Nampinga Robert Heriel kuhusu dhana ya umasikini

Nampinga Robert Heriel kuhusu dhana ya umasikini

Jocasta

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2014
Posts
475
Reaction score
600
Habari ndugu zangu, imenilazimu kuandika kupinga dhana iliyotolewa na member mwenzetu tajwa hapo juu

Hili Ni bandiko linalolenga kukosoa mtazamo wake juu ya dhana fikirishi ya umaskini ambayo aliieleza Kama "Laana" Jambo ambalo si sahihi

✓Kwanza ameshindwa kuonesha ya kwamba binadamu awe na Nini au akoswe Nini ndo awe maskini hii Ni kwasababu dhana ya umaskini Haina maana moja, Maskini wa Dar yaweza kuwa Tajiri Tarime

✓Biblia na vitabu vingine vya kiroho vinatambua dhana ya umaskini na vimeshauri tuwasaidie kwa kuweka hazina zetu juu Yao kwa kuwapa mavazi na chakula kwakuwa tupo nao siku zote
✓Umaskini siyo Laana Kama anavyohisi mwenzetu,Binadamu anaweza zaliwa maskini,yeye kuwa tajili Ni juhudi zake binafsi

Naomba kuwasilisha ndugu zangu
 
Habari ndugu zangu,imenilazimu kuandika kupinga dhana iliyotolewa na member mwenzetu tajwa hapo juu

Hili Ni bandiko linalolenga kukosoa mtazamo wake juu ya dhana fikirishi ya umaskini ambayo aliieleza Kama "Laana" Jambo ambalo si sahihi
✓kwanza ameshindwa kuonesha ya kwamba binadamu awe na Nini au akoswe Nini ndo awe maskini hii Ni kwasababu dhana ya umaskini Haina maana moja,Maskini wa Dar yaweza kuwa Tajiri Tarime
✓Biblia na vitabu vingine vya kiroho vinatambua dhana ya umaskini na vimeshauri tuwasaidie kwa kuweka hazina zetu juu Yao kwa kuwapa mavazi na chakula kwakuwa tupo nao siku zote
✓Umaskini siyo Laana Kama anavyohisi mwenzetu,Binadamu anaweza zaliwa maskini,yeye kuwa tajili Ni juhudi zake binafsi

Naomba kuwasilisha ndugu zangu
Taikon uje huku upangue hoja hii nina imani uko safarini Dsm kwasasa.
 
Usibebe kilakitu kinachoandikwa humu ....Kila mtu huandika mtazamo wake Kaz kwako msomaji.Nitasema Mandingo ndo yenyewe ukienda kuiga kuparamia Mandingo utaishia kupasuliwa kizazi Kumbe saiz Yako ni bamia
 
Hata mimi nilimuuliza masikini ni nani lakini hakusema.Mwenye tumilioni 3 benki na m-pesa laki saba anajiona tajiri lakini pesa hiyo ni ya kununulia mahitaji ya wiki moja huko Washington Dc.Je,masikini ni nani?? Au turejee maandiko ambayo ndo yanamweleza vizuri masikini ni nani,bahati mbaya yeye haamini hata maandiko hayo maana alipingana nayo LIVE kwa kusema tusiwasaidie!
 
Taikon wa fasihi yako sahihi kabisa
FB_IMG_1661582069159.jpg


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Nakusapoti asilimia zote ,like andiko la Taikon moja Kati ya andiko lake la hovyo kuwahi kuleta humu haswa aliposema umasikini ni laana wakati Dunia inahitaji utofauti ili maisha yaendelee na wafuasi wengi wa Mitume na Manabii walikua watu wa chini na masikini.
Hata Yesu alifanya kazi na walio Maskini
 
Habari ndugu zangu,imenilazimu kuandika kupinga dhana iliyotolewa na member mwenzetu tajwa hapo juu

Hili Ni bandiko linalolenga kukosoa mtazamo wake juu ya dhana fikirishi ya umaskini ambayo aliieleza Kama "Laana" Jambo ambalo si sahihi
✓kwanza ameshindwa kuonesha ya kwamba binadamu awe na Nini au akoswe Nini ndo awe maskini hii Ni kwasababu dhana ya umaskini Haina maana moja,Maskini wa Dar yaweza kuwa Tajiri Tarime
✓Biblia na vitabu vingine vya kiroho vinatambua dhana ya umaskini na vimeshauri tuwasaidie kwa kuweka hazina zetu juu Yao kwa kuwapa mavazi na chakula kwakuwa tupo nao siku zote
✓Umaskini siyo Laana Kama anavyohisi mwenzetu,Binadamu anaweza zaliwa maskini,yeye kuwa tajili Ni juhudi zake binafsi

Naomba kuwasilisha ndugu zangu

Mkuu Kwanza Nashukuru Kwa kunipinga na kutoa Mtazamo wako dhidi ya mtazamo wangu.

Turudi kwenye Mjadala.

Topic ya Poverty ipo Kidato cha tatu Kwa waliofika elimu ya Upili.
Maana ya umasikini inafahamika Kwa waliofika madarasa hayo.
Individual level umasikini ni kitendo au Hali ya mtu kukosa mahitaji yake ya msingi Kama chakula, mavazi, makazi. Ingawaje yapo nahitaji mengine ya ziada yaliyoongezeka ambayo nayo yanachukuliwa Kama sehemu ya basic needs mfano Sex, mawasiliano ya simu n.k.
Tubakie katika maana hiyo ya msingi..

Ukishakuwa masikini upo katika kundi la wenye Laana ukubali au ukatae.
KIVIPI?

LAANA ni neno ambalo moja Kwa moja linahusu suala la kiimani, miungu, supernatural power,.
Mtu yeyote ukimsikia anasema kuhusu Laana basi ujue anaamini katika miungu.
Hakuna miungu hakuna laana.

Kisayansi hakuna laana. Ila kiimani Laana Ipo.
Kinyume cha Laana ni Baraka.
Unaposema baraka pia unazungumzia mambo ya kiimani, miungu na mambo dhahania.
Kisayansi hakuna kitu inaitwa Baraka

LAANA NI NINI?
Laana ni tamko, Kauli anayotamkiwa mtu au kikundi cha watu iliyodhamiria kudhuru au kuleta madhara, maangamizo, baada ya mtu au watu hao kuvunja kanuni au amri Fulani.
Laana inahusu zaidi miungu na mara nyingi hutolewa Kwa nguvu za miungu, au Kwa jina la miungu.

Kwa mujibu wa maandiko, laana za awali zilizotamkwa binadamu ni Kama ifuatavyo;
1. Kifo au mauti
2. Njaa( ardhi imelaaniwa hivyo mwanaume atakula Kwa jasho)
3. Mwanamke kuzaa Kwa uchungu Ile ni laana.

Kwa kifupi Laana no adhabu huku Baraka ni Zawadi.

Sasa kivipi umasikini uwe ni laana? Na iweje Masikini wawe wamelaaniwa?

Ili mtu aitwe masikini kuna viashiria, vifuatavyo ni baadhi ya viashiria kuwa mtu au jamii Fulani ni masikini

1. High mortality Rate/kiwango kikubwa cha wanaokufa.
Vifo vya watoto wachanga kuwa vingi na watu kufa mapema kabla ya uzee kutokana na sababu nyingi tuu ikiwemo Huduma duni za Afya, njaa, elimu ndogo n.k.

Kumbuka kifo ni laana na umasikini unapelekea vifo kuwa vingi. Biblia inaeleza wazi kuhusu Hilo.

2. Makazi duni na maisha duni/ poor living conditions.
Mtu anaishi makazi mabovu, mazingira hatarishi ni moja ya viashiria kuwa mtu au jamii Fulani ni masikini.
Ni laana kuishi makazi Duni. Tafsiri ya moja Kwa moja ni adhabu kuishi makazi duni, machafu, mbavu za mbwa.

3. Kiwango kikubwa cha wajinga/ High Illiteracy rate.
Kukosa elimu pia ni Dalili ya Masikini, yaani kukosa elimu ni sehemu ya laana.
Biblia inasema, watu wangu wanaangamia Kwa Kukosa Maarifa.
Laana kumbuka ndio kuangamia kwenyewe.
Ukiwa huna elimu utashindwa kuishi maisha mazuri, utakuwa mjingamjinga.
Sasa hapo kwenye elimu ndio kuna Formal, non-formal and Informal education.

Yaani kuwa mjinga tuu ni laana tosha, maana ukiwa na akili huwezi kuwa Masikini.

4. Njaa/Hunger
Kula Mlo mmoja, utapiamlo, kukosa kabisa Kula chakula ni Dalili za umasikini.
Kumbuka Njaa ni laana kama unabisha nitakuleta vifungu vyakutosha tuu! Kumbuka Ardhi ililaaniwa ili watu wafe njaa😂😂.

5. Maradhi
Maradhi husababisha umasikini, na umasikini husababisha Maradhi. Yaani Maradhi na umasikini ni marafiki Pacha ukimjumlisha na ndugu Yao ujinga.
Kumbuka Maradhi pia ni laana, na Biblia inaeleza

Pia kumbuka Yesu alitoa Laana yake pia kuwa asiyefanya kazi Kula na asile yaani afe kwanjaa.
Na njaa ni moja ya indicator muhimu ya umasikini.

Soma kumbukumbu la Torati 28
Utaona ni Kwa namna gani Umasikini ni laana.

Masikini wasaidie lakini wenye uhitaji/watakaokuomba msaada Ila kujipendekeza Kwa masikini wasiohitaji msaada wako nakuhakikishia matokeo yake utayapata na yatakuwa mabaya zaidi

Umasikini ni laana.
Masikini wamelaaniwa.

Kumbuka zipo laana za watu wote na zipo laana za kundi Fulani. Kifo ni laana ya kila kiumbe kilichozaliwa na Mwanamke, umasikini ni laana ya kundi Fulani la watu.

Kama ilivyo zipo baraka za watu wote na zipo baraka za watu wakundi Fulani. Nuru ya jua au mvua au hewa ni baraka Kwa watu wote, lakini madini, uzuri, Utajiri, nguvu ni baraka Kwa kundi Fulani la watu.

Huo ndio ukweli.

Umasikini ndio ushetani wenyewe, ndio laana, ni mauti.
 
Mkuu Kwanza Nashukuru Kwa kunipinga na kutoa Mtazamo wako dhidi ya mtazamo wangu.

Turudi kwenye Mjadala.

Topic ya Poverty ipo Kidato cha tatu Kwa waliofika elimu ya Upili.
Maana ya umasikini inafahamika Kwa waliofika madarasa hayo.
Individual level umasikini ni kitendo au Hali ya mtu kukosa mahitaji yake ya msingi Kama chakula, mavazi, makazi. Ingawaje yapo nahitaji mengine ya ziada yaliyoongezeka ambayo nayo yanachukuliwa Kama sehemu ya basic needs mfano Sex, mawasiliano ya simu n.k.
Tubakie katika maana hiyo ya msingi..

Ukishakuwa masikini upo katika kundi la wenye Laana ukubali au ukatae.
KIVIPI?

LAANA ni neno ambalo moja Kwa moja linahusu suala la kiimani, miungu, supernatural power,.
Mtu yeyote ukimsikia anasema kuhusu Laana basi ujue anaamini katika miungu.
Hakuna miungu hakuna laana.

Kisayansi hakuna laana. Ila kiimani Laana Ipo.
Kinyume cha Laana ni Baraka.
Unaposema baraka pia unazungumzia mambo ya kiimani, miungu na mambo dhahania.
Kisayansi hakuna kitu inaitwa Baraka

LAANA NI NINI?
Laana ni tamko, Kauli anayotamkiwa mtu au kikundi cha watu iliyodhamiria kudhuru au kuleta madhara, maangamizo, baada ya mtu au watu hao kuvunja kanuni au amri Fulani.
Laana inahusu zaidi miungu na mara nyingi hutolewa Kwa nguvu za miungu, au Kwa jina la miungu.

Kwa mujibu wa maandiko, laana za awali zilizotamkwa binadamu ni Kama ifuatavyo;
1. Kifo au mauti
2. Njaa( ardhi imelaaniwa hivyo mwanaume atakula Kwa jasho)
3. Mwanamke kuzaa Kwa uchungu Ile ni laana.

Kwa kifupi Laana no adhabu huku Baraka ni Zawadi.

Sasa kivipi umasikini uwe ni laana? Na iweje Masikini wawe wamelaaniwa?

Ili mtu aitwe masikini kuna viashiria, vifuatavyo ni baadhi ya viashiria kuwa mtu au jamii Fulani ni masikini

1. High mortality Rate/kiwango kikubwa cha wanaokufa.
Vifo vya watoto wachanga kuwa vingi na watu kufa mapema kabla ya uzee kutokana na sababu nyingi tuu ikiwemo Huduma duni za Afya, njaa, elimu ndogo n.k.

Kumbuka kifo ni laana na umasikini unapelekea vifo kuwa vingi. Biblia inaeleza wazi kuhusu Hilo.

2. Makazi duni na maisha duni/ poor living conditions.
Mtu anaishi makazi mabovu, mazingira hatarishi ni moja ya viashiria kuwa mtu au jamii Fulani ni masikini.
Ni laana kuishi makazi Duni. Tafsiri ya moja Kwa moja ni adhabu kuishi makazi duni, machafu, mbavu za mbwa.

3. Kiwango kikubwa cha wajinga/ High Illiteracy rate.
Kukosa elimu pia ni Dalili ya Masikini, yaani kukosa elimu ni sehemu ya laana.
Biblia inasema, watu wangu wanaangamia Kwa Kukosa Maarifa.
Laana kumbuka ndio kuangamia kwenyewe.
Ukiwa huna elimu utashindwa kuishi maisha mazuri, utakuwa mjingamjinga.
Sasa hapo kwenye elimu ndio kuna Formal, non-formal and Informal education.

Yaani kuwa mjinga tuu ni laana tosha, maana ukiwa na akili huwezi kuwa Masikini.

4. Njaa/Hunger
Kula Mlo mmoja, utapiamlo, kukosa kabisa Kula chakula ni Dalili za umasikini.
Kumbuka Njaa ni laana kama unabisha nitakuleta vifungu vyakutosha tuu! Kumbuka Ardhi ililaaniwa ili watu wafe njaa[emoji23][emoji23].

Pia kumbuka Yesu alitoa Laana yake pia kuwa asiyefanya kazi Kula na asile yaani afe kwanjaa.
Na njaa ni moja ya indicator muhimu ya umasikini.

Soma kumbukumbu la Torati 28
Utaona ni Kwa namna gani Umasikini ni laana.

Masikini wasaidie lakini wenye uhitaji/watakaokuomba msaada Ila kujipendekeza Kwa masikini wasiohitaji msaada wako nakuhakikishia matokeo yake utayapata na yatakuwa mabaya zaidi

Umasikini ni laana.
Masikini wamelaaniwa.

Kumbuka zipo laana za watu wote na zipo laana za kundi Fulani. Kifo ni laana ya kila kiumbe kilichozaliwa na Mwanamke, umasikini ni laana ya kundi Fulani la watu.

Kama ilivyo zipo baraka za watu wote na zipo baraka za watu wakundi Fulani. Nuru ya jua au mvua au hewa ni baraka Kwa watu wote, lakini madini, uzuri, Utajiri, nguvu ni baraka Kwa kundi Fulani la watu.

Huo ndio ukweli.

Umasikini ndio ushetani wenyewe, ndio laana, ni mauti.
Kuna Fukara, masikini na Tajiri

Fukara ni mtu ambae anashindwa kumudu mahitaji ya msingi kama vile chakula, malazi na makazi

Masikni ni mtu ambae hana uwezo wa kukidhi mahitaji yake ya msingi kama nilivyoainisha hapo juu na kuwa na akiba

Tajiri ni mungu peke mkwasi wa kila kitu,

Kinyume cha laana ni baraka ukimaanisha Laana ni kwa masikini na Baraka ni kwa matajiri sio kweli!

Kuna masikini wana baraka na matajiri wenye laana imagine mtu ni tajiri lakini ameupata kwa kuua, kudhurumu, kuchukua mali za mayatima n.k . Muda mwengine ni tajiri lakini ana migogoro ya kifamilia, anaandamwa na magonjwa na mambo mengine mengi tu.

Na,unakuta kuna,masikini wengine wanaishi vizuri familia zao zimetulia, anakula vizuri ,anaishi vzr hana msongo wa mawazo na mambo mengine mengi tu.

Point yangu sio kila masikini ana laana wengine ni mtihani kutoka kwa menyezi mungu hapa duniani
 
Kuna Fukara, masikini na Tajiri

Fukara ni mtu ambae anashindwa kumudu mahitaji ya msingi kama vile chakula, malazi na makazi

Masikni ni mtu ambae ana uwezo wa kukidhi mahitaji yake ya msingi kama nilivyoainisha hapo juu na kuwa na akiba

Tajiri ni mungu peke mkwasi wa kila kitu,

Kinyume cha laana ni baraka ukimaani
sha Laana ni kwa masikini na Baraka ni kwa matajiri sio kweli!

Kuna masikini wana baraka na matajiri wenye laana imagine mtu ni tajiri lakini ameupata kwa kuua, kudhurumu, kuchukua mali za mayatima n.k . Muda mwengine ni tajiri lakini ana migogoro ya kifamilia, anaandamwa na magonjwa na mambo mengine mengi tu.

Na,unakuta kuna,masikini wengine wanaishi vizuri familia zao zimetulia, anakula vizuri ,anaishi vzr hana msongo wa mawazo na mambo mengine mengi tu.

Point yangu sio kila masikini ana laana wengine ni mtihani kutoka kwa menyezi mungu hapa duniani

Ukishakuwa masikini tayari unalaana huwezi ishi vizuri ukiwa masikini wewe. Acha kudanganya au kujidanganya hapa.

Mkeo habari vizuri,
Kila siku mlo mmoja,
Makazi mabovu,
Watoto wanasoma Kwa tabu, bado useme unaishi vizuri Kwa Amani?

Ukishakuwa masikini tayari unalaana unachopaswa kukifanya ni kukabiliana na laana hiyo.

Matajiri wenye laana wapo lakini sio katika kipengele cha Pesa au Mali.

Laana ni adhabu,
Ndio maana nikataja indicators umasikini hapo na kuzifungamanisha na zinavyoingiliana na laana.

Sijawahi ona Masikini anayeishi Vizuri.
 
Kuna Fukara, masikini na Tajiri

Fukara ni mtu ambae anashindwa kumudu mahitaji ya msingi kama vile chakula, malazi na makazi

Masikni ni mtu ambae ana uwezo wa kukidhi mahitaji yake ya msingi kama nilivyoainisha hapo juu na kuwa na akiba

Tajiri ni mungu peke mkwasi wa kila kitu,

Kinyume cha laana ni baraka ukimaani
sha Laana ni kwa masikini na Baraka ni kwa matajiri sio kweli!

Kuna masikini wana baraka na matajiri wenye laana imagine mtu ni tajiri lakini ameupata kwa kuua, kudhurumu, kuchukua mali za mayatima n.k . Muda mwengine ni tajiri lakini ana migogoro ya kifamilia, anaandamwa na magonjwa na mambo mengine mengi tu.

Na,unakuta kuna,masikini wengine wanaishi vizuri familia zao zimetulia, anakula vizuri ,anaishi vzr hana msongo wa mawazo na mambo mengine mengi tu.

Point yangu sio kila masikini ana laana wengine ni mtihani kutoka kwa menyezi mungu hapa duniani

Yaani familia Masikini watoto hawajaenda shule kisa Ada, Itulie😂😂
Mkeo hujamnunulia zawadi mwaka watano bado familia Itulie.
Huna pesa ya Hospitali bado familia itulie😀

Mkuu kuwa Sirius kidogo
 
Robert haya mambo umeyachanganya mno,wacha ibaki hivyo kama zamani.Kwa unyongaji huu wa hoja kama bit za Funga huna cha kuboresha!

Kwa ulivyoeleza basi katika jamii hamna mtu masikini!
 
Back
Top Bottom