Nani yupo sahihi,Afande Sele au Mrisho Mpoto?

Jameni ee ule wimbo ni uzalendo kwa ccm na sio nchi, yaani lundo lote wasanii music ndio kamuona huyo mkongo, labda na yeye ni walewale si wa kigoma yule huenda ni mrundi kwa kwake siyo shida.
 
Maneno Makali ya AFANDE SELE kutoka Instagram Kwa MRISHO MPOTO na Majibu ya MPOTO kwa AFANDE SELE...

Afande Sele King - Rafiki yangu mkubwa mjomba mpoto kama ni kweli wewe ndio ulikua kinara ktk kusimamia utayarishaji wa wimbo maalumu wa kuhamasisha uzalendo kwa taifa halafu ukashawishi kuondolewa kwa baadhi ya wasanii wazawa ndani ya wimbo huo na badala yake ukampa nafasi rafiki yetu christian bella kushiriki ktk wimbo huo unaowahusu watanzania wkt ukijua wazi kuwa bella pamoja na ukweli ni rafiki yetu sana lkn bado yeye sio mtz bali ni mcongoman....ktk hili mjomba umetukosea sana watanzania wenzako na kwa hakika kama ingekua kitendo chako hicho umekifanya kwa nchi zilizoshiba uzalendo na zisizovaa joho la unafki mjomba ulistahili kukatwa nywele zako na kupigwa risasi angalau tano kichwani kwa uchache tena hadharani kwani ulichofanya ni usaliti kwa nchi yako na ni aina flani ya uhaini...

Majibu

Mrisho Mpoto Akijibu - Kaka yangu @afandeseleking Bado narudia kusema kwamba heshima nnayokupa inatoka Mbali sana kwenye chumba cha nne cha moyo Wangu... Sihitaji kupoteza wino Mwingi kukukumbusha tofauti iliyopo kati ya UZALENDO, UZAWA na URAIA kwasababu nina uhakika unazifahamu vyema isipokuwa huenda leo haujaamkia ule ubavu sahihi na ule wa ukarimu wako ulionao siku zote, mpaka ukakataa uwepo wangu hapa Duniani Kwa kunichagulia adhabu ya kupigwa risasi tano tena za kichwa... kwakua hukuniuliza hili jambo kabla Itoshe kusema hunitaki tena...hivyo basi kabla sijapigwa hizo risasi tano nitakachofanya ni kukupa maelezo machache yatakayokufanya uipate picha ya UZALENDO.. Hivi unajua kama John Okello alipigania uhuru wa Zanzibar!? Majeshi yetu yamepigania uhuru wa msumbiji na hata Chegu sio mcuba na alipigania uhuru wa Cuba na Congo pia.. Na je unajua kama kuna wazawa wanaoangamiza maslahi ya nchi na kuna wazalendo wasiobagua!? Kaka, Afrika ni moja na waafrika wote ni ndugu zetu ( umajumui Afrika, tena ukichimba huko sana kwa hapa nchini utakuna na Prof Shivji) .. na ndio maana hata mwenge wa uhuru uliwekwa juu ya mlima kilimanjaro ili kumulikia nchi nyingine.. Kumbuka hiyo mitizamo ya KIUZAWA Mwalimu aliita mitizamo membamba.. kwa maana ya kwamba ipo kwa ajili ya Kuiangamiza afrika

Na mwisho ningependa kukuuliza--->Je umezisikia shangwe za wazalendo na wazawa leo hapa dodoma baada ya kusikia Babu Seya na familia yake wamepewa msamaha wa rais!!? Wewe ni RASTA kaka.. kumbuka siku zote CHUKI HUMUUMIZA ANAYEIHIFADHI.. [HASHTAG]#AfrikaUnite[/HASHTAG] ✊


Nani yupo sahihi kati ya hawa mafahari wawili?
Je kuwa Mzalendo ni lazima uwe mzawa wa nchi husika?
Maneno yenye busara.
 
Mrisho sio mtu ninaemkubali sana, Afande Sele ni kati ya wasanii naowakubali.

Lakini Mrisho anazo hoja za maana zaidi na mifano yenye nguvu sana sijui kama Afande ataweza jibu
 
Afande sele yupo sahihi ila mrisho mpoto ana hoja madhubuti...

Jibu lolote linaweza kuwa sahihi ama si sahihi kutegemeana na sababu za jibu lako.
 
Mrisho alichofanya ni kucheza na fikra kwa kutumia muda mrefu kuandaa jibu. Afande ametoa hoja sahihi kabisa na ina mashiko huwezi kuimbia taifa uzalendo kwa kuacha wasanii wazawa na kumchukua mtu wa taifa jingine ambae si mzawa wa nchi hiyo wakati nchi ina wasanii wazawa. Mrisho amechukua muda mwingi na mifano kutetea hoja na anaonekana kama ameshinda kwa kuwa ameweka na mifano na uenda ameshirikisha hata watu wengine kuandaa jibu kwa Afande.

My take Mrisho kuwa mzalendo kwa kuboost watanzania wenzako huyo mcongo atabaki kuwa mcongo na ata kizazi chake bado kitaitwa wacongo tupeane fursa na kataa kuwa kaa
 
nilicho gundua ni bora kusoma stori za Beira Baby Boy kuliko kusikiliza mawazo ya humu.

yaani mmoja akisema mpoto yuko sahihi basi wafuatao kuchangia wako mkondo huo huo, akianza kwa kusema afande yuko sahihi basi wote afande afande.

sasa mlipewa vichwa vya nini? mpoto analeta mifano ya che guevara kuipigania cuba eti ndo uzalendo pumbavu kabisa. che kazipigania nchi nyingi hadi kongo. sio kwamba alikuwa mzalendo wa nchi izo bali hakupenda utawala wa kibepari yeye ni mzalendo kwa itikadi ya ujamaa (alikuwa tayari kuifia katika nchi yoyote)

mpoto kakosea, aliupima vp? uzalendo wa bella dhidi ya afande ama hao alio watoa. kama tu siamini yule mzalendo # 1 tunamuona ni muharibifu leo tunaanzaje sema eti bella ni mzalendo kuliko walio ondolewa
 
y
Mpoto yuko sawa sana hii dhana ya uzawa iko kwa nchi maskini sana pia inachangiwa sana na ubinafsi uliokubuhu kama jambo linafanyika kwa maslah mapana ya nchi hakuna haja yakuangalia ni nan anayelifanya ndio maana kwenye jesh la marekan kunawapare kibao mpaka wamatengo tukija kwenye soka ufaransa ni mfano tosha na balaa lake wote tunalijua namaliza kwakusema afande mbinafsi kwa kiwango cha kawaida kabisa
yaani akili zako na mpoto ni sawa, unataka jeshi la marekani liwe na wahindi wekundu (wenyeji wa kule ambao ni asilimia 2% huku 98 ni wahamiaji.

unaongelea ufaransa wanao amini kwenye assimilation pilicy na kuwaona watu toka makoloni yako kuwa sawa na wafaransa asili

mbona mnakuja na mifano ya kijinga jinga ko wataka twambia tz wakongo ni wengi kuliko watanzani, wataka tukuamini wakongo ni sawa na watanzania asili

acheni mambo hayo mrisho kachemka kafata umaarufu wa bella ila sio uzalendo. kwanza mwenyewe tu uzalendo wake unatia shaka vp kuhusu bella.
 
tatizo unapowatoa wazawa kwenye shughuli za Taifa lao na kuwaweka wageni Unatumia kigezo gani..........? lengo ni nini.......? Wazawa walioenguliwa wanajisikiaje......?
 
y

yaani akili zako na mpoto ni sawa, unataka jeshi la marekani liwe na wahindi wekundu (wenyeji wa kule ambao ni asilimia 2% huku 98 ni wahamiaji.

unaongelea ufaransa wanao amini kwenye assimilation pilicy na kuwaona watu toka makoloni yako kuwa sawa na wafaransa asili

mbona mnakuja na mifano ya kijinga jinga ko wataka twambia tz wakongo ni wengi kuliko watanzani, wataka tukuamini wakongo ni sawa na watanzania asili

acheni mambo hayo mrisho kachemka kafata umaarufu wa bella ila sio uzalendo. kwanza mwenyewe tu uzalendo wake unatia shaka vp kuhusu bella.
Kama nilivotangulia kusema awali hii dhana ya uzawa ni dhana ya watu wabinafsi kupindukia na most of them ni kutoka mataifa duni kupindukia justin bieber sio mmarekan anold schwazniger sio mmarekan celine dion pia ni mkanada unless kama case study yako ni north korea au somalia mpoto yuko sawa kabisa unless kama hilo shavu angempa fally ipupa ila mzee wa masauti tuko nae mitaani uku na punde anaukana uraia wake wa kongo nyie bado mnamuona sio mzalendo
 
Kwanza hakuna Ras kati yao, hzo rasta ni symbol tu ya USANII wao. Pili hakuna aliye sahihi kwa jinsi nilivyosoma. Kama alivyoeleza mpoto hoja za afande zinakosa mashiko kwa vigezo alivyotumia UZALENDO, UZAWA nk. Lkn Km kuna wanamziki watz Mpoto aliwatoa alipaswa aeleze sababu za kiufundi za kuwatoa kwan nao walikuwa na haki ya kushiriki labda km bela alihitajika sana vocally. Otheryz Mpoto alifanya uhuni kwa sababu za kiswahiba. Haya mengine ya kusema Prof. shivji ni asian me napingana nayo ni low sana, ni sawa na kusema Akon ni mgana. Mtu akishakuwa raia wa kidumu wa nchi fulani kuwa mzalendo ni wajibu wake, so mifano kuwa wakina prof shivji wanapigania nchi, ni uzushi tu. Yeye km msomi na mwanazuoni anafanya wajibu wake na ndivo wasomi wengi wanapaswa kufanya hvo, kuonyesha njia, kukosoa nk
 
Maneno Makali ya AFANDE SELE kutoka Instagram Kwa MRISHO MPOTO na Majibu ya MPOTO kwa AFANDE SELE...

Afande Sele King - Rafiki yangu mkubwa mjomba mpoto kama ni kweli wewe ndio ulikua kinara ktk kusimamia utayarishaji wa wimbo maalumu wa kuhamasisha uzalendo kwa taifa halafu ukashawishi kuondolewa kwa baadhi ya wasanii wazawa ndani ya wimbo huo na badala yake ukampa nafasi rafiki yetu christian bella kushiriki ktk wimbo huo unaowahusu watanzania wkt ukijua wazi kuwa bella pamoja na ukweli ni rafiki yetu sana lkn bado yeye sio mtz bali ni mcongoman....ktk hili mjomba umetukosea sana watanzania wenzako na kwa hakika kama ingekua kitendo chako hicho umekifanya kwa nchi zilizoshiba uzalendo na zisizovaa joho la unafki mjomba ulistahili kukatwa nywele zako na kupigwa risasi angalau tano kichwani kwa uchache tena hadharani kwani ulichofanya ni usaliti kwa nchi yako na ni aina flani ya uhaini...

Majibu

Mrisho Mpoto Akijibu - Kaka yangu @afandeseleking Bado narudia kusema kwamba heshima nnayokupa inatoka Mbali sana kwenye chumba cha nne cha moyo Wangu... Sihitaji kupoteza wino Mwingi kukukumbusha tofauti iliyopo kati ya UZALENDO, UZAWA na URAIA kwasababu nina uhakika unazifahamu vyema isipokuwa huenda leo haujaamkia ule ubavu sahihi na ule wa ukarimu wako ulionao siku zote, mpaka ukakataa uwepo wangu hapa Duniani Kwa kunichagulia adhabu ya kupigwa risasi tano tena za kichwa... kwakua hukuniuliza hili jambo kabla Itoshe kusema hunitaki tena...hivyo basi kabla sijapigwa hizo risasi tano nitakachofanya ni kukupa maelezo machache yatakayokufanya uipate picha ya UZALENDO.. Hivi unajua kama John Okello alipigania uhuru wa Zanzibar!? Majeshi yetu yamepigania uhuru wa msumbiji na hata Chegu sio mcuba na alipigania uhuru wa Cuba na Congo pia.. Na je unajua kama kuna wazawa wanaoangamiza maslahi ya nchi na kuna wazalendo wasiobagua!? Kaka, Afrika ni moja na waafrika wote ni ndugu zetu ( umajumui Afrika, tena ukichimba huko sana kwa hapa nchini utakuna na Prof Shivji) .. na ndio maana hata mwenge wa uhuru uliwekwa juu ya mlima kilimanjaro ili kumulikia nchi nyingine.. Kumbuka hiyo mitizamo ya KIUZAWA Mwalimu aliita mitizamo membamba.. kwa maana ya kwamba ipo kwa ajili ya Kuiangamiza afrika

Na mwisho ningependa kukuuliza--->Je umezisikia shangwe za wazalendo na wazawa leo hapa dodoma baada ya kusikia Babu Seya na familia yake wamepewa msamaha wa rais!!? Wewe ni RASTA kaka.. kumbuka siku zote CHUKI HUMUUMIZA ANAYEIHIFADHI.. [HASHTAG]#AfrikaUnite[/HASHTAG] ✊


Nani yupo sahihi kati ya hawa mafahari wawili?
Je kuwa Mzalendo ni lazima uwe mzawa wa nchi husika?

Amemjibu vizuri sana na kiungwana
 
Mrisho mpoto ni mnafiki mchumia tumbo,

Kwahiyo anataka kuuaminisha umma yule nyoso ni mzalendo kuliko waliachwa,

Kwanza uzalendo haumasishwa uzalendo unatoka moyoni
Hii imenikumbusha alivowakilisha kenya uko nchi za watu kwenye tamasha la kiswahili japo alijitetea sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom