Saidama
JF-Expert Member
- Jun 10, 2022
- 500
- 944
Kama kichwa cha habari kinavyoeleza, ni jambo lililotushtua kama familia kutokana na uajabu wake.
Ipo hivi, siku ya juzi tar 19 majira ya saa sita kasoro usiku nikiwa nimelala fofofo, simu yangu ambayo ilikuwa kwenye 'vibration mode' ilikuwa ikiita.
Wife kwakuwa alikuwa bado hajalala akawa ananiamsha niipokee lakini kabla hajafanikiwa kuniamsha akashangazwa kuona namba iliyokuwa inanipigia ni namba yake mwenyewe ambayo anatumia kwenye simu yake na wakati huo simu yake akiwa nayo mkononi, cha kushangaza zaidi ni kuwa simu yake haikuwa na salio la kuweza kupiga wala kubeep na haikuwa inaonesha kama inapiga simu, lakini kwenye simu yangu inaonekana ni namba yake ndiyo inapiga, namba yake ambayo nimeisave vizuri kabisa.
Wife akaamua kupokea mwenyewe tu ili aone ni kitu gani. Hakukuwa na sauti yoyote iliyosikika na yeye pia hakuongea chochote. Akawa ameiskilizia mpaka sekunde ya 31 akakata.
Kwakuwa nilikuwa nimechoka sana wife hakutaka kuniamsha na badala yake akaja kunielezea kila kitu asubuhi ambapo iliingia habari nyingine ya kushangaza tena.
Mama yangu mzazi alimpigia simu wife kumuuliza kwanini alikuwa anampigia usiku wa manane, hii ikiwa na maana kuwa namba hii ya wife ilionekana ikimpigia mama yangu mzazi pia usiku ule ule hali ya kuwa haikuwa na salio na kwenye simu ya wife hakuna call history wala hakuna salio la kupiga wala kubeep.
Sasa kitu kinachochagiza wasiwasi kwenye hili ni kwamba namba hii anayotumia wife ni namba iliyokuwa ikitumiwa na marehemu bibi yangu mzaa mama kama namba ya akiba na ina usajili kamili wa marehemu bibi ambae alifariki mwaka jana.
Hapa ndo kidogo pamefanya tuwe na wasiwasi.
Mimi kichwani mpaka sasa nina maswali mawili, kwamba je inawezekana likawa ni swala la kimtandao? au ni jambo linalohusiana na mambo ya giza kutokana na kua namba hii ilikua ikitumiwa na marehemu bibi yangu?
Kiukweli nimeshindwa kabisa kuelewa mpaka sasa. Naombeni msaada wa mawazo yenu jamani kwa ambao huenda mnafahamu au mmewai kuona mambo kama haya.
Ipo hivi, siku ya juzi tar 19 majira ya saa sita kasoro usiku nikiwa nimelala fofofo, simu yangu ambayo ilikuwa kwenye 'vibration mode' ilikuwa ikiita.
Wife kwakuwa alikuwa bado hajalala akawa ananiamsha niipokee lakini kabla hajafanikiwa kuniamsha akashangazwa kuona namba iliyokuwa inanipigia ni namba yake mwenyewe ambayo anatumia kwenye simu yake na wakati huo simu yake akiwa nayo mkononi, cha kushangaza zaidi ni kuwa simu yake haikuwa na salio la kuweza kupiga wala kubeep na haikuwa inaonesha kama inapiga simu, lakini kwenye simu yangu inaonekana ni namba yake ndiyo inapiga, namba yake ambayo nimeisave vizuri kabisa.
Wife akaamua kupokea mwenyewe tu ili aone ni kitu gani. Hakukuwa na sauti yoyote iliyosikika na yeye pia hakuongea chochote. Akawa ameiskilizia mpaka sekunde ya 31 akakata.
Kwakuwa nilikuwa nimechoka sana wife hakutaka kuniamsha na badala yake akaja kunielezea kila kitu asubuhi ambapo iliingia habari nyingine ya kushangaza tena.
Mama yangu mzazi alimpigia simu wife kumuuliza kwanini alikuwa anampigia usiku wa manane, hii ikiwa na maana kuwa namba hii ya wife ilionekana ikimpigia mama yangu mzazi pia usiku ule ule hali ya kuwa haikuwa na salio na kwenye simu ya wife hakuna call history wala hakuna salio la kupiga wala kubeep.
Sasa kitu kinachochagiza wasiwasi kwenye hili ni kwamba namba hii anayotumia wife ni namba iliyokuwa ikitumiwa na marehemu bibi yangu mzaa mama kama namba ya akiba na ina usajili kamili wa marehemu bibi ambae alifariki mwaka jana.
Hapa ndo kidogo pamefanya tuwe na wasiwasi.
Mimi kichwani mpaka sasa nina maswali mawili, kwamba je inawezekana likawa ni swala la kimtandao? au ni jambo linalohusiana na mambo ya giza kutokana na kua namba hii ilikua ikitumiwa na marehemu bibi yangu?
Kiukweli nimeshindwa kabisa kuelewa mpaka sasa. Naombeni msaada wa mawazo yenu jamani kwa ambao huenda mnafahamu au mmewai kuona mambo kama haya.