Intelligent businessman
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 26,126
- 52,881
Kabla hujaanza kusoma vizuri, naomba kwanza urejee kichwa cha habari hapo juu, kielewe vizuri halafu ndiyo uendelee kusoma,
Binafsi ukija kwa mbele yangu na kunitupia swali la haraka, kutaka nikutajie wasanii watano ambao nawakubali sana,
Basi jina la Mfalme wa Rhymes (Afande Sele) litakuwa miongoni mwao,
Kwanini???
Afande ni miongoni mwa Wasanii ambao nawaelewa sana nyimbo zao, enzi za kutamba kwake kwenye gemu, Afande Sele alikuwa Balozi mzuri sana wa jamii ya watanzania,
Kwa sababu Mshikaji alikuwa anaimba nyimbo zenye kugusa jamii,
Mwenyewe katika kiitikio cha wimbo wa Ndugu Zangu anasema....
Napenda ndugu zangu
toka moyoni mwangu uuhh, siwezi idharau nchi yangu,
kutenga ndugu zangu
kwa iman yangu itakua dhambi mbele za mungu
Ndugu hao ambao Afande Sele amewaongelea katika wimbo huo, ni sisi Watanzania wenzake,
Ni wimbo mzuri sana ambao mtu ukiusikiliza unapata mambo mawili kwa wakati mmoja,
Kwanza kuelimika, wimbo huo unakuelimisha vizuri sana,
Pili burudani ambayo mtu unaipata wakati wa kuisikiliza ngoma hiyo, lakini pia Afande Sele kama binadamu ana kasoro zake, na moja ya kasoro yake kubwa, ni kupenda kuwapangia wasanii wenzake nini cha kuimba,
Kivipi???
Afande Sele anapenda kuzitoa kasoro nyimbo za wenzake, kitu ambacho alikuwa anakitaka Afande Sele kutoka kwa wasanii wenzake, watunge nyimbo zenye kugusa jamii kama vile yeye anavyofanya.
Hapa ndipo Mfalme huyo wa Rhymes anapokosea, na huenda ndiyo sababu ya kuingia kwenye bifu na baadhi ya wasanii wenzake,
Halafu kama hujui Afande Sele ni bingwa na mtaalamu kweli wa kuvunja darasa ambalo analitoa yeye mwenyewe, yaani Mshikaji anatoa wimbo uliyo na ujumbe wa kukemea jambo fulani, halafu yeye mwenyewe anakuja kutoa wimbo wa kufanya kile ambacho amekikemea katika wimbo wake wa kwanza,
Kivipi???
Nitakupa mfano ili twende sawa,
Nenda kasikilize wimbo wake wa Mtazamo, katika Verse yake Afande Sele anasema,
Asante Professor Jay
Majani na Ulamaa mmegusa n’napopataka
Nami kwenye mtazamo nina jambo nataka kuweka
Maana kila kukicha emcees wanaongezeka
Nasema very nice, yes rap kama dhehebu
Emcees kama wafuasi
Wingi wa wasanii unaonesha ni dini safi
Yaani imekubalika, waumini tuko wengi
Lakini bado nashaka
Sijapata uhakika, wote tumesadiki
Ama wengine ni fake mmetumwa kama mamluki
Maanake hamna maana
Mna-rap ili mradi rap, mistari imekosa vina
Yenye vina haina maana
Na kila mnapokaa mnapenda kusengenyana
Mnapenda kutetana na mnapenda kurumbana
Mimi naogopa sana
Kwa jinsi navyoelewa mwishoni mtatukanana
Ama inawezekana mwishoni mkaja chinjana
Na wote tunao-rap tuonekane hatuna maana
Wapi ilipo Taarab
Ilikuja kwa kishindo, hata wagumu walishausudu
Kwa ajili ya marumbano mwishoni ikafa kibudu
Shabiki piga simu, changia mawazo yako
Nani tutamlaumu, kama rap ita-cease kwa kuendekeza upuuzi
Nani tumchune ngozi, producer aliyerekodi
Ama labda DJ anaepiga kwenye kipindi
Wengi wanapenda rap, ajabu rap haiwapendi
Waungwana wanaiacha, wapumbavu hawaambiliki
Hivi kwani lazima tuwe wote wanamuziki
Mi nadhani ingetosha wengine mbaki ushabiki
Huu ni wangu mtazamo masela msijenge chuki
Hata na Majani, yoh
Unaona namna Afande Sele alivyosema, mimi nashika mistari yenye kusema,
(Mnapenda kutetana na mnapenda kurumbana
Mimi naogopa sana
Kwa jinsi navyoelewa mwishoni mtatukanana
Ama inawezekana mwishoni mkaja chinjana)
Katika mistari hiyo Afande Sele anaonekana ni kwa namna gani hafurahishwi na marumbano na kutetana, yeye ana hofu vitu hivyo huenda Baadaye watu wakaja kuchinjana,
Lakini upande wa pili kwenye wimbo wa Darubini kali, ni yeye Afande Sele anayaanzisha marumbano kwa kuwadisi Bwana misosi na O Ten, katika wimbo huo Afande Sele anamwambia Bwana misosi, "kuna vitu vya kuimba vyenye maana kila kona, na siyo nyimbo nzima anataja taja majina tu, tena kwa mistari isiyo na vina" Binafsi sijaona kosa la Bwana misosi katika ule wimbo wa Nitoke vipi,
Kwanini???
Mwanzoni wa ule wimbo ndiyo utaelewa vizuri nini maana ya msemo, pale Bwana misosi aliposema,
(Misosi Nitoke vipi nafanya tafiti ya ndani
Sitaki ulimbukeni nataka kuuza duka
Na hawa ni baadhi ya waliopanda chati Nchini
Na huu ni upeo wangu tu
Nitoke namna gani
Nasema upeo wangu tu
Nitoke namna gani)
Hata kwa akili za Chekechea utabaini Bwana misosi katika ule wimbo ni swali ambalo anatuuliza Mashabiki, na ndiyo maana anatutajia wasanii ambao tumeshazisikia kazi zao, na yeye anauliza atoke vipi? Bahati nzuri nusu ya wasanii ambao amewataja katika ule wimbo, wamempa kampani kwa kuonekana katika ile video, lakini pia hakuwataja kwa ubaya, hata yeye Afande Sele ametajwa katika ule wimbo, Bwana misosi alisema,
(Afande mkuki moyoni
Morogoro ukamuingia) kwa namna ninavyojua mimi Afande ni jina la heshima ambalo mwanajeshi au askari yeyote anamwita mkubwa wake. Inalingana na neno la Kiingereza "Sir" Lakini ajabu Afande Sele hakuwa akijua hilo, na pia hakutaka hata kuelewa nini maana ya upeo wangu!!! Uzuri ni kwamba Bwana misosi alilijua hilo la kukosolewa na Afande Sele, Bwana misosi alikuja na majibu pale alipomwambia Afande Sele katika moja ya nyimbo zake wenye Kiitikio chenye kusema,
(Nikitunga nyimbo haina vina
We kaishi palipo na vina
Uganda Bongo na Kenya
Ninatoa Radha bila kubana)
Hakukuwa na marumbano ya muda mrefu kwa wasanii hawa wawili, lakini iliripotiwa kwenye vyombo vya habari, kuwa wawili hawa haziivi kabisa, na chanzo ilisemekana ni katika hizo nyimbo zao,
Na kama ilikuwa kweli maana yake nini???
Hapo hakuna jibu zaidi ya kusema, Afande Sele alivunja darasa ambalo alilitoa yeye mwenyewe katika wimbo wa mtazamo,
Nitoke vipi ya Bwana misosi haikuwa mbaya, na hata Mashabiki tuliipokea vizuri, na kupitia wimbo huo ambao ndiyo ulibeba jina la Albamu, ilipelekea Albamu hiyo kufanya vizuri sokoni, na jina la Bwana misosi likawa kubwa ndani na nje ya nchi, wote tuliona namna Bwana misosi alivyokuwa akifanya kazi na wasanii mbalimbali wa kutoka nje ya nchi, kama Uganda na Kenya,
Binafsi ukija kwa mbele yangu na kunitupia swali la haraka, kutaka nikutajie wasanii watano ambao nawakubali sana,
Basi jina la Mfalme wa Rhymes (Afande Sele) litakuwa miongoni mwao,
Kwanini???
Afande ni miongoni mwa Wasanii ambao nawaelewa sana nyimbo zao, enzi za kutamba kwake kwenye gemu, Afande Sele alikuwa Balozi mzuri sana wa jamii ya watanzania,
Kwa sababu Mshikaji alikuwa anaimba nyimbo zenye kugusa jamii,
Mwenyewe katika kiitikio cha wimbo wa Ndugu Zangu anasema....
Napenda ndugu zangu
toka moyoni mwangu uuhh, siwezi idharau nchi yangu,
kutenga ndugu zangu
kwa iman yangu itakua dhambi mbele za mungu
Ndugu hao ambao Afande Sele amewaongelea katika wimbo huo, ni sisi Watanzania wenzake,
Ni wimbo mzuri sana ambao mtu ukiusikiliza unapata mambo mawili kwa wakati mmoja,
Kwanza kuelimika, wimbo huo unakuelimisha vizuri sana,
Pili burudani ambayo mtu unaipata wakati wa kuisikiliza ngoma hiyo, lakini pia Afande Sele kama binadamu ana kasoro zake, na moja ya kasoro yake kubwa, ni kupenda kuwapangia wasanii wenzake nini cha kuimba,
Kivipi???
Afande Sele anapenda kuzitoa kasoro nyimbo za wenzake, kitu ambacho alikuwa anakitaka Afande Sele kutoka kwa wasanii wenzake, watunge nyimbo zenye kugusa jamii kama vile yeye anavyofanya.
Hapa ndipo Mfalme huyo wa Rhymes anapokosea, na huenda ndiyo sababu ya kuingia kwenye bifu na baadhi ya wasanii wenzake,
Halafu kama hujui Afande Sele ni bingwa na mtaalamu kweli wa kuvunja darasa ambalo analitoa yeye mwenyewe, yaani Mshikaji anatoa wimbo uliyo na ujumbe wa kukemea jambo fulani, halafu yeye mwenyewe anakuja kutoa wimbo wa kufanya kile ambacho amekikemea katika wimbo wake wa kwanza,
Kivipi???
Nitakupa mfano ili twende sawa,
Nenda kasikilize wimbo wake wa Mtazamo, katika Verse yake Afande Sele anasema,
Asante Professor Jay
Majani na Ulamaa mmegusa n’napopataka
Nami kwenye mtazamo nina jambo nataka kuweka
Maana kila kukicha emcees wanaongezeka
Nasema very nice, yes rap kama dhehebu
Emcees kama wafuasi
Wingi wa wasanii unaonesha ni dini safi
Yaani imekubalika, waumini tuko wengi
Lakini bado nashaka
Sijapata uhakika, wote tumesadiki
Ama wengine ni fake mmetumwa kama mamluki
Maanake hamna maana
Mna-rap ili mradi rap, mistari imekosa vina
Yenye vina haina maana
Na kila mnapokaa mnapenda kusengenyana
Mnapenda kutetana na mnapenda kurumbana
Mimi naogopa sana
Kwa jinsi navyoelewa mwishoni mtatukanana
Ama inawezekana mwishoni mkaja chinjana
Na wote tunao-rap tuonekane hatuna maana
Wapi ilipo Taarab
Ilikuja kwa kishindo, hata wagumu walishausudu
Kwa ajili ya marumbano mwishoni ikafa kibudu
Shabiki piga simu, changia mawazo yako
Nani tutamlaumu, kama rap ita-cease kwa kuendekeza upuuzi
Nani tumchune ngozi, producer aliyerekodi
Ama labda DJ anaepiga kwenye kipindi
Wengi wanapenda rap, ajabu rap haiwapendi
Waungwana wanaiacha, wapumbavu hawaambiliki
Hivi kwani lazima tuwe wote wanamuziki
Mi nadhani ingetosha wengine mbaki ushabiki
Huu ni wangu mtazamo masela msijenge chuki
Hata na Majani, yoh
Unaona namna Afande Sele alivyosema, mimi nashika mistari yenye kusema,
(Mnapenda kutetana na mnapenda kurumbana
Mimi naogopa sana
Kwa jinsi navyoelewa mwishoni mtatukanana
Ama inawezekana mwishoni mkaja chinjana)
Katika mistari hiyo Afande Sele anaonekana ni kwa namna gani hafurahishwi na marumbano na kutetana, yeye ana hofu vitu hivyo huenda Baadaye watu wakaja kuchinjana,
Lakini upande wa pili kwenye wimbo wa Darubini kali, ni yeye Afande Sele anayaanzisha marumbano kwa kuwadisi Bwana misosi na O Ten, katika wimbo huo Afande Sele anamwambia Bwana misosi, "kuna vitu vya kuimba vyenye maana kila kona, na siyo nyimbo nzima anataja taja majina tu, tena kwa mistari isiyo na vina" Binafsi sijaona kosa la Bwana misosi katika ule wimbo wa Nitoke vipi,
Kwanini???
Mwanzoni wa ule wimbo ndiyo utaelewa vizuri nini maana ya msemo, pale Bwana misosi aliposema,
(Misosi Nitoke vipi nafanya tafiti ya ndani
Sitaki ulimbukeni nataka kuuza duka
Na hawa ni baadhi ya waliopanda chati Nchini
Na huu ni upeo wangu tu
Nitoke namna gani
Nasema upeo wangu tu
Nitoke namna gani)
Hata kwa akili za Chekechea utabaini Bwana misosi katika ule wimbo ni swali ambalo anatuuliza Mashabiki, na ndiyo maana anatutajia wasanii ambao tumeshazisikia kazi zao, na yeye anauliza atoke vipi? Bahati nzuri nusu ya wasanii ambao amewataja katika ule wimbo, wamempa kampani kwa kuonekana katika ile video, lakini pia hakuwataja kwa ubaya, hata yeye Afande Sele ametajwa katika ule wimbo, Bwana misosi alisema,
(Afande mkuki moyoni
Morogoro ukamuingia) kwa namna ninavyojua mimi Afande ni jina la heshima ambalo mwanajeshi au askari yeyote anamwita mkubwa wake. Inalingana na neno la Kiingereza "Sir" Lakini ajabu Afande Sele hakuwa akijua hilo, na pia hakutaka hata kuelewa nini maana ya upeo wangu!!! Uzuri ni kwamba Bwana misosi alilijua hilo la kukosolewa na Afande Sele, Bwana misosi alikuja na majibu pale alipomwambia Afande Sele katika moja ya nyimbo zake wenye Kiitikio chenye kusema,
(Nikitunga nyimbo haina vina
We kaishi palipo na vina
Uganda Bongo na Kenya
Ninatoa Radha bila kubana)
Hakukuwa na marumbano ya muda mrefu kwa wasanii hawa wawili, lakini iliripotiwa kwenye vyombo vya habari, kuwa wawili hawa haziivi kabisa, na chanzo ilisemekana ni katika hizo nyimbo zao,
Na kama ilikuwa kweli maana yake nini???
Hapo hakuna jibu zaidi ya kusema, Afande Sele alivunja darasa ambalo alilitoa yeye mwenyewe katika wimbo wa mtazamo,
Nitoke vipi ya Bwana misosi haikuwa mbaya, na hata Mashabiki tuliipokea vizuri, na kupitia wimbo huo ambao ndiyo ulibeba jina la Albamu, ilipelekea Albamu hiyo kufanya vizuri sokoni, na jina la Bwana misosi likawa kubwa ndani na nje ya nchi, wote tuliona namna Bwana misosi alivyokuwa akifanya kazi na wasanii mbalimbali wa kutoka nje ya nchi, kama Uganda na Kenya,