bolivia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2021
- 3,156
- 5,327
Umuwezi yule TAIKON WA FASIHI YUKO DEEP SNA ROBERT HERIEL
Rejea Uzi wa Robert Heriel na Jocasta, maelezo uliyotoa hayana uhusiano na mjadala uliopo mezani.Where is politics? Assuming by science you mean natural science.
Hata hiyo high IQ na BOT,,,, japo simkubali sana mwenda zake alitufumbua kuwa si wote walioko huko wana huo uwezo wa kuwa intelligent,,,wengi ni udugu tu,,,, connection (politics).
SIASA yetu inazalisha UMASIKINI mkubwa wa MWILI na AKILI, matokeo yake tunakuwa MASIKINI na kuanza kulaumiana kwa kushindwa kutofautisha UMASIKINI na MASIKINI.
Tusaidiane kutafuta suluhisho la tatizo - UMASIKINI, wala tusijione kuwa wenye uwezo mkubwa wa kufikiria kwa hivyo vijisenti tunavyomiliki.
Umuwezi yule TAIKON WA FASIHI YUKO DEEP SNA ROBERT HERIEL
Kwenye suala la masikin wa Dar n tofauti na masikin wa Tarime hapo umedanganya mkuu, masikini n masikin tu masikini wa London ni sawa sawa na masikini wa Gongolamboto
Mimi nilikujibu wewe sikuujibu Uzi wa Robert Heriel na Jocasta, hasa uliposemaRejea Uzi wa Robert Heriel na Jocasta, maelezo uliyotoa hayana uhusiano na mjadala uliopo mezani.
Hii theory gan Dada inasema hivi?. Sabab umaskini ni tatizo la jamii ambalo tunahitaji nadharia zinazoweza kuyaelezea matatizo ya Jamii. Umasikin sio tatizo la mtu, maelezo yako yanalitoa tatizo la jamii kwenye levo ya Jamii na kulifanya kuwa tatizo la MTU BINAFSI. Kwa msimamo huo, mjadala huu hauna maana.Scientifically Kila mtu anapata riziki kulingana na thinking capacity yake Mwenye uwezo mdogo wa kufikiri ataangukia vibarua vya kwenye mkonge wakati mwingine aliekaa darasani due to his high intelligence anaangukia BOT.
God, science and religion depend on one another to finalize findings.
Kuna mahali unapwaya, nakusoma kwa uzuri😀😀😀
Leo watu hawajui masikini ni Nani? Na hawajui maana ya Masikini.
Lakini wakiwekewa Tozo wanasema wao ni Masikini 😂😂
Rejea Uzi wa Robert Heriel UMASKINI ninaouzingumzia ni personal level yaani BINAFSI .Hii theory gan Dada inasema hivi?. Sabab umaskini ni tatizo la jamii ambalo tunahitaji nadharia zinazoweza kuyaelezea matatizo ya Jamii. Umasikin sio tatizo la mtu, maelezo yako yanalitoa tatizo la jamii kwenye levo ya Jamii na kulifanya kuwa tatizo la MTU BINAFSI. Kwa msimamo huo, mjadala huu hauna maana.
Nadharia zangu hapa znaruhusu kukubAli maelezo yako kwani Zinanipa sabab ya kukubali kwamba 'wahanga pia huwa wanalaumiwa' na tatizo la jamii litageuzwa kuwa la mtu binafsi. Wakosao ajira wataambiwa hawko kompitent, wazembe au hawatafuti kazi then wajiajiri. Masikini wataambiwa wa some, waache Ujinga, wale vizuri ili akili ziongezeke. (Mfumo umewatenga).
Bhas mada ibadilike, umasikin sio tatizo la mtu binafsi ROBERT HERIELRejea Uzi wa Robert Heriel UMASKINI ninaouzingumzia ni personal level yaani BINAFSI .
Hakuna mambo ya siasa ndani ya huu Uzi hapa mjadala ni Hali Cha kuwa maskini.
Hakuna anayepinga umasikini mbaya wala anayesoma mzuri bali kuhusu laana hapo na kutosaidiwa na kuacha wafe hapo ndipo kwenye upinzani.Watu wanaleta maneno maneno!
Umasikini ni mbaya Sana. Ninauchukia mno.
Ukiujua au kuuguliwa huko Hospitalini unahangaika na mgonjwa hapohapo unahangaishwa na mawazo.
Unawaza chakula cha watoto, kumvalisha na kumtunza mke, unawaza wazazi, unaweza Kodi ya nyumba, yaani!
Inashangaza watu wanajifanya hawajui maana ya Masikini ilhali kila siku wanailaumu serikali Kwa kutoza Kodi masikini 😀😀
Unaposema Tanzania nchi masikini maana yake nchi iliyolaaniwa..aisee kuchomoka itakuwa issue bongo.Mkuu Kwanza Nashukuru Kwa kunipinga na kutoa Mtazamo wako dhidi ya mtazamo wangu.
Turudi kwenye Mjadala.
Topic ya Poverty ipo Kidato cha tatu Kwa waliofika elimu ya Upili.
Maana ya umasikini inafahamika Kwa waliofika madarasa hayo.
Individual level umasikini ni kitendo au Hali ya mtu kukosa mahitaji yake ya msingi Kama chakula, mavazi, makazi. Ingawaje yapo nahitaji mengine ya ziada yaliyoongezeka ambayo nayo yanachukuliwa Kama sehemu ya basic needs mfano Sex, mawasiliano ya simu n.k.
Tubakie katika maana hiyo ya msingi..
Ukishakuwa masikini upo katika kundi la wenye Laana ukubali au ukatae.
KIVIPI?
LAANA ni neno ambalo moja Kwa moja linahusu suala la kiimani, miungu, supernatural power,.
Mtu yeyote ukimsikia anasema kuhusu Laana basi ujue anaamini katika miungu.
Hakuna miungu hakuna laana.
Kisayansi hakuna laana. Ila kiimani Laana Ipo.
Kinyume cha Laana ni Baraka.
Unaposema baraka pia unazungumzia mambo ya kiimani, miungu na mambo dhahania.
Kisayansi hakuna kitu inaitwa Baraka
LAANA NI NINI?
Laana ni tamko, Kauli anayotamkiwa mtu au kikundi cha watu iliyodhamiria kudhuru au kuleta madhara, maangamizo, baada ya mtu au watu hao kuvunja kanuni au amri Fulani.
Laana inahusu zaidi miungu na mara nyingi hutolewa Kwa nguvu za miungu, au Kwa jina la miungu.
Kwa mujibu wa maandiko, laana za awali zilizotamkwa binadamu ni Kama ifuatavyo;
1. Kifo au mauti
2. Njaa( ardhi imelaaniwa hivyo mwanaume atakula Kwa jasho)
3. Mwanamke kuzaa Kwa uchungu Ile ni laana.
Kwa kifupi Laana no adhabu huku Baraka ni Zawadi.
Sasa kivipi umasikini uwe ni laana? Na iweje Masikini wawe wamelaaniwa?
Ili mtu aitwe masikini kuna viashiria, vifuatavyo ni baadhi ya viashiria kuwa mtu au jamii Fulani ni masikini
1. High mortality Rate/kiwango kikubwa cha wanaokufa.
Vifo vya watoto wachanga kuwa vingi na watu kufa mapema kabla ya uzee kutokana na sababu nyingi tuu ikiwemo Huduma duni za Afya, njaa, elimu ndogo n.k.
Kumbuka kifo ni laana na umasikini unapelekea vifo kuwa vingi. Biblia inaeleza wazi kuhusu Hilo.
2. Makazi duni na maisha duni/ poor living conditions.
Mtu anaishi makazi mabovu, mazingira hatarishi ni moja ya viashiria kuwa mtu au jamii Fulani ni masikini.
Ni laana kuishi makazi Duni. Tafsiri ya moja Kwa moja ni adhabu kuishi makazi duni, machafu, mbavu za mbwa.
3. Kiwango kikubwa cha wajinga/ High Illiteracy rate.
Kukosa elimu pia ni Dalili ya Masikini, yaani kukosa elimu ni sehemu ya laana.
Biblia inasema, watu wangu wanaangamia Kwa Kukosa Maarifa.
Laana kumbuka ndio kuangamia kwenyewe.
Ukiwa huna elimu utashindwa kuishi maisha mazuri, utakuwa mjingamjinga.
Sasa hapo kwenye elimu ndio kuna Formal, non-formal and Informal education.
Yaani kuwa mjinga tuu ni laana tosha, maana ukiwa na akili huwezi kuwa Masikini.
4. Njaa/Hunger
Kula Mlo mmoja, utapiamlo, kukosa kabisa Kula chakula ni Dalili za umasikini.
Kumbuka Njaa ni laana kama unabisha nitakuleta vifungu vyakutosha tuu! Kumbuka Ardhi ililaaniwa ili watu wafe njaa[emoji23][emoji23].
5. Maradhi
Maradhi husababisha umasikini, na umasikini husababisha Maradhi. Yaani Maradhi na umasikini ni marafiki Pacha ukimjumlisha na ndugu Yao ujinga.
Kumbuka Maradhi pia ni laana, na Biblia inaeleza
Pia kumbuka Yesu alitoa Laana yake pia kuwa asiyefanya kazi Kula na asile yaani afe kwanjaa.
Na njaa ni moja ya indicator muhimu ya umasikini.
Soma kumbukumbu la Torati 28
Utaona ni Kwa namna gani Umasikini ni laana.
Masikini wasaidie lakini wenye uhitaji/watakaokuomba msaada Ila kujipendekeza Kwa masikini wasiohitaji msaada wako nakuhakikishia matokeo yake utayapata na yatakuwa mabaya zaidi
Umasikini ni laana.
Masikini wamelaaniwa.
Kumbuka zipo laana za watu wote na zipo laana za kundi Fulani. Kifo ni laana ya kila kiumbe kilichozaliwa na Mwanamke, umasikini ni laana ya kundi Fulani la watu.
Kama ilivyo zipo baraka za watu wote na zipo baraka za watu wakundi Fulani. Nuru ya jua au mvua au hewa ni baraka Kwa watu wote, lakini madini, uzuri, Utajiri, nguvu ni baraka Kwa kundi Fulani la watu.
Huo ndio ukweli.
Umasikini ndio ushetani wenyewe, ndio laana, ni mauti.
Unaposema Tanzania nchi masikini maana yake nchi iliyolaaniwa..aisee kuchomoka itakuwa issue bongo.
Scientism ni tatizo.Scientifically Kila mtu anapata riziki kulingana na thinking capacity yake Mwenye uwezo mdogo wa kufikiri ataangukia vibarua vya kwenye mkonge wakati mwingine aliekaa darasani due to his high intelligence anaangukia BOT.
God, science and religion depend on one another to finalize findings.
How?Scientism ni tatizo.
Ingekuwa umaskini ni laana basi juhudi za kuinua maskini zingekuwa hazifanikiwi..Andiko lako linaonesha kuwa umasikini ni ujinga.
Na mimi pia nimeamua Kuona hivyo ...
Ujinga waweza kuondoshwa,
Kama uko na resources karibu unaweza kutupatia maana mbali mbali za laana/curse ujinga/ignorance.
Kama vile umechanganya mada mkuu Heriel Umemix science Pamoja na dini Andiko lako linaleta mkanganyiko
Nakubaliana na wewe mkuu , umasikini ni kukosa maarifa au kuwa na maarifa lakini kushindwa kuyatumia.Ingekuwa umaskini ni laana basi juhudi za kuinua maskini zingekuwa hazifanikiwi..
Hakuna cha laana ni mazingira yasiyo rafiki/wezeahi ndio humfanya mtu kuwa maskini.
Mfumo unataka wengine wawe masikini wengine wawe matajiri. Ndio mana hata watu wote tukisoma wapo watakaofanya kazi zinazolet umasikini. Huu mfumo ni piramidi. Lazima Kuna jitu liwe juu zaidi ya wenzie. Suala la umasikin Lita kuwepo mpaka mfumo huu ubadilike. La sivyo tupunguze tu gep Kati ya maskini na tajiri lisiwe kubwa. Manake haiwezekani ELON MUSK awe na hela nyingi kuliko WatAnzania wote dunianiNakubaliana na wewe mkuu , umasikini ni kukosa maarifa au kuwa na maarifa lakini kushindwa kuyatumia.
Nini kifanyike kujikwamua kwenye umasikini At individual level first ...
mtu/mwanadamu amepewa akili Utashi wa kukabiliana na mazingira yanayomzunguka/kutatua Changamoto zake.
Kwani kuwa na pesa ndo utajiri?