sana kwa simu na kunikera kiasi cha kufanya hata hayo mazungumzo nayofanya kuwa hayana maana, sababu concentration inakuwa zero kwa ajiri ya kujieleza niko wapi,niko na nani,nafanya nini,kwa nini tuwe hapo na tusiende nyumbani,narudi saa ngapi, na vitisho vingi, na mimi natoka, na mambo mengine mengi tu, haiishii hapo nikirudi nyumbani ndio inakuwa tabu ni ugomvi usio wa kawaida. for five years now.Hiyo ni tisa.

KUMI
MATUMIZI YA PESA
Sijui nilielezeje hili. wakati namtongoza, nilimuona kama mtu mmoja makini sana kwenye mambo ya pesa, kwanza hakuwa tayari tutumie pesa nyingi tukiwa nae, kuna siku tulienda disco tulipotoka disco tukaenda kulala Kilimanjaro kemplinski, kesho yake ilileta ugomvi mkubwa sana, kwamba ninamatumizi makubwa na mabaya ya pesa ukizingatia tulipokuwa disco (maisha club) nilikutana na marafiki kadhaa nikawapiga pombe vibaya sana, so aliweza mpaka kunieleza kwenye pombe tu tumetumia kiasi gani (alichukua bili zote nilizolipia).

Na katika swala la Pombe akanilazimisha niache, nami nikapunguza kiasi.

Kabla ya Kufunga ndoa, tayari nilikuwa na maisha safi kabisa, nasomesha ndugu zangu, nimejenga nyumba yangu LockCity na nikawa naendeleza kiwanja viwanja viwili DAR.

Baada ya Kufunga ndoa, kila kitu kikasimama.

Nyumba moja niliyokuwa najenga, nilimpatia bwana mdogo wangu aimalizie alafu akae yeye, mimi nikaendelea kupanga nikiamini with my economist wife, ntamalizia hiyo nyumba nakuamia ndani ya mwaka mmoja. wapi, hiyo nyumba nimeishia kuiuza mwaka huu.

PESA ZINAKWENDA WAPI.
Nampa yeye, kwanza nilimpa kazi ya kusimamia hiyo nyumba iishe, kwa mantiki kwamba ni nyumba yake,aimalizie kwa namna roho yake inavyopenda na kuifurnish kwa umaridadi wa aina anayoiota yeye.

Kwanza alianza kunieleza anazungusha hizo pesa, na kweli nyumbani akawa na mahela mengi kwelikweli, japo nilikuwa namkanya, lakini aliendelea kusisitiza kwamba biashara anazofanya zinahitaji awe na pesa wakati wote, anakaa na zaidi ya milioni ishirini ndani, anatembea kwenye gari na si chini ya milioni tano, nikastudy biashara husika nikaona kuna ukweli wa kuhitaji kuwa na pesa mkononi, lakini nikimuambia tukae nimsaidie kupiga hesabu tujue anapataje faida anakataa tena anakuwa mkali kwelikweli.

Mwisho wa siku, ananiletea story inayoonyesha kwamba kuna watu wanachelewa kumlipa pesa zake, namuongezea, wakati huo asilimia themanini ya mshahara nampatia.

Ni mengi Jamani, kuna mambo positive anafanya, lakini ndio kama kubadirisha thamani za ndani,kubadirisha gari,n.k

Mwaka huu mwezi wa saba, nikaachana na mambo ya kuajiriwa, nikaanza kufanya mambo yangu mwenyewe, niliamini kwamba, mambo ya chakula, nyumbani hayawezi kumshinda, pango la nyumba siwezi kushindwa kulipa.

Mwaka huu nikapata matatizo ya kiafya, nikalazimika kuuza haraka sana nyumba iliyokuwa haijaisha (ambayo alishindwa kuiendeleza kwa asilimia zaidi ya tisini), nikauza na kiwanja changu, magari mawili niliyokuwa natumia, nasikia gari analotumia yeye ambalo ndio lenye thamani kubwa kulinganisha na yale niliyokuwa natumia mimi alikataa kuuza, japo ndilo nilimuelekeza aliuze nikijua litauzika kwa haraka, yeye aliniambia hakuna mtu aliyejitokeza japo kuliulizia.


Naomba msaada, najua atapita hapa kusoma na ataelewa ni mimi nimepost, na namzungumzia yeye, lakini kwa kweli kabisa, nafikilia kulifikisha swala hili kwa wazazi na ndugu zangu ndani ya wiki mbili hizi nikiwa mwanza, nafikiria kuachana na huyu mwanamke.

Nimeamua kulileta hili hapa, kwanza ili kupunguza pressure na hazira nilizonazo, na zaidi kupata ushauri usioegemea upande wowote, sababu najua nilifikisha home, uwezekano wa kupita hata bila kujadiliwa ni asilimia zaidi ya mia, na nimejizuia kufanya hivyo kwa muda mrefu nikijua matokeo ndio yatakuwa hayo.

NINGEWEZA KUKUPA POLE LAKINI HAINAMAANA MAANA WEWE NISHUJAA NISEME HONGERA,Baadayakusema hayo nakwambia hivi kaa sehem isiwe kwenyekiti chinikabisa turia ,utapatajibu la kimungu, achana nakaurimbiu alichokiunganisha. mungu,Yesu wakati saa yakuteswaimekaribia alisema iki"wezekana kikombehiki kiniepuke.kwahiyo wewe amuwa kusuka au kunyowa. onyo usimuwazie kufa. afya yako kwasasa unaendereaje ?? ---
 
Mkuu kwanza ninakupa pole Sana narudia tena pole Sana nimesoma kwa makini story yako huku mapigo ya moyo yakiongezeka kwa kasi Sana Kana kwamba ni Mimi yamenikuta!! Narudia tena pole Sana na nimesoma vizuri komenti za wachangiaji wengi wanaona kwamba hukua na mawasiliano ya moja kwa moja,! Kitu Kimoja ambacho kimekuponza ni uaminifu mkubwa Sana kwa mkeo na mkeo ameshakupima akagundua udhaifu wako Ndio maana yote hayo yanatokea! Unaogopa kelele zake na Ndio maana ukimkalisha Hakuna unachopata!! Swala langu ni moja tu MKUU KUANZA UPYA SI UJINGA UMEOA PEPO! Alijifanya mwema kwako wakati wa uchumba kukudhibiti matumizi ili uone huyu anafaa kumbe sio! Baada ya kuingia kwenye ndoa akua mmiliki sasa anafanya hata ambacho hukifanyi! Na kutokana na matendo yake machafu anajua na wewe unaweza fanya Ndio maana ukiwa hata na rafiki zako anakua mkali!! Tokea umemuoa maisha na uchumi unashuka sasa huyo mtu wa nini La mwisho ambalo Kama ni Mimi navunja ndoa siku ya harusi ni kutuma picha za utupu wake kwa wanaume wawili tofauti mkuu nikuulize swali mkeo ulimuolea Mahari milioni Mia sasa unazionea uchungu?!! Mzee ungekua bro wangu mie tungepigana Kama unaendelea kukaa na hilo jini nasikia uchungu Sana yaani!!
 
Kwavile umesema atapita hapa na atajua unamzungumzia yeye basi ngoja nisubiri apite ajibu kwanza tuhuma kama wanasaiasa then nitawashauri kwa pamoja.
 
Back
Top Bottom