naomba kukazia maneno sahihi ya kiswahili na matumizi yake

Kule visiwani pia wenzetu wanasema suali na sisi bara tunasema swali. Mfano: "sikulielewa suali lako" na "sikulielewa swali lako" neno lipi kati ya haya mawili ni sahihi.
kuhusiana na utofauti wa neno SWALI na SUALI ni hivi, hapa ni kwamba kuna umbo la ndani na umbo la nje mara zote umbo la nje ni vile linavyotamkwa wakati umbo la ndani ni kwa kuzingatia asili ya neno lenyewe, hivyo neno SWALI linatokana na neno la asili SUALA, lakini lugha ya kiswahili ina kanuni zake, kwa mfano, kanuni ya uyeyushaji ndiyo inatupatia neno SWALI, yaani'
U+A=WA yaani
S(U+A)LI=SWALI..
Hii ina maana kuwa wa-zanzibari wana wanapendelea kutumia na kutamka umbo la ndani la neno hilo wakati wa-bara (TZ) wanatumia umbo la nje katika kutamka.

UZIADA: Hata hivyo,kanuni hii hatuwezi kuitumia katika neno SUALA ili kupunguza utata utakaojitokeza mfn;
SWALA,yaweza kuwa ibada (worship), au myama wa porini jamii ya mbuzi, hivyo itabakia kuwa SUALA badala ya S(U+A)LA=(yaani)
SWALA.
NAWASILISHA...
 
Miss Judith nashukuru umeleta huu mjadala mzuri kabisa. Pamoja na uzuri wa mjadala nina mashaka na usahii wa maana na matumizi ya baadhi ya maneno uliyoyaleta hapo juu.
Mimi nafahamu kwamba neno kama NDIMI tayari liko nafsi ya kwanza umoja. Linatokana na muungano wa kivumishi kitenzi-nomino thibitishi: NDIO na kiwakilishi nafsi MIMI
NDIO+WEWE = NDIWE
NDIO+HII/HIYO = NDIYO
Neno UKWELI liko sahii, na wingi wake ni KWELI. Maana inategemea sana
Nitarudi hapa jamvini kuendeleza uchambuzi na kuleta vielelezo na vyanzo vya maelezo yangu.

Wewe umenena. Miss Judith alitaka kunichanga nya kabisa. Maneno takriban yote aliyoandika ni sahihi isipokuwa yana matumizi tofauti. Mfano maneno ya NDIYO na NDIO.
 
Back
Top Bottom