Nalia kama sio kutoa machozi, wanaume mkoje?

Nalia kama sio kutoa machozi, wanaume mkoje?

Wana JF,

Niliempata haeleweki kabadilika ghafla, hivi nina nini mimi hapa nalia tu, kweli wanaume pasua kichwa.

Nimechoka sasa wacha nitulie tu Mungu ataniletea.

Sitaki mwanaume kuanzia sasa
Wanaume huwa tunaumizwa sana,ukikuta mwanaume kaumizwa basi ni mara kumi ya mwanamke aliyeumizwa asikwambie mtu alafu huwa hata hamjali wala kuwa na huruma

Sisi huwa tunawekeza upendo pamoja na kuwahudumia pia huenda mwanamke akawa na kipaumbele kuliko hata ndugu wakati mwingine huduma zote muhimu na zisizo muhimu
Likija kutokea la kutokea maumivu yake huwa hayapimiki huwa tunavumilia tu na wakati mwingine watu wanahofia kuchekwa huenda maendeleo yako yalisimama umepot3za pesa nyingi
Wewe unalia kwa moja tu
 
Pole ndugu yangu.. sina la kuongeza, maana kumshaur mtu wakati stress ni kumpigilia msumali wa moto na kumtonesha donda

Ila tambua jambo moja tu la msingi, hii tabia ya kuumizwa na mmoja ukajumlisha wote duniani si sahihi.. wanaume na wanawke wote ni viumbe, unavyoshutumu wanaume utasema wanawake nyinyi ndio safi, kumbe kuna wanawake nao si timamu ambao nao wakiharibu mwanaume nasi utasikia wanawake hawana maana.. ni shutuma tu kwa kila upande, ila kiuhalisia kila upande kuna wazuri na wabovu, sasa sote ni binaadamu hatujakamilika..

Nikwambie tu hapo bahati yako mbaya, kitulize tu chini utampata mwanaume safi, ambae mwisho utajuta kwanin haukumjua mapema.
[emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124]
 
Si kila mwanaume ndiye uliyeandikiwa, hata viatu visipokutosha vitabana au kupwaya
Hapa tu kwenye kusema "kuandikiwa mme au mke" na utajiri ama shida ndo huwa sielewi kabisa kama kuna ukweli wowote.
Kama kungekuwa na kuandikiwa kwa nini wengine kila kukicha tunalia tu kwa kukutana na waumizao, kwa nini anayeandika asitupeleke moja kwa moja kwa wale aliotuandikia ili kuepusha vibuti na divorce za mara kwa mara?
Unakuta mtu amekaa na mpenzi, mke au mme kwa miaka mingi halafu inakuja tu paaah wanaachana halafu mtu anakuja anasema ilikuwa imeandikwa
 
Usilie, tafuta mwinginempaka kisomeke dada na ukimpata mgande akuoe kabisa
 
Hapa tu kwenye kusema "kuandikiwa mme au mke" na utajiri ama shida ndo huwa sielewi kabisa kama kuna ukweli wowote.
Kama kungekuwa na kuandikiwa kwa nini wengine kila kukicha tunalia tu kwa kukutana na waumizao, kwa nini anayeandika asitupeleke moja kwa moja kwa wale aliotuandikia ili kuepusha vibuti na divorce za mara kwa mara?
Unakuta mtu amekaa na mpenzi, mke au mme kwa miaka mingi halafu inakuja tu paaah wanaachana halafu mtu anakuja anasema ilikuwa imeandikwa
Mshirikishe Mungu katika mawazo na maamuzi yako. Hakuna aliye kamiliia lakini wote mkiwa na hofu vya Mungu mtatafakari kabla ya kutenda.
Kibaya ni kulazimisha penzi lisipokuwepo, ukifika mahali unamaliza kazi lakini hutaki kurudi nyumbani jua hapo ni wrong number.

Mungu hutupangia watu wa kuowa au kuolewa nao lakini tunakuwa na papara either kuanza ngono zembe mapema, kuolewa kwaajili ua utajiri so kuoa uzuri wa sura. Wengine hukutana na andiko wakiwa 50+.
 
Wana JF,

Niliempata haeleweki kabadilika ghafla, hivi nina nini mimi hapa nalia tu, kweli wanaume pasua kichwa.

Nimechoka sasa wacha nitulie tu Mungu ataniletea.

Sitaki mwanaume kuanzia sasa
Hutak Mwanaume Kuanzia Sasa Hapo Hapo Unasema Mungu Atakuletea

Ndio Maana anakuletea Wabovu
 
Tatzo inbox yako haujibu, hapo ndipo unapopishana na sisi akina Adamu wafia tunda [emoji56]
 
Namshukuru mungu nimepata mwanamke anaejielewa kuchepuka kwangu ni hulka ya kiuanaume tu ila
Hana wivu wa kijinga
Ananiheshimu
Ingawa siendani nae mpaka sasa ananipenda na kuniheshimu
 
Back
Top Bottom