NANI KAMA MUNGU? Mzee wa upako!

NANI KAMA MUNGU? Mzee wa upako!

Status
Not open for further replies.
Na mim nimejiuliza hili swali.
simu ya mzee wa upako ni 0713 725473
Mashart yake ni kwamba unatuma msg na shida yako ndipo yeye akupigie!!! Hii ni dalili ya utapeli mwingine!!!
Huwa anachagua watu wa kuongea nao kukwepa maswali ya waandishi wa habari!!!
Pale kwake ni mtu anayependa nyama poli na huwa analetewa hapo haijulikani anayepeleka hapo lakini siku za nyuma aliwahi kutelekeza Gari lake la Kifahali Leaders Club huku akiwa amelewa!!!
Yeye haoni Shida yapo mahubiri yake ambayo anahasisha watu wa Tabora kulima Tumbako na kuwahimiza kuvuta sigara wakati taasisi za kupambana na kifua kikuu zinapinga!!!
Gazeti la Nyakati liliwahi kuandika haya Maaskofu wakashangaa sana!!!
 
naomba nieleze kwa jinsi ninavyojua kazi ya Mungu'
Kila Mtumishi wa Mungu amepewa kipawa au talent au gift yake kwa makusudi ya kuujenga mwili wa Kristo ambao ni Kanisa
Nyie wote mnaopotosha au kumkandya Mzee wa Upako mnatenda dhambi bila kujua kwa sababu ni mtumishi wa Mungu''kwangu mimi Mzee wa Upako ni mtumishi wa Mungu mwenye mapungufu na udhaifu wa kibinadamu'sina haki ya kumhukumu kwa sababu anayemtumikia ataweza kunihukumu kwa kumdharau mtumishi wake''
Ndugu zangu kuna gharama kubwa za kulipa kwa watu wanaodharau na kuhukumu watumishi wa Mungu'ondoa kabisa ulimi wako kumsema vibaya mtumishi wa Mungu wala usiruhusu moyo wako kumwazia mabaya'KATIKA JINA LA YESU AMEN
Mzee wa upako anasema Maaskofu wa Mwanza ni Washenzi na Wapumbavu Je hapo anamtumikia nani???
 
hosea 4:6

my people are destroyed from lack of
knowledge.
“Because you have rejected knowledge,
I also reject you as my priests;
because you have ignored the law of your
God,
I also will ignore your children.
 
simu ya mzee wa upako ni 0713 725473
Mashart yake ni kwamba unatuma msg na shida yako ndipo yeye akupigie!!! Hii ni dalili ya utapeli mwingine!!!
Huwa anachagua watu wa kuongea nao kukwepa maswali ya waandishi wa habari!!!
Pale kwake ni mtu anayependa nyama poli na huwa analetewa hapo haijulikani anayepeleka hapo lakini siku za nyuma aliwahi kutelekeza Gari lake la Kifahali Leaders Club huku akiwa amelewa!!!
Yeye haoni Shida yapo mahubiri yake ambayo anahasisha watu wa Tabora kulima Tumbako na kuwahimiza kuvuta sigara wakati taasisi za kupambana na kifua kikuu zinapinga!!!
Gazeti la Nyakati liliwahi kuandika haya Maaskofu wakashangaa sana!!!

aise wewe unamfahamu vzr huyu jamaa. hebu funguka zaid bas. umesema ameoa staff wa TBC, ni nan huyo?? vp khs family yake? watoto wake wanasoma wp?? marafik zake ni akina nan?? hupendelea kufanya nin tofaut na huduma yake ya kuhubiri??
 
Hii imenishangaza sana. Yanakuja maneno yanauliza "nani kama Mungu?" Then jibu linakuja,Mzee wa Upako! Mi sijaelewa hapo wadau! Huyu Katapila,Transformer Antony Lusekelo ni kama Mungu? Na anachohubiri hasa hasa ni watu kuwa matajiri,kuongeza mapato n.k! Wanaomfaham jamani,asije akawa anapotosha watu! Ila kama ni nguvu za Mungu au mungu mmh! Tusaidiane!Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
Mliishaambiwa mtawatambua kwa matendo yao!
 
aise wewe unamfahamu vzr huyu jamaa. hebu funguka zaid bas. umesema ameoa staff wa TBC, ni nan huyo?? vp khs family yake? watoto wake wanasoma wp?? marafik zake ni akina nan?? hupendelea kufanya nin tofaut na huduma yake ya kuhubiri??
Kuhusu Marafiki zake angalia gazeti la leo tarehe 28/7/2013 la Nyakati utawaona marafiki zake!!!!!
Hapo ndipo utakaopo ona hatari iliyopo!!!
 
Akinya kuku kanya
Akinya bata kaharisha, haloo halooooooo
halo ya Lusekelo
 
Hii imenishangaza sana. Yanakuja maneno yanauliza "nani kama Mungu?" Then jibu linakuja,Mzee wa Upako! Mi sijaelewa hapo wadau! Huyu Katapila,Transformer Antony Lusekelo ni kama Mungu? Na anachohubiri hasa hasa ni watu kuwa matajiri,kuongeza mapato n.k! Wanaomfaham jamani,asije akawa anapotosha watu! Ila kama ni nguvu za Mungu au mungu mmh! Tusaidiane!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums


Jesus is God, in contrast, Allah is Anti-God.
 
View attachment 104549
Mzee wa Upako akiwa na Rafiki yake (JK) Ikulu Dar Tarehe 22 July 2013
Picha hiyo imepigwa baada ya Kufuturu Pamoja!!!
Nakumbuka Mwaka 2010 Maaskofu Mbeya waligome Futari angalia hapa!!!


Maaskofu wamgomea Kikwete.



*Wadai Mwaliko huo ni rushwa ya wazi wazi.

*Afananishwa sawa na wagombea wengine.
*Wahoji nafasi ya Rais wakati kipindi kimekwisha .

MAASKOFU wa makanisa ya kikristo na wachungaji mkoa wa Mbeya walioalikwa kwa ajili ya kula futari(kufuturu) na Rais Jakaya Kikwete Ikulu ndogo jijini Mbeya wengi wamegomea wito huo kwa madai kuwa hawawezi kushiriki na rais hasa ikizingatiwa kuwa hiki ni kipindi cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.

Kuwa kushiriki kwao kwenye futari hiyo waliyotakiwa wawe wamefika Ikulu ndogo majira ya saa 12 jioni na kushiriki na rais kisingekuwa kitendo cha wao kuaminiwa na waumini wao wakimlinganisha Kikwete sawa na wagombea wengine wa urais wanaostahili kupatiwa haki sawa bila upendeleo.

Habari za ndani ambazo Tanzania Daima imezipata zinadai kuwa maaskofu na wachungaji wa dini mbalimbali wapatao 40 walioalikwa kula futari juzi jioni na Rais Kikwete katika Ikulu ndogo ya Mbeya kwa kauli moja waliweza kususia mwaliko huo na kutoa sababu za kutokushiriki.

Mbali ya waalikwa wengi kushindwa kufika Ikulu, habari za uhakika zimeuelezea mwaliko huo kuwa haukuwa na manufaa yoyote kwa viongozi wa kikiristo ambao hawakufunga na wasingeweza kushiriki futari inayopaswa kuliwa na ndugu zao waislamu waliofunga.

Kikubwa zaidi kilichojitokeza kwenye mwaliko huo ni madai yaliyotolewa na baadhi ya viongozi wa kikiristo ambao walionyesha mashaka makubwa ya mwaliko huo wa Ikulu hasa wakizingatia kuwa nafasi iliyotumiwa na Ikulu ya kuwaalika haikuwa sahihi kwa kuwa kushiriki kwao kungeweza kutafsiriwa vibaya.

Mmoja wa Maaskofu aliyepata nafasi ya kuzungumza na Tanzania Daima alisema kuwa wameugomea mwaliko huo na kuuona kuwa ni rushwa na hawakupaswa kualikwa kipindi hiki ambacho jamii nzima ya watanzania inawatazama viongozi wa wote wa dini na kutaka kujua wameegemea upande upi.

Askofu huyo ambaye aliomba jina lake lisitajwe kwa kuwa sio msemaji wa umoja wao,alisema kuwa ni vyema viongozi wa madhehebu ya dini wakajipima na kuwa makini hasa kipindi hiki cha kampeni kwa kuwa ni rahisi wengine kuweza kununuliwa kutokana na fedha nyingi zinazomwagwa kipindi cha uchaguzi.

Hata hivyo Tanzania Daima ilifanikiwa kupata nakala ya kadi za mwaliko zilizosambazwa kwa viongozi hao wa dini ikisomeka hivi "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete anayo furaha kumkaribisha/kuwakaribisha, Mhe,Bwana na Bibi/Bi….. katika tafrija Rasmi ya FUTARI itakayofanyika MBEYA saa 12;jioni… usiku ikitakiwa jibu lifikishwe kwa mpambe wa rais Ikulu" ilisomeka hivyo na kuwataka waalikwa wote kuwa nadhifu.

Kufuatia wito huo ilibainika kuwa baadhi ya maaskofu kwa pamoja waliandika ujumbe wa kulaani kitendo hicho kwa madai kuwa kinaonyesha rushwa ya wazi wazi hasa ikizingatia kuwa hawajafunga hivyo ni kwa nini wale futari ya watu waliofunga na kutoa wito kwa watanzania wote,maaskofu na wachungaji wasikubali mialiko ya aina hiyo ni dhambi.

Askofu wa Kanisa la Pentekoste Evangelisti,Zebadia Mwanyerere Mwakatage alipohojiwa alisema kuwa hakupata mwaliko huo na hata kama angepata asingeweza kwenda kwa kuwa kitendo cha kualikwa na rais akiwa mgombea hakikustahili na asingeweza kwenda labda kama angealikwa na Shehe lakini sio mgombea huyo wa urais.

Mwakatage alisema kuwa ni makosa viongozi wa dini kushiriki kwenye mialiko ya wagombea na kwa kuwa rais anatumia kofia yake wakati ni mgombea sawa na wengine kungewapa shida na anashukuru hakuweza kualikwa kwani mara nyingi hata viongozi wa serikali wanapoalikwa na viongozi wa dini huwa hawaendi.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wakristo mkoa wa Mbeya,Askofu John Mwela wa Kanisa la Anglican Dayosisi ya nyanda za juu kusini alisema kuwa anaungana na msimamo wa maaskofu wenzake na wachungaji waliokataa kwenda kwenye mwaliko huo kwa kuwa kwa kufanya hivyo wangekuwa wanapingana na msimamo walionao wa kuto kumpendelea mgombea yoyote.

"Nchi hii hivi sasa haina rais isipokuwa tunatafuta rais,hivi sasa Kikwete ni mgombea urais kutoka CCM anagombea urais sawa na wengine tukisema twende Ikulu tumealikwa na Rais ni makosa,sijui haya mambo yamekaaje,najua futari ni kwa wale waliofunga sasa sisi wakristo tunakwenda kula futari kivipi ?" alihoji Askofu Mwela.

Askofu Mwela alisema kuwa amepatiwa kadi ya mwaliko iliyochelewa kumfikia na hata kama angeipata mapema asingeweza kwenda kwa kuwa hajafunga na hata hivyo kwao kama viongozi wa dini ingewapa shida machoni mwa waumini wao kwa kuwa hawatakiwi kuegemea upande wowote wa wagombea.

"Naunga mkono maamuzi ya wenzangu waliokataa kwenda Ikulu,kama waliliona hilo ni vyema tukawa na msimamo,tatizo huyu ni mgombea sawa na wengine na isitoshe ingekuwa tumealikwa kwenye dhifa hapo tungeenda kula chakula sio kufuturu hatukufunga sasa ningeenda kufanya nini huko" alisisitiza Askofu Mwela.

Kiongozi huyo wa madhehebu ya kikiristo mkoa wa Mbeya aliwataka waumini wa madhehebu hayo kuwa makini kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mkuu na kuwahimiza kuhudhuria kwenye mikutano ya vyama vyote ili kuweza kuwasikiliza,Madiwani,Wabunge na Wagombea wa Urais kwa lengo la kuweza kuchagua viongozi bora siku ya kupiga kura itakapofika.

Askofu wa Kanisa Katoliki,Evaristo Chengula alipotafutwa kutoa maoni yake kuhusu mwaliko huo wa Ikulu ilidaiwa kuwa amesafiri nje ya mkoa huo sambamba na maaskofu wengine Alinikisa Cheyo wa kanisa la Moraviani na Thomas Daminius Kongoro wa Pentekoste Assembless Of God(PAG) wote hawakuweza kupatikana kutoa maoni yao au kuthibitisha kama walikuwa miongoni mwa waalikwa.

Umoja wa makanisa ya kikiristo unaunganisha madhehemu manne ya Jumuiya ya Kikiristo Tanzania(CCT)Makanisa ya Kikatoliki(TEC),Jumuiya ya Kipentekoste(PCT) na makanisa huru ambayo,Mwenyekiti wake mkoani Mbeya ni Askofu Mwela wa Anglikani.

Mwisho.
 
Asante mkuu KING KING kwa maelezo yako. Huwa nasikitika sana hasa watu wanapopotea na kujikuta wanatoa pesa zao kwa hizi injili za toa ubarikiwe na kupanda mbegu. Ukisoma agano jipya hakuna sehemu hata moja ambayo Yesu amesisitiza utoaji wa pesa au kumjaribu Mungu kwa pesa. Na hata ukifuatilia mitume hawakufundisha mafundisho ya aina hii sijui tunaelekea wapi tu.
 
Last edited by a moderator:
Tuyachunguzeni maandiko ndugu zangu. Mtawatambua kwa matendo yao......siku za mwisho watajitokeza manabii wa uongo...yu mkini hata wateule watadanganywa
 
Jesus is God, in contrast, Allah is Anti-God.

Ucpende kudandia v2 kwa mbele, kama unataka kujadili maswala hayo weka post yako na c kuleta chuki zako za kdn hata sehem ambayo haihuck.., kama kweli unaamin Yesu n Mungu na Allah co Mungu weka post yako then 2bishane kwa hoja co kujfcha kwenye Migongo ya post za wanaume au na ww Mliberali?
 
Tatizo mkishasikia fulani yuko hivi basi na kila kitu chake kibaya. Leo hii twiga angeuchukia mti alao majani kisa una miba angeishi? Msikilizeni Lusekelo maana kuna mengi ya kujifunza pia japo mnasema ni tapeli
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom