Nanenane Exhibition: Popote ulipo tupeane updates hapa

Clark boots

JF-Expert Member
Jun 5, 2017
6,402
5,526
Haya wakulima wenzangu wale, wafanya biashara pia na makampuni mbalimbali katika kuelekea kilele cha siku ya wakulima almaarufu nanenane naomba tutumie uzi huu kupeana updates. Ni kwa namna gani mambo yanazidi kunoga huko viwanjani.

*kanda ya Nyanda za juu kusini - Mbeya
*Kanda ya kusini - Lindi ngongo
*Kanda ya Magharibi
*Kanda ya kaskazini
*Na kanda zote kwa ujumla.

Binafsi nipo Morogoro mji hapa naona mambo yanazidi kunoga jamani mabanda kama yote, makampuni mbalimbali yapo hapa karibuni sana tuje kujifunza mambo mbalimbali kuhusu sekta hii nyeti ya kilimo.

Morogoro standup.

====
SIKUKUU YA KITAIFA YA WAKULIMA/ SIKUKUU YA NANENANE

Nane Nane ni sikukuu ya wakulima nchini Tanzania, inayoadhimisha tarehe 8 mwezi wa 8 kila mwaka ambayo huwapa fursa wakulima, taasisi na wadau mbalimbali wa kilimo kote nchini kuonesha bidhaa zao na mafanikio yao katika mwaka husika

Miaka iliyopita sherehe hizi zilikuwa zikifanywa tarehe saba Julai kila mwaka. Sherehe hii inatayarishwa na kuratibiwa na Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika kwa kushirikiana na Shirika la Chama cha Kilimo Tanzania ‘TASO’ na kuhusisha Taasisi, Wizara na mtu mmoja mmoja wanaoshughulika na kilimo

Nanenane iliadhimishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1977 ili kuongezea nguvu sera ya Serikali ya wakati huo ya ‘ Siasa ni Kilimo ‘, ambapo wakulima katika wilaya, mkoa na kitaifa walionesha mazao yao ya kilimo, pembejeo pamoja na kufundishwa namna ya kutumia pembejeo

Maadhimisho haya husherehekewa katika ngazi ya kanda ambapo kanda ya nyanda za juu za kusini zinafanyika viwanja vya John Mwakangale mjini Mbeya. Kwa kanda ya Kaskazini, sherehe zinafanyika viwanja vya Themi, Arusha, wakati kanda ya Mashariki zinafanyika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Morogoro na Kanda ya Ziwa, zinafanyika Mwanza, Viwanja vya Nyamhongolo na Kanda ya mwisho ni kusini, zinafanyika Ngongo
 
Nilipo mimi yamekua ni maonyesho ya bia+Nyama choma,yaani tukipigiana simu ni straight kwny banda la bia mambo ya kuzurura kwny mabanda ya watu mwishowe ujikwae uumie aisee.
 
Wiki nzima hii nimekosa nafasi japo kilele nileo ila minatarajia kwenda kesho ambayo ndio ninanafasi ..sasa cjui bado nitakuta mabanda yapo wazi au nitakuta mabanda mengi washafunga nakuondoka
 
Nilipo mimi yamekua ni maonyesho ya bia+Nyama choma,yaani tukipigiana simu ni straight kwny banda la bia mambo ya kuzurura kwny mabanda ya watu mwishowe ujikwae uumie aisee.
Hahahaaa, huku Moro mambo kama yote bado tupo hadi kesho karibu sana
 
Wiki nzima hii nimekosa nafasi japo kilele nileo ila minatarajia kwenda kesho ambayo ndio ninanafasi ..sasa cjui bado nitakuta mabanda yapo wazi au nitakuta mabanda mengi washafunga nakuondoka
Inamalizika Jumatatu.. Hvyo Leo tembelea kanda yoyote ya maonesha utakuta mambo yanaendelea.
Kama uko Moro bado mambo yanaendelea
 
Inamalizika Jumatatu.. Hvyo Leo tembelea kanda yoyote ya maonesha utakuta mambo yanaendelea.
Kama uko Moro bado mambo yanaendelea
Yah nimekuja nanenane Mbeya maonesho bado yanaendelea japo watu wengi wapo ktk harakati zakufunga funga,
namabanda mengine tayari yameshafungwa
 
Hakuna maonyesho yaliyokuwa mabovu kama ya Moro. Nilikutana kupoteza nauli yangu.
 
Ukitoa benk, na makampuni ya matrekta pamoja na JKT, Kulikua na nini kingine?
Taasisi mbalimbali za kilimo ambazo mkulima kama mimi hvyo ndo vitu vyangu vya msingi.
Apart from that even businesses kibao zilikuwepo sasa sijui we ukitaka uone biashara za uchawi ndo ungeona kupo poa..!!ety
 
Je unahitaji kulima mahindi na hauna muda wa kusimamia? Au unataka upate mavuno mengi zaidi? Njoo ofisini kwetu.

Ofisi ya YAD yenye wataalamu wabobezi wa kilimo sasa inakuletea mpango wa kusimamia shughuli zote za shambani. Mkulima utatukabidhi shughuli zako pale shambani kwako sisi tutafanya kila kitu kwa utaalamu zaidi na kukukabidhi mazao yako yakiwa yamekomaa. Gharama zetu ni nafuu sana na tunakuhakikishia kwa ekari moja kuvuna mahindi zaidi ya gunia 30. Usihangaike sasa, sisi tupo kwa ajili yako, Kwa Wale ambao hawana mashamba tutakuwezesha kupata mashamba ya kukodi kwa elfu 40 tu na mashamba ya kununua kwa elfu 60 tu hata ukihitaji ekari 100 za kununua utazipata kwa bei hiyo hiyo.

Kwa maelezo zaidi fika ofisini kwetu.
Jengo la NSSF SONGEA
Ghorofa ya 3 chumba no. 317
Simu. 0621133117
 
Back
Top Bottom