Namwambia Mungu

Namwambia Mungu

Aah aah maisha magumu ktk nyanja nyingi sana.

Me kakipato ninako kidogo but kila nikianzisha relationship natendwa na hawa viumbe. Sasa sina hata ka demu yani,natia hurumaaa.Uwezo wa kukahudumia ninao but sipatu ili nituliee aaaargh
 
Hata baba anaweza akanunua kila kitu akawwka ndani na Bado watoto wakafa njaa wasipoamua kupika ama kikapikwa wasile.
Ndivo ilivo kwa Mungu anaona yote lakini anataka utayari wetu was kuyapata, pia kufuata utaratibu alioweka.

Ndo awali nilisema Mimi ni dhaifu kwasababu najua yawezekana kuna mahali nilikosea ndo Mana napitia haya.
Kwakua yeye ni mwenye huruma amuitaye humuutikia
Jitume mkuu... Huyo unayemdhania atakupotezea muda
Usikufuru ndugu yangu
Kukufuru ni kufanyaje?
 
Aah aah maisha magumu ktk nyanja nyingi sana.

Me kakipato ninako kidogo but kila nikianzisha relationship natendwa na hawa viumbe. Sasa sina hata ka demu yani,natia hurumaaa.Uwezo wa kukahudumia ninao but sipatu ili nituliee aaaargh
Nalo ni tatiZo bro Seema Nini pingine Mungu anakuepusha na kitu vuta subira ndoa ni uzima au mauti
 
Kukufuru ni kukana uwepo na uwezo Mungu. Kumbuka kila kitu kina chanzo vitu havikutokea tuu
Ukisema kukana maanae yake namjua alafu namkana! Mimi simjui na wala maelezo yanayomuelezea hayapatani na akili

Pia unaposema kila kitu kina chanzo chake itabidi yeye pia awe na chanzo chake.... Haiwezekani yeye mwerevu kuliko sisi asiwe na chanzo
 
Soma vitabu vinavyo mhusu utamjua
Ukisema kukana maanae yake namjua alafu namkana! Mimi simjui na wala maelezo yanayomuelezea hayapatani na akili

Pia unaposema kila kitu kina chanzo chake itabidi yeye pia awe na chanzo chake.... Haiwezekani yeye mwerevu kuliko sisi asiwe na chanzo
 
Pole.sana mkuu, Mapito tumeumbiwa binadamu ndugu, lakini kumbuka unapopita Kote huku hauko pekeyako.
Lakini swala la ku divorce kuna mtu alikushauri kwamba kama bado unahisi unampenda mkeo na hauko tayari kubeba maumivu basi usimuache
 
Kwako Mungu baba mlezi wa dunia na Mbingu.

Am broke Guy, dhaifu na mdhambi!

Najua mengi mazuri umenitendea zaidi hata Sasa unanifanyia mengi mazuri nashkuru kwa yoote.

Dua na Sala ni udhihirisho wa imani kwa matendo. Nami sitosita kuendelea kutimiza kwakua najua wewe ni msikivu na mwaminifu.

Mungu mlezi wangu hii ndio status/ hali yangu kwa Sasa

1. Spiritual - down
2. Financial - broke
3. Relationship - broke
4. Ideas - broke.

Najihisi kupoteza imani kwa Yale nayapitia nakose nguvu hata za kupiga magoti kusujudu kukulilia kutokana na mfululizo wa matukio magumu uliyoruhusu niyapitie. Niokoe kwa Hilo Mungu baba mlezi wangu.

Nilipoteza kazi, ukanipa biashara nayo ikafa Sasa Sina la kufanya na majukumu yamenielemea hata watoto ulionipa nashindwa kuwatunza.

Ukanipa Ndoa Nikaipenda ndoa yangu nayo ukaruhusu isambaratike japo nilikuomba ndoa yangu idumu kwakua sikutaka wanangu wakue na single parent Kama niliyoyapitia Mimi. Nimebaki mwenyewe na watoto tunamsubiria Mama yao atarudi lini. Ingilia Kati Baba

Ulinibariki nikawa mtu smart mwenye mawaZo very constructive and attractive, now days siko hivo Tena kwa Sababu Nina experience failure nyingi kuliko mafanikio kwakipindi kirefu Sasa. Naogopa hata kufanya maamuzi japo maisha ni maamuzi.

Najua maombi ni Siri, lakini nayaandika haapa ili kesho iwe ushuhuda kwamba nalikuita ukaniitikia, ukanifuta machozi na kuniinua Tena.
Katikati ya Giza Nene hili Bado Kuna sauti ndogo inaniambia Mimi ni mshindi, nami nimeamua kuisikiliza kwa makini nakuishikilia.

Ombi hili Baba Mungu liwaguse wote wanaopitia changamoto katika maisha yao!
Amin
Amen
 
Pole.sana mkuu, Mapito tumeumbiwa binadamu ndugu, lakini kumbuka unapopita Kote huku hauko pekeyako.
Lakini swala la ku divorce kuna mtu alikushauri kwamba kama bado unahisi unampenda mkeo na hauko tayari kubeba maumivu basi usimuache
Mwenyewe haeleweki binafsi nimeshamwambie aje hataki nataka nadhani ni Hali yangu ya uchumi
 
Ulimuona wapi au moyo wako na hisia zinakutuma?

Moyo na hisia zako ni whims na matamanio,sio reality!

Rationality ni mwanadamu kuishi constantly solving reality,reality ni vitu provable,kama sio provable ni just a dream,fikiriko tu!

Vitu vya kufikirika ili ujisikie raha ni kujidanganya tu,unakwepa reality!
Kuna mambo binadamu walikwama nikamuita akafanya so he is really
 
Pole mkuu ,pia tunashukuru Kwa kumkumbusha Mungu atukumbuke tunaopitia magumu.Aisee maisha yako upsidedown sometimes unaweza kufuru.unajitahidi kutenda mema na kusaidia Sana watu at the end majanga mfululizo yanakupiga ,unamlilia Mungu why me.But hakuna namna nikumtegemea na kupigana ,Mana hakuna wa kubadili matokeo Kama sie yeye na sisi.
 
Back
Top Bottom