Mimi nawapenda watu wa aina hii:
a. Wanaouliza maswali wasiokubali kirahisirahisi: Hili ni kunddi la watu ambao lolote litakalosemwa kuhusu jambo lolote mwitikiio wao wa kwanza ni "je ni kweli", "nani kashuhudia", "Lete picha", "ushahidi uko wapi". Yaani ni kundi la inquisitive minds. Hawa ni watu ambao wakijiridisha kiakili basi huamini moyoni. Kundi la Wanafilosia.
b. Wanaofikiri kabla ya kuanza kujibu: Kundi hili pia lina watu ambao wakisoma kitu hata kikiwagusa vipi hawakurupuki kujibu mara moja bali hutumia muda kurudia kusoma tena, na hata kama kinawagusa wanafikiria kujibu kwanza kwani wanataka wazungumza wanachomaanisha na wamaanishe wanachozungumza. Kundi hili halijibu kutoka katika hisia bali katika kufikiria. Hili mara nyingi ni kundi la watu ambao tunaweza kusema walipoingia darasani na darasa liliwaingia; siyo walioingia darasani na darasa likawapita! Kundi la Wasomi
c. Watu ambao hawakasiriki kirahisi na hawana tahamaki ya pupa. Mara nyingi watu tunaposikia vitu tunaweza kuumizwa, kushtushwa, kutishwa au hata kukasirishwa sana. Katika maisha ya kawaida unaposoma JF unaweza ukajikuta unapata hasira za ghalfa au taharuki ya aina yake. Sasa wapo watu ambao JF imewafundisha ustahimivu na uvumilivu wa aina yake. Mambo ambayo zamani yalikuwa yanawasumbua kwenye mtandaao huu wamejifunza kuyachukulia "with a light sense of humor" kiasi kwamba hawakasiriki kirahisi. Nakumbuka zamani kulikuwa na watu wakianza kupingwa humu wanakimbia na kuisusa JF na kuhuzunika na wengine hata kujisikia kulia kwani walisema walichomaanisha lakini watu "wakawaelewa vibaya". Kumbe baada ya muda wakaja kujua sisi sote humu ni ndugu moja, na tunataniana, kuchokozana na wakati mwingine kukasirishana and then kuchekeshana! Utaona watu wamejifunza uvumilivu ambao umewasaidia hata katika maisha nje ya "virtual world" tunayoishi sasa. Kundi la Wachekeshaji.
d. Watu ambao wanapenda kujenga urafiki kuliko uadui. Kuna kundi limo humu ambalo watu wake wanapenda kuwa marafiki na watu na hawana jambo lolote la kutafuta ugomvi na mtu. Hawa hawapendi kusema kitu kitakachomuudhi mtu au kufanya kitu ambacho kitasababisha mtu ajisikie kaonewa, kadhalilishwa, katukanwa au kwa namna moja au nyingine kafanywa duni. Kundi hili liko sensitive sana kwa hisia za watu wengine, ni wapole, wanajali na hawachelewi kuja na kuwa wapatanishi wakiona mambo yanaanza kukorogeka kati ya wanachama. Hili ni kundi la Wapatanishi.
Naam! Kwa namna moja au nyingine na kutegemeana na siku kwa siku sote tunajikuta wakati mmoja au mwingine tukiwa katika mojawapo ya makundi haya. Wachache huishi katika "box" la kundi mojawapo na hawatoki humo. Wachache waliwahi kuwemo kwenye box moja na wameweza kutoka katika kile kinachoitwa "kufikiri nje ya sanduku". Na wengine wako kwenye makundi yote hayo na zaidi. Ana kheri yule aliyeko mwote. Huyo is my best inspiration, my best friend, my best company and is the best of the best.
M.M.