Maneno yenye busara.Maneno Makali ya AFANDE SELE kutoka Instagram Kwa MRISHO MPOTO na Majibu ya MPOTO kwa AFANDE SELE...
Afande Sele King - Rafiki yangu mkubwa mjomba mpoto kama ni kweli wewe ndio ulikua kinara ktk kusimamia utayarishaji wa wimbo maalumu wa kuhamasisha uzalendo kwa taifa halafu ukashawishi kuondolewa kwa baadhi ya wasanii wazawa ndani ya wimbo huo na badala yake ukampa nafasi rafiki yetu christian bella kushiriki ktk wimbo huo unaowahusu watanzania wkt ukijua wazi kuwa bella pamoja na ukweli ni rafiki yetu sana lkn bado yeye sio mtz bali ni mcongoman....ktk hili mjomba umetukosea sana watanzania wenzako na kwa hakika kama ingekua kitendo chako hicho umekifanya kwa nchi zilizoshiba uzalendo na zisizovaa joho la unafki mjomba ulistahili kukatwa nywele zako na kupigwa risasi angalau tano kichwani kwa uchache tena hadharani kwani ulichofanya ni usaliti kwa nchi yako na ni aina flani ya uhaini...
Majibu
Mrisho Mpoto Akijibu - Kaka yangu @afandeseleking Bado narudia kusema kwamba heshima nnayokupa inatoka Mbali sana kwenye chumba cha nne cha moyo Wangu... Sihitaji kupoteza wino Mwingi kukukumbusha tofauti iliyopo kati ya UZALENDO, UZAWA na URAIA kwasababu nina uhakika unazifahamu vyema isipokuwa huenda leo haujaamkia ule ubavu sahihi na ule wa ukarimu wako ulionao siku zote, mpaka ukakataa uwepo wangu hapa Duniani Kwa kunichagulia adhabu ya kupigwa risasi tano tena za kichwa... kwakua hukuniuliza hili jambo kabla Itoshe kusema hunitaki tena...hivyo basi kabla sijapigwa hizo risasi tano nitakachofanya ni kukupa maelezo machache yatakayokufanya uipate picha ya UZALENDO.. Hivi unajua kama John Okello alipigania uhuru wa Zanzibar!? Majeshi yetu yamepigania uhuru wa msumbiji na hata Chegu sio mcuba na alipigania uhuru wa Cuba na Congo pia.. Na je unajua kama kuna wazawa wanaoangamiza maslahi ya nchi na kuna wazalendo wasiobagua!? Kaka, Afrika ni moja na waafrika wote ni ndugu zetu ( umajumui Afrika, tena ukichimba huko sana kwa hapa nchini utakuna na Prof Shivji) .. na ndio maana hata mwenge wa uhuru uliwekwa juu ya mlima kilimanjaro ili kumulikia nchi nyingine.. Kumbuka hiyo mitizamo ya KIUZAWA Mwalimu aliita mitizamo membamba.. kwa maana ya kwamba ipo kwa ajili ya Kuiangamiza afrika
Na mwisho ningependa kukuuliza--->Je umezisikia shangwe za wazalendo na wazawa leo hapa dodoma baada ya kusikia Babu Seya na familia yake wamepewa msamaha wa rais!!? Wewe ni RASTA kaka.. kumbuka siku zote CHUKI HUMUUMIZA ANAYEIHIFADHI.. [HASHTAG]#AfrikaUnite[/HASHTAG] ✊
Nani yupo sahihi kati ya hawa mafahari wawili?
Je kuwa Mzalendo ni lazima uwe mzawa wa nchi husika?
OkMrisho mpoto amemaliza kila kitu
Ila hapa mrisho mpoto kajibu kwa akili sana!!!
yaani akili zako na mpoto ni sawa, unataka jeshi la marekani liwe na wahindi wekundu (wenyeji wa kule ambao ni asilimia 2% huku 98 ni wahamiaji.Mpoto yuko sawa sana hii dhana ya uzawa iko kwa nchi maskini sana pia inachangiwa sana na ubinafsi uliokubuhu kama jambo linafanyika kwa maslah mapana ya nchi hakuna haja yakuangalia ni nan anayelifanya ndio maana kwenye jesh la marekan kunawapare kibao mpaka wamatengo tukija kwenye soka ufaransa ni mfano tosha na balaa lake wote tunalijua namaliza kwakusema afande mbinafsi kwa kiwango cha kawaida kabisa
Kama nilivotangulia kusema awali hii dhana ya uzawa ni dhana ya watu wabinafsi kupindukia na most of them ni kutoka mataifa duni kupindukia justin bieber sio mmarekan anold schwazniger sio mmarekan celine dion pia ni mkanada unless kama case study yako ni north korea au somalia mpoto yuko sawa kabisa unless kama hilo shavu angempa fally ipupa ila mzee wa masauti tuko nae mitaani uku na punde anaukana uraia wake wa kongo nyie bado mnamuona sio mzalendoy
yaani akili zako na mpoto ni sawa, unataka jeshi la marekani liwe na wahindi wekundu (wenyeji wa kule ambao ni asilimia 2% huku 98 ni wahamiaji.
unaongelea ufaransa wanao amini kwenye assimilation pilicy na kuwaona watu toka makoloni yako kuwa sawa na wafaransa asili
mbona mnakuja na mifano ya kijinga jinga ko wataka twambia tz wakongo ni wengi kuliko watanzani, wataka tukuamini wakongo ni sawa na watanzania asili
acheni mambo hayo mrisho kachemka kafata umaarufu wa bella ila sio uzalendo. kwanza mwenyewe tu uzalendo wake unatia shaka vp kuhusu bella.
Maneno Makali ya AFANDE SELE kutoka Instagram Kwa MRISHO MPOTO na Majibu ya MPOTO kwa AFANDE SELE...
Afande Sele King - Rafiki yangu mkubwa mjomba mpoto kama ni kweli wewe ndio ulikua kinara ktk kusimamia utayarishaji wa wimbo maalumu wa kuhamasisha uzalendo kwa taifa halafu ukashawishi kuondolewa kwa baadhi ya wasanii wazawa ndani ya wimbo huo na badala yake ukampa nafasi rafiki yetu christian bella kushiriki ktk wimbo huo unaowahusu watanzania wkt ukijua wazi kuwa bella pamoja na ukweli ni rafiki yetu sana lkn bado yeye sio mtz bali ni mcongoman....ktk hili mjomba umetukosea sana watanzania wenzako na kwa hakika kama ingekua kitendo chako hicho umekifanya kwa nchi zilizoshiba uzalendo na zisizovaa joho la unafki mjomba ulistahili kukatwa nywele zako na kupigwa risasi angalau tano kichwani kwa uchache tena hadharani kwani ulichofanya ni usaliti kwa nchi yako na ni aina flani ya uhaini...
Majibu
Mrisho Mpoto Akijibu - Kaka yangu @afandeseleking Bado narudia kusema kwamba heshima nnayokupa inatoka Mbali sana kwenye chumba cha nne cha moyo Wangu... Sihitaji kupoteza wino Mwingi kukukumbusha tofauti iliyopo kati ya UZALENDO, UZAWA na URAIA kwasababu nina uhakika unazifahamu vyema isipokuwa huenda leo haujaamkia ule ubavu sahihi na ule wa ukarimu wako ulionao siku zote, mpaka ukakataa uwepo wangu hapa Duniani Kwa kunichagulia adhabu ya kupigwa risasi tano tena za kichwa... kwakua hukuniuliza hili jambo kabla Itoshe kusema hunitaki tena...hivyo basi kabla sijapigwa hizo risasi tano nitakachofanya ni kukupa maelezo machache yatakayokufanya uipate picha ya UZALENDO.. Hivi unajua kama John Okello alipigania uhuru wa Zanzibar!? Majeshi yetu yamepigania uhuru wa msumbiji na hata Chegu sio mcuba na alipigania uhuru wa Cuba na Congo pia.. Na je unajua kama kuna wazawa wanaoangamiza maslahi ya nchi na kuna wazalendo wasiobagua!? Kaka, Afrika ni moja na waafrika wote ni ndugu zetu ( umajumui Afrika, tena ukichimba huko sana kwa hapa nchini utakuna na Prof Shivji) .. na ndio maana hata mwenge wa uhuru uliwekwa juu ya mlima kilimanjaro ili kumulikia nchi nyingine.. Kumbuka hiyo mitizamo ya KIUZAWA Mwalimu aliita mitizamo membamba.. kwa maana ya kwamba ipo kwa ajili ya Kuiangamiza afrika
Na mwisho ningependa kukuuliza--->Je umezisikia shangwe za wazalendo na wazawa leo hapa dodoma baada ya kusikia Babu Seya na familia yake wamepewa msamaha wa rais!!? Wewe ni RASTA kaka.. kumbuka siku zote CHUKI HUMUUMIZA ANAYEIHIFADHI.. [HASHTAG]#AfrikaUnite[/HASHTAG] ✊
Nani yupo sahihi kati ya hawa mafahari wawili?
Je kuwa Mzalendo ni lazima uwe mzawa wa nchi husika?
Hii imenikumbusha alivowakilisha kenya uko nchi za watu kwenye tamasha la kiswahili japo alijitetea sanaMrisho mpoto ni mnafiki mchumia tumbo,
Kwahiyo anataka kuuaminisha umma yule nyoso ni mzalendo kuliko waliachwa,
Kwanza uzalendo haumasishwa uzalendo unatoka moyoni