Namibia yapunguza kodi ya mafuta kwa 50%

Namibia yapunguza kodi ya mafuta kwa 50%

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,434
Reaction score
14,666
Serikali ya Namibia kupitia Waziri wa Nishati na Madini, Modestus Amutse wamepunguza kodi ya Mafuta kwa asilimia 50 ili Makampuni yasipandishe bei ambapo itaumiza Wananchi, Amutse ametoa tangazo hilo tangu Machi 27 ambapo unafuu wa Kodi utadumu kwa miezi mitatu wakati ambao wanasikilizia hali ya vita ambapo Serikali ya Namibia itapoteza mapato ya dola Million 29 kila mwezi kutokana na Unafuu huo walioweka.

Bei mpya za Mafuta nchini humo zilizotangazwa leo kuna ongezeko kidogo kwenye petrol ambapo imepanda kwa dola 0.15 sawa na SHILLING 388 za Kitanzania huku Diesel ikipanda kwa dola 0.23 sawa na SHILLING 595 za Kitanzania.

Chanzo: Ecofin Agency
 
Ukija Taleban republic ndio wamegeuza fursa nchi ya kingese sana hii!
20250831_150127.jpg
 
Wapunguze kodi kwa miezi mitatu ili kuangalia hali ya vita huko mnaendeleaje kwa jinsi ilivyo mafuta yakua bei ndogo Zambia wakati wakitumia bandari yetu na Tazama pipe line...
 
Hizi ndio serikali zinajielewa, take austerity measures kwa kipindi kifupi hadi hali itulie, unawasaidis wananchi wako. Tanzania viongozi wengi ni wapiga dili, watu kati, usitegemee situation za hivi kukuta serikali ikikaa upande wa wananchi.
Cut VAT and other taxes by 50% walau, ili kupunguza mzigo kwa watu wako, wewe upo busy kuongeza bei kwa almost Tzs. 1000 huku unawapiga biti wasafirishaji wasipandishe bei, are you for real?
 
Back
Top Bottom