Juzi nilikuwa nasikiliza huu mwimbo mpya wa lady jd and Mr.Blue, nilishawahi kupenda!! Nyimbo hii ilinigusa sana and nikajiuliza kama kuna binadamu hapa tanzania/duniani above the age of 25 hajawahi kuumizwa na mpenzi/wapenzi wake!! Naamini hakuna mtu ambaye hajawahi kutendwa katika love!! Na kila mtu ana hadithi yake jinsi alivyoteswa/tendwa. Mimi mpenzi wangu alinikimbia/alinitenda nikiwa chuo mwaka wa kwanza mwaka 2008, nilipotafuta kisa nikagundua kuwa alitongozwa na jamaa ambaye alikuwa ameshamaliza chuo and alikuwa amepata kazi benki, so msichana kwa tamaa ya fedha akakubali akanitosa mwanafunzi, mbaya zaidi mimi ndio niliwakutanisha na kuwatambulisha!!ILINIUMA SANA HIYO ISHU!! Bahati nzuri/sijui kama ni bahati nzuri jamaa alimtosa! Now nipo chuo mwaka wa mwisho, next month namaliza yule msichana ananitafuta saaaanaa!! Anajua karibu nakula shavu! HIVI KUNA MTU ABOVE AGE 25 HAJAWAHI KUUMIZWA????/ WHAT IS YOUR STORY???