SONGOKA, umeandika hoja tano kutetea msimamo kwamba huenda, kuna mtu kamfukuza Mh Rais Dar na hivyo kukimbilia Dodoma. Hoja zako zikiwa zimehaririwa ili kuzipa muundo wa kimantiki unaoonyesha major premise, minor premise na conclusion, ni hizi hapa:
- Kama mpango wa Mh Rais na Serikali yake kuhamia Dodoma ulikuwepo tangu Mei mwaka huu, basi, katika bajeti ya 2016/2017 wangeweka fungu la kuhama. Lakini atika bajeti ya 2016/2017 hakuna fungu la serikali kuhamia Dodoma. Hivyo, huenda, kuna mtu kamfukuza Mh Rais Dar.
- Kama mpango wa Mh Rais na Serikali yake kuhamia Dodoma ulikuwepo tangu Mei mwaka huu, basi, Waziri Mkuu angetoa taarifa hii katika majumuisho yake katika bunge la bajeti ili kuwapa mawaziri taarifa rasmi na muda wa kuhama. Lakini, Waziri Mkuu hakutoa taarifa hii katika majumuisho yake katika bunge la bajeti ili kuwapa mawaziri taarifa rasmi na muda wa kuhama. Hivyo, huenda, kuna mtu kamfukuza Mh Rais Dar.
- Kama mpango wa Mh Rais na Serikali yake kuhamia Dodoma ulikuwepo tangu Mei mwaka huu, basi, CCM wasingehangaika kulazimisha kuchakachua matokeo ya umeya wa jiji la Dar. Lakini, CCM walihangaika kulazimisha kuchakachua matokeo ya umeya wa jiji la Dar kutokana na wasiwasi kwamba rais hawezi kuwa katika jiji linaloongozwa na upinzani. Hivyo, huenda, kuna mtu kamfukuza Mh Rais Dar.
- Kama mpango wa Mh Rais na Serikali yake kuhamia Dodoma ulikuwepo tangu Mei mwaka huu, basi, nina uhakika Rais asingepeleka bil 12 mahakamani kwa mkupuo wakati wizara zake zote hazina bujeti ya kuhamia Dodoma katika fedha walizotenga. Lakini, Rais amepeleka bil 12 mahakamani kwa mkupuo wakati wizara zake zote hazina bujeti ya kuhamia Dodoma katika fedha walizotenga. Hivyo, huenda, kuna mtu kamfukuza Mh Rais Dar.
- Kama mpango wa Mh Rais na Serikali yake kuhamia Dodoma ulikuwepo tangu Mei mwaka huu, basi, Rais asingejikita katika ujenzi wa flyover Dar ili kupunguza foleni wakati barabara za Dodoma anakotaka kuhamia ni nyembamba kama mti a kitendo cha kuhamia Dodoma kinaweza kupunguza foleni Dar. Lakini, Rais amejikita katika ujenzi wa flyover Dar ili kupunguza foleni wakati barabara za Dodoma anakotaka kuhamia ni nyembamba kama mti na kitendo cha kuhamia Dodoma kinaweza kupunguza foleni Dar. Hivyo, huenda, kuna mtu kamfukuza Mh Rais Dar.
- Kama mpango wa Mh Rais na Serikali yake kuhamia Dodoma ulikuwepo tangu Mei mwaka huu, basi, Rais, kwa kuzingatia uhitaji wa nyumba utakaoongezeka Dodoma kwa sababu ya kuhamia huko, asingezuia miradi mipya ya NHC kule Dodoma. Lakini, Rais, bila kuzingatia uhitaji wa nyumba utakaoongezeka Dodoma kwa sababu ya kuhamia huko, amezuia miradi mipya ya NHC kule Dodoma. Hivyo, huenda, kuna mtu kamfukuza Mh Rais Dar.
Nazikataa hoja zote tano kwa sababu mbili. Kwanza, major premises (blue text) zote zinaelea hewani. Hazina supporting evidence. Nauliza: ni kwanini unafikiri kwamba major premises (blue text) zako zinapaswa kukubalika?
Na pili, sioni kama hitimisho lako linafuata kimantiki kutoka kwenye premises. Nauliza tena: Ni kwa nini ufikirie kuwa rais kafukuzwa badala ya kufikiria sababu nyingine, kama vile kupeleka serikali karibu na wananchi ili kuharakisha monotoring and evaluation?