Nanunua nguo kila ninapokutana na machinga hata kama sizihitaji, nifanyeje kuondokana na tabia hii?

Kuna nyumba niliingia yule kaka ana viatu nahisi pea 100 zinafika. Nae akadai kama wewe hivyo hivyo akifika mahala akaona kiatu kizuri ananunua awe anauhitaji au la ilimradi kimemvutia anabeba.
 
Nani mwingine ana zoea kama la kwangu la kununua nguo kila unapoletewa na mtembezaji. Nikikaa home naona nimejaza sana nguo hata ambazo sizivai masanduku Kwa makabati Mpaka chumba kinageuka kero kinanuka nguo(mitumba hasa +dukani).

Kila nikitaka kuzigawa nashindwa nianzie wapi ama nimpe nani na hata kama nikimpa mhitaji siku moja moja awe mnywaji mwenzangu au mzoa taka basi nitaishia kumchagulia dosho kadhaa moja au mbili na sio nguo kali ya fashion zile nzuri zinazoita ingawa sizivai hata mwaka mzima.

Kugawa imekuwa ni kama nataka, sitaki maana kuna kipindi unachafua nguo zote zile code za kwendA ila bado unakuwa na mzigo wa akiba still unatoka nazo Safi kwenye mishe.

Sasa cha ajabu najua Nina nguo kibao ila bado Nikikaa bar au kitaa ikaletwa nguo naiona kazi nzuri hii lazima nilipe hela.

Hii sijui tunaita ulafi, uchoyo au roho mbaya au ubinafsi Kwa maana akili Kiukweli inataman jambo moja niwe na nguo chache ila nzuri na mambo yataenda tu fresh mfano form six zako kali 5,jeans na cardet 10 kali, t shirt 5, boxer 10 kali.

Inakuwa imeisha Sasa Mara makanzu kibao, makoti kibao, ma suruali ya mwaka juzi, mashati ya 2021. Chumba kinatia Mpaka uvivu kupumzika Kwa utuli.
Zamani nilikuwa chizi kama wewe, lakini sasa hivi sioni muhimu tena kununuanunua kama wewe,
Mwaka jana nilipaki mizigo kwenye shangazi kaja kwa ajili ya kijijini, bado nitafanya hivyo tena mwaka huu.
Nataka nibaki na pea 10 ya kila kitu, japo ukiwa na mzigo mkubwa unavaa tu.
Jifunze kutembea na pesa kidogo kwenye wallet. Sio kila unachoona unanunua, ukiwa Bar wakipitishapitisha jifanye huwaoni.
 
Kua na nguo nyingi sana sio kitu kibaya kwa sababu inafanya unakua na options nyingi na unakua huchakazi nguo kwa sababu unaivaa mara chache ndani ya muda mrefu. Muhimu tu ni kuhakikisha unanunua nguo nzuri kweli kweli ili usije jikuta unakua na nguo nyingi ambazo hazieleweki
 
Hivi Tanzania kitu kama hichi hakijafika hadi zama hizi?


Ni wakati sasa watu waanzishe vitu kama hivyo kuondoa kadhia ya kitu/vitu usivyokuwa na uhitaji navyo tena basi jua kuna mtu/watu wana uhitaji navyo sio vya kutupa.
 
Back
Top Bottom