Namtafutia baba yangu mke

Namtafutia baba yangu mke

hapana, hiyo ni kazi ya baba, kama asipopendezwa nae, mwacheni apate wa kupendezwa nae! mbona atawapata tu, naelewa kwamba unam miss mama but kwa hili hapana, unaweza kupata mama pasua kichwa ikawa tabu kabisaa, mzee atoke hapo grocery za jirani japo anywe fanta kitaeleweka tu!
akiwa pasua kichwa si tutamtimua bwana! wewe niforwadie tu hao macandidate
 
Ila hiyo kazi ngumu sana, mnaweza kumleta huyo mama mkajuta kwanini mlifanya hivyo. Wengine co wazuri na wanavuruga familia esp. akijua kuna na kaurithi kadogo.....

na atakaejua kuna ka urithi lazima ategeshe mimba japo kwa nguvu!
 
si unaona ninapokuambia hii kazi muachieni mzee mwenyewe, tena mkimfanya ajione kama mpweke sana anaweza kuwachezea shere kabisa, mie mzee wangu huyo ana miaka 68 nasikia alioa dogo dogo wa 31yrs, ndio alimaliza pesa zote na kamuachia katoto ambako ni kama katukuu pesa zilivyoisha mdada kaolewa na wa rika lake, Smile, tulia!
ooohhh duh kwani nyamayao huna mama dear?
ila na huyo mdada alikuwa mdogo sana bwana loh
 
Mpwa wangu Smile sidhani kama kuna upendo mkubwa zaidi ya huo, yaani umtafutie mzazi wako kiburudisho!!! Ila nimechanganyikiwa na huo mstari wa Bible kwenye signature yako, hutaki yeye amtumikie Bwana??? Just curiosity
 
Last edited by a moderator:
hapo ndio mtammaliza mzee sasa, umtimue wakati yeye ndio kafa/kaoza?
baba yetu mkubwa alifiwa na mke akaoa tena alikuwa na watoto 5 huyu mke mdogo akapiga tena 5 mzee! hapana chezeiya hakuna rangi mzee aliacha kuona
 
Mpwa wangu Smile sidhani kama kuna upendo mkubwa zaidi ya huo, yaani umtafutie mzazi wako kiburudisho!!! Ila nimechanganyikiwa na huo mstari wa Bible kwenye signature yako, hutaki yeye amtumikie Bwana??? Just curiosity
ndo hivo jombaa kwa nini mzee ateseke bwana! yeye hawezi kumtumikia bwana ni mzee sasa
 
Back
Top Bottom