naomba kukazia maneno sahihi ya kiswahili na matumizi yake

Miss Judith nadhani neno kufariki ni sahihi, huwezi kuweka neno kufa kama mbadala wa kufariki, mfano ukitaka sema kuwa fulani "kafa", ni sahihi kusema "fulani kafariki dunia" , japo hata neo kufa ni sahihi hasa kueleza tendo la kufariki!
 
Miss Judith nadhani neno kufariki ni sahihi, huwezi kuweka neno kufa kama mbadala wa kufariki, mfano ukitaka sema kuwa fulani "kafa", ni sahihi kusema "fulani kafariki dunia" , japo hata neo kufa ni sahihi hasa kueleza tendo la kufariki!

kufariki dunia ni nahau ikiwa na maana ya kutengana (separate) na dunia. neno fariki limetokana na neno faraka. hivyo mtu anayekufa anakuwa amefarakana (ametengana au kwa kingerza ame-separate) na dunia na ndiyo iasema "amefariki dunia". kwa hiyo neno sahihi ni kufa na kufariki dunia ni nahau inayokusudia kukata makali ya neno lenyewe. ni sawa na kusema fulani "anajamiiana" na fulani kwa lengo la kupunguza ukali wa neno halisi wakati neno lake sahihi linajulikana na kila mtu
 
Hapa nadhani sahihi ni ....ama....au... Neno aidha, lina maana na matumizi tofauti.

mpendwa, kila lugha iliyosanifiwa ina kanuni zake za kisarufi. sarufi ya kiswahili na kiingereza ni tofauti. wengi wanatumia "aidha... au..." kwakufuatisha sarufi ya kiingereza ya ".... either... or...." ukitumia "aidha" hupaswi kutumia "au" pia ukitumia "au" huhitaji kutumia "ama". mifano ifuatayo inafafanua zaidi juu ya matumizi ya maneno haya:
1. aidha, mheshimiwa spika alinukuu kanuni ya 68 na kumzuia mh. lema kuzungumza
2. mh. spika alimtaka mh. lema kutoa ushahidi wa madai yake hayo au kufuta kauli yake
3. mh. spika alifafanua kuwa mh. lema anatakiwa kutoa ushahidi wake papo hapo ama atakabiliwa na azimio la bunge

NB:
wengine pia huchanganya na kusema mfano
a) "mh. spika alifafanua kuwa mh. lema anatakiwa kutoa ushahidi wake papo hapo ama sivyo atakabiliwa na azimio la bunge"

hayo nayo ni makosa. usahihi wake ni:

b) "mh. spika alifafanua kuwa mh. lema anatakiwa kutoa ushahidi wake papo hapo la sivyo akabiliwa na azimio la bunge"

nadhani tuko pamoja sasa

Glory to God
 
ndugu yangu BAK yote ni sahihi na yana maana tofauti. swala linatokana na mambo ya ibada hasa ya kiislamu, kwa ibada za kikristu wanatumia sala zaidi lakini yote yana maana sawa au inayokaribiana na prayer/worship kwa kingereza. ila hilo la pili la "suala" linamaanisha " an isshue" kwa kiingereza na wingi wake ni masuala yaani issues. huo ndio usahihi wake na yapaswa kutumika hivyo kote bara na visiwani.

Glory to God
Wataalamu wa kudadavua kiswahili hukubaliana kwa jambo hili: kiswahili cha bara hakifanani kwa kila kitu na kile cha visiwani ila vyote ni sanifu kulingana na sehemu. Mfano; markiti na soko, nyimbo na wimbo, afisi na ofisi,skuli na shule, jaa na jalala.... Ahsanteni sana kwa utulivu wenu
 
mpendwa, kila lugha iliyosanifiwa ina kanuni zake za kisarufi. sarufi ya kiswahili na kiingereza ni tofauti. wengi wanatumia "aidha... au..." kwakufuatisha sarufi ya kiingereza ya ".... either... or...." ukitumia "aidha" hupaswi kutumia "au" pia ukitumia "au" huhitaji kutumia "ama". mifano ifuatayo inafafanua zaidi juu ya matumizi ya maneno haya:
1. aidha, mheshimiwa spika alinukuu kanuni ya 68 na kumzuia mh. lema kuzungumza
2. mh. spika alimtaka mh. lema kutoa ushahidi wa madai yake hayo au kufuta kauli yake
3. mh. spika alifafanua kuwa mh. lema anatakiwa kutoa ushahidi wake papo hapo ama atakabiliwa na azimio la bunge

NB:
wengine pia huchanganya na kusema mfano
a) "mh. spika alifafanua kuwa mh. lema anatakiwa kutoa ushahidi wake papo hapo ama sivyo atakabiliwa na azimio la bunge"

hayo nayo ni makosa. usahihi wake ni:

b) "mh. spika alifafanua kuwa mh. lema anatakiwa kutoa ushahidi wake papo hapo la sivyo akabiliwa na azimio la bunge"

nadhani tuko pamoja sasa

Glory to God
Dada Judith nakubaliana na wewe kwamba kila lugha ina kanuni zake za kisarufi. Aidha, nakubaliana na wewe kuwa watu wengi huchanganya matumizi ya maneno aidha..au kwa kudhani yana ufanano na maneno either ...or.. ya lugha ya kiingereza. Kama nilivyobainisha awali maneno ya kiswahili yanayotumika kwa kanuni ile ile ya kiingereza ya matumizi ya maneno either ...or.. ni ama....au....Kwa mfano:-
Mheshimiwa Spika alimtaka Mheshimiwas Godbless Lema ama akanushe kauli yake au athibitishe kwa maandishi kama atakavyoelekezwa kwa mujibu wa Kanuni za Bunge.
Nakubaliana na wewe pia kwa matumizi ya maneno ama sivyo ambayo kwa kawaida hutumika kuonyesha msisitizo au kukazia jambo kwa wasikilizaji.
Neno aidha husimama badala ya maeno yafutayo: isitoshe, kadhalika, pia, au vilevile. Kwa maana hizo haliwezi kuchomoka ghafla mwanzo wa taarifa au mazungumzo. Tuko pamoja.
 
Nina swala kuhusu sarufi.

ipi ni sahihi ?

"The novel that she's writing":
1. "Riwaya anayoiandika"
2. "Riwaya anayoandika"

"the book she's reading":
1. "Kitabu anachokisoma"
2. "Kitabu anachosoma"

Yaani, if the subject is carrying out an action on the direct object, is it enough to just put the "o"- of reference (=yo, cho, etc.) in the verb or does the object infix (=yoi, choki, etc.) have to be there too?

It confuses me because i've seen people do both, it's like there's no correct rule and people just write what they want to write...
 
Nina swala kuhusu sarufi.

ipi ni sahihi ?

"The novel that she's writing":
1. "Riwaya anayoiandika"
2. "Riwaya anayoandika"

"the book she's reading":
1. "Kitabu anachokisoma"
2. "Kitabu anachosoma"

Yaani, if the subject is carrying out an action on the direct object, is it enough to just put the "o"- of reference (=yo, cho, etc.) in the verb or does the object infix (=yoi, choki, etc.) have to be there too?

It confuses me because i've seen people do both, it's like there's no correct rule and people just write what they want to write...

mpendwa,

ni rahisi kwa kiingereza kutofautisha simple present tense (SPT) na present continuous tense (PCT)

sentensi ulizotoa kwa kiingereza zote ziko katika present continous tense zikianzia na object yaani kitendwa. katika simple present tense zingekuwa
1. the novel that she writes
2. the book she reads

kwa hizo za kiswahili zote ni sawa ila #1 ni wakati uliopo unaoendelea (PCT) na #2 ni wakati uliopo (SPT)

infix ya mwanzo husimama kuakisi object na inayofuatia huakisi wakati uliopo na unaendelea. kama wakati ni uliopo (usioendelea) basi infix ya kwanza tu yatosha.

thanks

sisi tumekuwa safi kwa sababu ya lile neno
 
Napenda kuchangia kidogo kuhusu hili la "irabu unganishi au dipthong kwa Kiingereza". Hii hufanyika zinapofuatana irabu mbili, hasa i+a, i+e, i+o, i+u (kama vile amkia, ndie, ndio). Tunaweza kuandika kama zilivyo hapo, lakini wakati wa matamshi huwa tunatamka na y mbele ya irabu ya kwanza bila kujizuwia (amkiya, ndiye, ndiyo). Kwa sababu hiyo, wengine huandika kama wanavyotamka. Mifano mengine ni u+a kama kwenye suala kwa swala, suali kwa swali. Bado hakuna makubaliano ya vipi kuandika maneno haya yenye irabu uanganishi.
 
Nachelea kukubaliana nawe kwa kila kitu. Mf. ndiwe tayari limebeba ile dhana ya wewe ndani yake. Huwezi kusema ndiwe wewe utakuwa umerudia neno wewe mara 2. kwa hiyo ndio wewe ni sahihi pia likimaanisha ndiwe. Pili tokea nje unamaana tokea nje uelekee ndani, wakati dhana ambayo unataka kuizungumzia hapa ni elekea nje. toka ndani ni sahihi pia. Na pia kuna mengine machache ambayo sikubalini nawe hapo juu. Inaonekana wewe unatumia kiswahili cha lahaja fulani zaidi na utaipenda zaidi hiyo ukiamini ndicho sahihi.

mazoea yanaweza kufanya maneno fulani yaonekane kuwa yanatumika kwa usahihi, lakini ukweli ni kinyume chake. mfano haya yafuatayo"

1. siyo, sahihi ni sio
2. ndiyo, sahihi ni ndio
3. ndio yeye, sahihi ni ndiye yeye
4. ndio wewe, shihi ni ndiwe wewe
5. ndio mimi, sahihi ni ndimi mimi
6. hichi, sahihi ni hiki
7. liwalo lote, sahihi ni lolote liwalo
8. onyesha, sahihi ni onesha
9. maonyesho, sahihi ni maonesho,
10. aidha... au..., sahihi ni aidha,..../......au......
11. siyo... wala...., sahihi ni si.... wala.....
12. kufariki, sahihi ni kufa
13. (fulani) anachechemea, sahihi ni (fulani) anachehechema/anachechemeka
14. shuka juu, sahihi ni shuka chini
15. toka nje, sahihi ni tokea nje/toka ndani
16. ukweli, sahihi ni kweli
17. uoga, sahihi ni woga
18. nk.

wengine mwaweza kuongeza ama kusahihisha.
wapendwa tukienzi kiswahili.

Glory to God
 
Wataalamu wa kudadavua kiswahili hukubaliana kwa jambo hili: kiswahili cha bara hakifanani kwa kila kitu na kile cha visiwani ila vyote ni sanifu kulingana na sehemu. Mfano; markiti na soko, nyimbo na wimbo, afisi na ofisi,skuli na shule, jaa na jalala.... Ahsanteni sana kwa utulivu wenu
nakubaliana nawe kuhusu kiswahili cha bara na visiwani. Lakini, kuhusu nyimbo na wimbo sikubaliani nawe. Wimbo ni umoja wakati nyimbo ni wingi. Kwa hiyo "wimbo wa JD ni mzuri sana". Nyimbo za JD ni nzuri sana" Hii dhana ya watu kusema "ile nyimbo yake niliipenda" ni uharibifu wa lugha. Hakuna upatanishon wa sarufi hapo (wingi na umoja). Nachukia sana watu wa redioni wanaposema hivyo.
 
Hapa nadhani sahihi ni ....ama....au... Neno aidha, lina maana na matumizi tofauti.

nakubali. ni ama......au. neno aidha lipo lakini matumizi yake ni mengine. Lina maanisha "zaidi ya hayo". Mfano. Waziri mkuu alibainisha mpango wa serilaki kupunguza matumizi yasiyo na manufaa. Aidha aliainisha pia kiasi cha fedha zinazotarajiwa kuokolewa kwa mpango huo.
 
Nachelea kukubaliana nawe kwa kila kitu. Mf. ndiwe tayari limebeba ile dhana ya wewe ndani yake. Huwezi kusema ndiwe wewe utakuwa umerudia neno wewe mara 2. kwa hiyo ndio wewe ni sahihi pia likimaanisha ndiwe. Pili tokea nje unamaana tokea nje uelekee ndani, wakati dhana ambayo unataka kuizungumzia hapa ni elekea nje. toka ndani ni sahihi pia. Na pia kuna mengine machache ambayo sikubalini nawe hapo juu. Inaonekana wewe unatumia kiswahili cha lahaja fulani zaidi na utaipenda zaidi hiyo ukiamini ndicho sahihi.

amngalia nilivyomjibu omukuru hapo chini

asante mpendwa
quote_icon.png
Originally Posted by Omukuru
Miss Judith nashukuru umeleta huu mjadala mzuri kabisa. Pamoja na uzuri wa mjadala nina mashaka na usahii wa maana na matumizi ya baadhi ya maneno uliyoyaleta hapo juu.
Mimi nafahamu kwamba neno kama NDIMI tayari liko nafsi ya kwanza umoja. Linatokana na muungano wa kivumishi kitenzi-nomino thibitishi: NDIO na kiwakilishi nafsi MIMI
NDIO+WEWE = NDIWE
NDIO+HII/HIYO = NDIYO
Neno UKWELI liko sahii, na wingi wake ni KWELI. Maana inategemea sana
Nitarudi hapa jamvini kuendeleza uchambuzi na kuleta vielelezo na vyanzo vya maelezo yangu.

nakubaliana nawe mpendwa, katika kiswahili kuna mikazo/misisitizo hutumiwa mara nyingi na huwa katika mtindo wa kurudia mfano mtu akisema "nyumba hihi hii", eneo hilihili, mtu huyu huyu, nk. neno hii linarudiwa kuonesha mkazo au msisitizo. hata unaposema "ndimi", ingetosha tu ila unapotaka kuongeza msisitizo kwa kurudia hilo neno ndio matumizi yake sahihi yapaswa kuwa ndimi mimi na sio "ndio mimi". vivyo hivyo katika ndiwe wewe

nashukuru umafafanua "ndio hii"= ndiyo

tuko pamoja katika kuboresha matumizi ya kiswahili.

Glory to God​
 
Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili-Kiingereza ya TUKI (UDSM) maneno yafuatayo ni sahihi kwa maana zifuatazo:

ndiyo kl yes, yeah.
sio nm [i-/zi-] broken pot.
siyo ki no, not so.
onyesh.a kt [ele] show, exhibit, demonstrate.


Hivyo dada Juddy unahitaji kutazama tena marejeo (reference) yako. Aidha navyofahamu hakuna neno "ndio" katika lugha ya Kiswahili.

[FONT=arial, helvetica, sans-serif][/FONT]
 
mazoea yanaweza kufanya maneno fulani yaonekane kuwa yanatumika kwa usahihi, lakini ukweli ni kinyume chake. mfano haya yafuatayo"

1. siyo, sahihi ni sio
2. ndiyo, sahihi ni ndio
3. ndio yeye, sahihi ni ndiye yeye
4. ndio wewe, shihi ni ndiwe wewe
5. ndio mimi, sahihi ni ndimi mimi
6. hichi, sahihi ni hiki
7. liwalo lote, sahihi ni lolote liwalo
8. onyesha, sahihi ni onesha
9. maonyesho, sahihi ni maonesho,
10. aidha... au..., sahihi ni aidha,..../......au......
11. siyo... wala...., sahihi ni si.... wala.....
12. kufariki, sahihi ni kufa
13. (fulani) anachechemea, sahihi ni (fulani) anachehechema/anachechemeka
14. shuka juu, sahihi ni shuka chini
15. toka nje, sahihi ni tokea nje/toka ndani
16. ukweli, sahihi ni kweli
17. uoga, sahihi ni woga
18. nk.

wengine mwaweza kuongeza ama kusahihisha.
wapendwa tukienzi kiswahili.

Glory to God

sitosema sn hapa lkn tujiulize hiki kiswahili sanifu/sahihi kinaweza kutuvusha katika hili wimbi la utandawazi? je mwaonaje sasa JF iweze kuanzisha mtandao wakujifunza kiingereza kwa kutumia audios au vidios zitakazo wawezesha baadhi ya wenzetu wasioweza vizuri kujifunza?
 
kufariki dunia ni nahau ikiwa na maana ya kutengana (separate) na dunia. neno fariki limetokana na neno faraka. hivyo mtu anayekufa anakuwa amefarakana (ametengana au kwa kingerza ame-separate) na dunia na ndiyo iasema "amefariki dunia". kwa hiyo neno sahihi ni kufa na kufariki dunia ni nahau inayokusudia kukata makali ya neno lenyewe. ni sawa na kusema fulani "anajamiiana" na fulani kwa lengo la kupunguza ukali wa neno halisi wakati neno lake sahihi linajulikana na kila mtu

Haswaa! Ni lazima lugha iwe tamu kimatamshi na pia ilete usikivu mzuri na usio na mtazamo wa kejeli au kukifu/kinyaa.
Mfano:
Ebwanae umesikia?
Ndugu yetu Allikobwa 'kafa'
kwa kauli kama hiyo unaweza kuona mapokeo yake si mazuri hasa tukichukulia kifo au msiba si jambo la mzaha.
Hapa ndipo wanalugha wakashauri zitumiwe zaidi Tafsida au nahau/misemo kupunguza ukali wa maneno.
Mf. Kuaga dunia, kata kamba/uzi, ametutoka, kututupa mkono na n.k.
Kwa mwendo huo basi ndo lugha hufanywa pambo ktk mazungumzo na maandishi yetu.
Kidumishwe Kiswahili.
 
sitosema sn hapa lkn tujiulize hiki kiswahili sanifu/sahihi kinaweza kutuvusha katika hili wimbi la utandawazi? je mwaonaje sasa JF iweze kuanzisha mtandao wakujifunza kiingereza kwa kutumia audios au vidios zitakazo wawezesha baadhi ya wenzetu wasioweza vizuri kujifunza?

hapo penye wino mkolezo, jibu langu ni: bila shaka !!
 
hapo penye wino mkolezo, jibu langu ni: bila shaka !!

Iwapo sie wazungumzaji wa lugha hii tunaendelea kudumu ktk mfumo huu bila shaka na lugha yetu itadumu na kuimarika na kugangamala ktk kila dhoruba.
Labda tu sie wazungumzaji tuitupe lugha yetu na kuweka mkazo katika lugha za kitawala za dunia hii mf. Kiingereza, kifaransa, kireno na n.k.
 
Back
Top Bottom