Nani kamfukuza Rais wetu Dar?

Nani kamfukuza Rais wetu Dar?

Naanza kuwa na wasiwasi na PM naona kila anachosema mkuu wake anakimbilia utekelezaji wa kasi ya ajabu baadaye anafeli.Mfano ni ile issue ya sukari walikurupuka vibaya mpaka sasa sukari haijashuka bei. Anapaswa kuwa mshauri sio bendera liyo na woga.Miezi miwili unahamisha serikali yote kwa bajeti gani? Nashauri Rais awe anaandikiwa hotuba na akubali kusoma ama sivyo matamko haya yatatimizwa bila kufuata utaratibu na uvunjaji wa sheria na viongozi wengi wanofanya kazi kwa woga kutetea vyeo vyao na matumbo yao.
Mmmh!! Mkuu usipate shidA! Kwani hujui chimbuko la elimu yetu kuanzia degr, master mpka PHd ni mwendo wa kukremisha mpka nucta+mbwembe kidooogo!
 
Kwa Rais asiyesafiri kama JPM, kuhamia Dodoma ni jambo zuri sana. Vipi uncle X angehamia huko na safari za Ulaya kila siku? si gharama za safari zingekuwa mara 10 zaidi!
 
Mbona hujiulizi pesa atakayolipa yule jamaa wa EFD feki zitaenda wapi? Mbona hujiulizi wawekezaji kadhaa waliokuwa wakikwepa kulipa kodi watalipa na pesa itaenda wapi?. Kuna pesa nyingi imebaki benki haina kazi, Dodoma makao makuu yanahamia.
Mkuu kwani we ni mgeni wa nchi hii au?! Pesa zikipatikana moj mw moj zinApelekwa kwenye barabara ambazo nyingi huwa hatuzioni!
Chenji hupelekwa kwenye kuongezea bajet mana nackia et bajt ni gas!
ISITOSHE MWAKA HUU HAKUNA FUNGU LILILO TENGWA KWA AJILI YA HIYO TREK! kumbuka msimamizi kadai et sept atakuwa kwa wgg!
ILA KIUKWELI HII NCHI HAINA DIRA YOYOTE ILE! KWANI HATUJUI TUENDAKO WALA TUTOKAPO! KILA MWENYE SAUTI utaka kuongea hili asikike!
Tujiulize.
1/ mara viwanda
2/ leo ndege
3/juzi walisema dom
4/ kesho sijui watasema nini?
MBAYA ZAIDI VYOTE WANAAHIDI WATAFANYA KATIKA BAJETI YA MWAKA HUU! ambayo baadhi wanadai et ni gas!
 
Wakati mwingine wana CCM ndiyo maana huwa hawawaelewi wapinzani wao. Sasa wanashangaa kwa nini wapinzani wao wanaonekana kuhoji hatua ya kuhamia Dodoma. Walitegemea wapinzani wao wasifie uamuzi huo? Uamuzi wa kuhamia Dodoma ni muda mrefu sana. Kama chama hiki na serikali zake kingekuwa makini na imara katika kutekeleza sera zake, uamuzi huu ungeshafanywa miaka zaidi ya 30 iliyopita. Ni kama uamuzi wa kila shule kuwa na madawati ya kutosha....., hili si jambo la kujivunia tena leo kwa vile nchi yetu ilitakiwa kufanya mambo haya miaka 50 iliyopita na siyo leo. Hakuna mtu anayeweza kusifia kitu kilichocheleweshwa kwa miaka 30. Kwa hiyo "milipuko ya sifa" wanayoitaka haiwezi kuwepo.
 
Back
Top Bottom