Naomba mawazo yako yanisaidie

Naomba mawazo yako yanisaidie

jaqfantasy212

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2012
Posts
542
Reaction score
258
Habari wakuu!!

Naona mwaka huu unataka kuwa wa majanga kwangu

Nimepata ujauzito ila mwanaume mwenyewe simsomi mahusiano yetu yapo yapo tu ilimrad..

Hapa nilipo nawaza mpk kichwa kinataka kupasuka, nawaza sijui niutoe lakin sijui pa kuanzia sijawah kutoa mimba

Nikisema nizae, mtu mwenyewe simsomi tupotupo tu

Kiumri nina miaka 27 simtegemei mtu na hata mtoto naweza kumlea mwenyewe..

Ila hofu yangu tu ni aina ya mahusiano tuliyonayo ndio inayonipa shida..

Naomba mawazo yako tafadhal
 
jack, as long as umesema una uwezo wa kulea mtoto mwenyewe bila company,

nakushauri dada we tulia uzae... unaweza kutoa hiyo mimba ikatoka na kizazi chote.. utajuta!!

km tatizo ni mwanaume, ongea nae usikie anakwambia nini, kama anazingua basi tupa kule..!!

jambo la msingi tu we lea mimba kwa amani tu....!!!
 
Lea ujauzito tu ndugu huyo jamaa kama hasomeki we piga chini.
Kuabort kuna mambo mengi pia imani zote zinapinga hilo swala.
BTW pole sana.
 
Mwenyewe unasema una uwezo wa kumlea mwenyeww bila kampani sasa hayo mawazo ya kuabort yanatoka wapi?
 
Usiutoe tafadhali, tena wewe una bahati unaweza kulea mwenyewe
 


be miss independent.
 
Last edited by a moderator:
Achana na mawazo ya kutoa mimba, Huyo ni mtoto asiye na hatia kwa nini umuhukumu kifo ?????

Zaa na umlee kwa amani zote, utaja ona matokeo ya huyo asieeleweka
 
Ulisahau siku ya kalenda kwa utamu wa penzi, any way usiitoe mimba hiyo
 
Usiutoe tafadhali, tena wewe una bahati unaweza kulea mwenyewe
watu wanatoa sababu hawana uwezo wa kulea yeye anao uwezo kwanini atake kutoa by the way kutoa always huwa ni last option ikiwa kila kitu kimeenda ndivyo sivyo kwakwe ndio kwanza mwanzo. hapaswi kutoa at all cost hasa ukizingatia anao uwezo
 
watu wanatoa sababu hawana uwezo wa kulea yeye anao uwezo kwanini atake kutoa by the way kutoa always huwa ni last option ikiwa kila kitu kimeenda ndivyo sivyo kwakwe ndio kwanza mwanzo. hapaswi kutoa at all cost hasa ukizingatia anao uwezo
Umeona hilo mkuu, safi sana

Na kwa upande wangu hata hao ambao hawana uwezo, sishauri watoe, kama unajua hali yako ngumu kwanini ulikubali kushika ujauzito? au kwanini ulikubali kufanya zinaa(ngono nzembe) huku ukijua outcome yake ni ujauzito/magonjwa ya zinaa?

Kama ikishatokea inabidi ukubali matokeo
 
Umeona hilo mkuu, safi sana

Na kwa upande wangu hata hao ambao hawana uwezo, sishauri watoe, kama unajua hali yako ngumu kwanini ulikubali kushika ujauzito? au kwanini ulikubali kufanya zinaa(ngono nzembe) huku ukijua outcome yake ni ujauzito/magonjwa ya zinaa?

Kama ikishatokea inabidi ukubali matokeo

la kujitakia halina majuto.
 
mmmh pole dada, nikushauri fumba macho sali anza mwanzo mpya..
ki umri umesogea sana na mavyakula haya ya siku izi we zaa tuu huyo,,usichelewe ase...
tomorrow never comes....
 
Una umri gani? Mbona ulichokiandika kinafanana na fikra za binti wa kidato cha pili? Unataka kusema hiyo mimba iliingia kwa bahati mbaya? Kama ni hivyo basi hustahili kuwa na huo umri uliotutajia. Unasema una uwezo wa kumlea mtoto ajaye peke yako halafu unasema unataka kuitoa mimba, mbona hueleweki? Sasa unataka tukushauri nini? Kama unaweza kumlea mtoto peke yako hayo mawazo ya kutoa mimba yanatokea wapi? Unasema humuelewi huyo mchumba wako, sawa ila hilo ni tatizo lako la uvivu wa kuchagua, mtoto wa tumboni mwako haimuhusu sasa kwanini umuue? Ndiyo huo ni uuaji. Kwa umri wako unatambua lipi jema na lipi baya fanya vyovyote unavyotaka hata nikikuambia usitoe neno langu si sheria.
 
Una umri gani? Mbona ulichokiandika kinafanana na fikra za binti wa kidato cha pili? Unataka kusema hiyo mimba iliingia kwa bahati mbaya? Kama ni hivyo basi hustahili kuwa na huo umri uliotutajia. Unasema una uwezo wa kumlea mtoto ajaye peke yako halafu unasema unataka kuitoa mimba, mbona hueleweki? Sasa unataka tukushauri nini? Kama unaweza kumlea mtoto peke yako hayo mawazo ya kutoa mimba yanatokea wapi? Unasema humuelewi huyo mchumba wako, sawa ila hilo ni tatizo lako la uvivu wa kuchagua, mtoto wa tumboni mwako haimuhusu sasa kwanini umuue? Ndiyo huo ni uuaji. Kwa umri wako unatambua lipi jema na lipi baya fanya vyovyote unavyotaka hata nikikuambia usitoe neno langu si sheria.
Tatizo lako umekuwa na kiherehere cha kuandika kabla husoma vizur na kuelewa..

Rudia kusoma vizur ndio utoe ushaur acha kudandia tren kwa mbele
 
Back
Top Bottom