Wewe unadhani kila anayehoji kuhusu Mungu ni "Edward" Hawkins??? 🤣(Stephen Hawkins).
Naanzia hapa, sio "Edward" ni "Richard Hawkins". Hakuna mtu mwenye akili salama anae weza kuhoji au kuuliza ya kuwa "Mola ameumbwa na nani",nasema hivi sababu kila kiumbe kimeumbwa kumjua Mola muumbwa hii inaitwa "Fitrah(Innate Disposition) ".
Mambo ya Stephen Hawkins hayo yako na yeye, sisi tunamjua "Stephen Hawking".
Na ukome kuleta post bila kwanza kuzisoma kwa kina.
Nakuja na hii, post ipo wazi sana, ndio maana mpama muda huu umeshindwa kukosoa nilichokiandika zaidi ya kulalamika na hili huliwezi mpaka unakufa.
Ndiyo maana nasema wewe uli copy- paste BLINDLY post usiyoijua vizuri ndiyo maana huwezi kuitetea hapa, mlete Muhusika wa hiyo post hapa wewe huwezi kuijibu kwakuwa siyo post yako.
Hitimisho lako imeonyesha wazi ya kuwa nilichokiandika nakijua ndio maana ukaamua kuandika ya kuwa sio kila mtu ni "Edward" (Japo umekosea kuandika jina la mkusudiwa).
Pili, hapa ubaonyesha ya kuwa ulivamia mada bila kuielewa ila sasa umeielewa, ndio maana huwezi kukosoa nilichokiandika kabla na baada.
Najua kutoa tarjama (tafsiri) kwako itakuwa ngumu, basi nakusamehe, wewe sasa jibu hayo maswali matatu tu.
Mpaka najiuliza, kwanini hujibu maswali yangu, naishia kucheka sana.
Ajabu wewe unaejua unashindwa kuelezea, na mimi naweza kukukosoa, sababu maana uliyoitoa inakuumbua wewe na inaonyesha ya kuwa "Sophist" ni mtu wa ghishi na mpindishaji maana ndio maana mfano ulioweka pale katika maana uliyo itoa ni kumuhusu "Mwanasiasa".
Maswali yako matatu nimeshayajibu huko nyuma zaidi ya mara moja,ni wewe tu utulize akili usome uelewe.
Japo kuna matatizo kuhusu maana ya Sophist, kuna maana ya asili na maana isiyo ya asili (loose meaning) wewe umechukua loose meaning, kwa ajili ya mjadala nikakubali tu hizo maana ulizotoa ili nije nikupige hapo baadaye, na hakika nimekupiga barabara kwani inakuaje eti Mtu "YEYOTE" aulize; je Mungu kaumbwa na nani??-- mtu huyo awe; muongo muongo, tapeli, hana elimu nk???!!, je unajuaje kwamba kila aulizaye hilo swali anakuwa na sifa hizo???, je wewe unaweza kuingia ndani ya moyo wa mtu na kusoma fikra zake???--- hayo ni baadhi ya maswali ya kujibu, hapo hutoki licha ya kujibaraguza kwako huku na huko.
Kijana mpaka unakufa maana nilizo zitoa na hii uliyoiweka wewe hivi punde kabla ile ya kwanza ambayo hukuweka marejeo hazina tofauti na huwezi kutoa utofauti wa maana hizo.
Sasa unaposemamimi nimechagua maana nyingine, nikikuuliza kwanini wewe hujachukua maana nilizo zitoa mimi ukachukua maana hiyo nyingine ? Japo hazina tofauti katika msingi wa maana ya maneno hayo. Sasa usiwe mjinga mpaka unakuwa kipofu wa moyo na akili, hufikirii.
Ahsante.