Asante sana mkuu KING KING kwa kutupa darasa. Ninaamini wengi wetu tumefaidika kwa kulielewa hilo.
Binafsi ninapata mashaka sana kuona jinsi 'makanisa' yanavyoibuka kila kukicha na watu wanaojiita watumishi wa Mungu wanavyoogelea kwenye dimbwi la utajiri wakati wanakondoo wanaowaongoza wakiendelea kuwa duni kwenye dimbwi la ufukara. Makanisa yamegezwa 'dili', sehemu ya kuchuma mali, badala ya kuwa nyumba ya Ibada na sehemu ya kuwapa waumini mwelekeo na mwongozo wa maisha bora hapa duniani na mbele ya Mungu! Wamesahau ya kwamba wao wanatakiwa wawe 'watumishi', wajishushe kama ambavyo vitabu vitakatifu vinaelekeza.
Wakumbuke ya kuwa hata Yesu Kristo alizaliwa kimaskini kwenye familia ya 'seremala' na akalelewa katika hali ya kimaskini. Hata mwishoni alipokuwa anaingia Yerusalemu, alipanda mwana punda. Wakati huo kulikuwa na warumi waliokuwa wanatumia farasi na magari ya kukokotwa na farasi! Mwenyezi Mungu hakushindwa kumleta Yesu kama tajiri!
Kama watumishi wa Mungu wanatakiwa waishi kufuata mifano hai ya Yesu Kristo, badala ya kujikweza na kutamba na utajiri wa kidunia ambao utapita. Kwangu mimi huyo Mzee wa Upako, Mama Lwakatare na wengine wanaojiita manabii na maaskofu ninawaona ni Manabii wa Uongo ambao vitabu vyote vya kidini vimetutahadharisha ya kuwa tutawaona wengi siku za mwisho.
Biblia inatuambia, 'Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako!' (Ufunuo wa Yohana 3:11)
Me sio mfuasi wamzee wa upako wala hayupo moyoni wala akilini mwangu,
ila unanishangaza sana na tafsiri yako ya Yesu juu ya umaskini ni nani aliekumbia Mungu anataka watu wake wateseke na umasikini,
umasikini unasababisha yafuatayo
kukosa ada ya kusoma
kukosa fedha za matibabu
kukosa mavazi na malazi bora
kukosa uwezo wa kumudu mlo kamili
kukosa ufanisi wa uendeshaji wa shughuli za maendeleo
kukosa sadaka zaka malimbuko na msaada kwa watu wasiojiweza. n.k
mambo haya yote ndo yanayo changia umasikini mkubwa kwa watu sasa kwa mujibu wa maelezo yako ndivyo Mungu anavyotaka iwe kwa wanadamu aliowaumba kwa sura na mfano wake?
Utajiri ni kutumia rasilimali ambazo ni asili Mungu alizoumba kwa ajili ya wanadamu ili waendelee kwa Utukufu wake,
kwa mujibu wa maelezo yako ni dhambi kuchimba madini, kufanya biashara, kufanya kazi, kulima, kufuga na kutoa huduma yoyote halali inayompa mtu kipato kinachomfanya awe tajiri kwa kuwa utajiri ni mafanikio ya hali ya juu ya upatikanaji wa faida ya kazi fulani halali,
Kwa kusema hivyo Mungu aliwafundisha Adam na Eva dhambi alipowakabidhi bustani wailime na kuitunza ambapo kwa maisha ya kileo wangeweza kuuza mazao waliyolima na kutajirika kwa mfumo wa money exchange
Hivyo unataka kusema kwamba tukienda maosipitalini na kukosa dawa, vifaa tiba, watoto wanakaa chini darasani, wamama wanajifungulia njiani, njaa, kutomudu kusoma vizuri, GDP ya taifa kuwa chini kutokana na low per capital income na matatizo mengine yote, kwamba maana yake ni umasikini [sio tajiri kumudu] ni mpango wa Mungu watu wake waishi hivyo au?
naomba jibu tu kwa namna ya kibinadamu na sio kwa kuzama kwenye NENO cause huko sijui hata utajiteteaje!