Nakuwa mzito kuomba mchango wa harusi

Nakuwa mzito kuomba mchango wa harusi

Hakikisha harusi yako unagharamia kila kitu mwenyewe hakikisha hakuna mtu anatoa hata mia yake ,utakuja kunishukuru
Ni kweli mkuu. Pia harusi sio lazima. Mwaka 2016 mtu wangu wa karibu alifunga ndoa na mkewe kanisani alafu wakeanda nyumbani kupumzika na ni mtu mwenye kipato kikubwa sana. Kwa wakati huo angeweza kufanya hata harusi ya milioni 70 kwa pesa zake. Ndugu walimaindi sana lakini hakuna namna. Anaishi na mkewe kwa amani zote hadi sasa. Huyu jamaa hachangii sherehe yoyote ile hiyo ni kanuni yake.
 
Ni kweli mkuu. Pia harusi sio lazima. Mwaka 2016 mtu wangu wa karibu alifunga ndoa na mkewe kanisani alafu wakeanda nyumbani kupumzika na ni mtu mwenye kipato kikubwa sana. Kwa wakati huo angeweza kufanya hata harusi ya milioni 70 kwa pesa zake. Ndugu walimaindi sana lakini hakuna namna. Anaishi na mkewe kwa amani zote hadi sasa. Huyu jamaa hachangii sherehe yoyote ile hiyo ni kanuni yake.
Ndiyo inavyotakiwa
 
Binafsi sitachanga mchango wa harusi. Harusi n kujipanga.
 
Dunia imebadilika ,uchumi umebadilika ,ifike mahali harusi za michango zipigwe marufuku.
Jamii inapenda hizi mambo balaa,mi niliwaambia sitaki sherehe na makorokoro yoyote wazee ndo walikuwa vinara wa kuniteta navyojisikia na kujiona mara kiburi ikafikia hatua mwanaume akaitwa tapeli mara mume wa mtu,, bla bla zikawa nyingi,, nilichofanya niliolewa kimya zile za kuibana nikawakata ngebe, watu 6 wanatosha kabisa kukamilisha ndoa ni wanandoa, wasimamizi mchungaji, mpiga picha, ndugu mmoja mmoja wa pande zote au hata wasipokuwepo, deal done
 
Kaka iyo ni plan nzuri sana ila Sasa utakutana na wazee wa Mila na deaturi Wana Fanya mambo kuwa magumu hasa uku uchagani..utajikuta unaingia gharama kubwa zaidi adi utachanganyikiwa ..
Unaoa wapi mzee au Rombo
 
Jamii inapenda hizi mambo balaa,mi niliwaambia sitaki sherehe na makorokoro yoyote wazee ndo walikuwa vinara wa kuniteta navyojisikia na kujiona mara kiburi ikafikia hatua mwanaume akaitwa tapeli mara mume wa mtu,, bla bla zikawa nyingi,, nilichofanya niliolewa kimya zile za kuibana nikawakata ngebe, watu 6 wanatosha kabisa kukamilisha ndoa ni wanandoa, wasimamizi mchungaji, mpiga picha, ndugu mmoja mmoja wa pande zote au hata wasipokuwepo, deal done
Ilikuwa nzuri sana

Sent from my RMX3231 using JamiiForums mobile app
 
Nilikuwa na mawazo kama yako kumbe kuchangisha watu siyo kwamba Huna hela ya harusi bali ni kutambua uwepo wao. Andaa kadi weka hata kiwango kidogo cha kuchangiwa. Binadamu usipochangisha na kuwaalika waje kula inaonekana kama dharau hiyo harusi yako watahudhiria watoto tu.

Ni kweli, lkn pia baadhi ya ndugu na jamaa hawatahudhuria sababu tu hawajatoa mchango.

Ukiwa na uwezo michango haina maana.
 
hatimaye harusi ili malizika vizuri Na mshukuru Mungu.

niseme michango ni jambo la kawaida sana na si wote wana penda kutoa michango,
nimejifunza yafuatayo wakati naomba michango.
1.kutoa ni moyo
2.utazungushwa na baadhi ya watu wakati unaomba mchango adi utajuta kwa nini unaomba.
3.kuna watu wana jitoa sana haijalishi anaifahamu historia yako au vip.
4.kuna watu hawatajigusa kabisa kukuchangia ,yan ni kama una wasumbua yani, na unakuta ni watu ambao upo nao katika mazingira ya kazi ya kila siku.
5.usidharau mtu ,aisee kuna mtu nilimfuata anichangie kiutani ila alipambana adi akanichangia kwa wakati,na sikumdhania kabisa.
6.nimejifunza pia kujitoa hata kama sina undugu na urafiki na mtu ,huwezi jua kujitoa kwako mara ya kwanza ndio una anza urafiki wa kudumu.
7.usichukie mtu kama hajakupa mchango ,huwezi jua anachopitia katika maisha yake.
8.tabasamu na kila mtu hata kama hajakupatia mchango.
9.washukuru wote waliokuchangia ukafanikisha harusi yako.
10.penda kujitoa hata kama unajitoa kwa kidogo haijalishi .wengi wanadhani kujitoa ni lazima ujitoe kwa kikubwa hapana.
 
[emoji23][emoji23] Na ukifuata kila anachokitaka mwanamke itakugharimu sana , vingine tunaforce kibingwa !! Mwanamke yupo tayari hata muingie madeni lakini sherehe ifanyike !

Unamuuliza mrembo hapa naona hujishughulishi na chochote kwanini tusifanye kisherehe kidogo halafu baadhi ya pesa nikufungulie Goli sehemu angalau usiwe mama wa nyumbani ujishikie visenti kidogo uwe na uhuru wa kifedha !! Atanuna atakwambia tutatafuta nyingine ila sherehe ya kufana ifanyike !

Baada ya muda huyo huyo atakurudia analalamika hapendi kukaa nyumbani ,ukimwambia we si ndo ulisema tutafuta nyingine ! Anakuruka anakwambia we si ndo kichwa cha Familia kwanini hukunizuia [emoji3]
Fear women.
KATAA NDOA
 
Back
Top Bottom