Nani kugombea urais 2015 Tanzania kupitia CCM?

WanaJamiiForums,

Naomba niwaulize na mnijibu kiufasaha kuna kitu mpaka sasa sikielewi kuhusu nani anayefaa hasa kuwa rais wa nchi hii mwakani kwani cabinet yote ya CCM kwa sasa inaonekana kuwa na dosari na hata ukikuta asiye na dosari basi uwezo wake ni mdogo najua tunawafahamu wanaodhaniwa sasa kama wasomi ambao ndio sisi sote nani atatufaa ki ukweli.
 
wanajamii forum naomba niwaulize na mnijibu kiufasaha kuna kitu mpaka sasa sikielewi kuhusu nani anayefaa hasa kuwa rais wa nchi hii mwakani kwani cabinet yote ya ccm kwa sasa inaonekana kuwa na dosari na hata ukikuta asiye na dosari basi uwezo wake ni mdogo najua tunawafahamu wanaodhaniwa sasa kama wosomi ambao ndio sisi sote nani atatufaa ki ukweli

Aliyekudanganya Watanzania ni wajinga mpaka wairudishe tena mijizi ya Ccm ni nani?
 
Upinzani hauna taasisi imara kutoa kiongozi mweledi na CCM bado haijapendekeza chaguo lake, ni jambo la kusubiri ili tuwaweke wote kwenye mizani.
 
Jaman anayefaa mbona anajulikana? Ni.PROFESA SOSPETER MWIJARUBI MUHONGO! Ni msomi, ana akili, anajituma, kiboko ya wapiga dili, anakubalika kimataifa.
 
Kila siku nasema; Hajajitambua bado kuwa yeye ndiye anayefaa kuipeperusha bendera ya ccm. Si mwingine bali ni yule mbunge wetu kijana kabisa aliyewahi kusema yule rais mtarajiwa hatatoka Kaskazini kipindi hiki. Naye si mwingine ni Riz Kikwete tuuuuu.
Naomba nimstue ajiandae kisaikolojia kuwa baada ya kulikwaa jimbo la Chalinze, sasa asogeee kidogo aingie Magogoni kama Mpangaji wetu mpya si ka kwenda msalimia babakee
 
Rais ajae lazima atoke ccm, upinzani bado hawajajipanga kuweza kuongoza nchi.Rais ajae ni EDWARD NGOYAI LOWASSA
 
Msitanganyike Rais wa nchi hii hawezi kutoka upinzani.Upinzani bado hawana uwezo wa kuongoza nchi.
Rais ajae ni mh Edward Ngoyai Lowassa
T2015 ENL
 
Msitanganyike Rais wa nchi hii hawezi kutoka upinzani.Upinzani bado hawana uwezo wa kuongoza nchi.
Rais ajae ni mh Edward Ngoyai Lowassa
T2015 ENL

...taja jina la kiongozi mwenye uzoefu wa kuongoza nchi na sio wizara wala chama, lowasa ameongoza nchi gani na huo uzoefu kaupata wapi....
 
kama ni maana ya uzoefu wa kuongoza ndo tuzingatie ktk kuchagua kiongoz nadhani tusingekua tunapiga kura
 
Kwa nguvu anayotumia Lowassa pamoja na ushawishi na nguvu aliyonayo ndani ya CCM na nje ya CCM, itakuwaJE CCM wakimpiga chini kupeperusha bendera yao hii 2015.
Tunatambua kuwa kuna kundi kubwa tu ndani ya CCM wasiomtaka Lowassa agombee urais kwa ticket ya CCM, na hata Mh. J.K kashasema asingependa amkabidhi nchi mtu mzima wa makamo yake, anataka ampe nchi kijana under 50.
Sasa kwanza kwa nguvu hizi za Lowassa, who can stop him!? And how!? Na if ikifanikiwa kumpiga chini, nini kitafuata!? Nini mustakabali wa TeamLowassa!?
 
Back
Top Bottom