Najuta kuoa mwanamke mwenye mtoto

Najuta kuoa mwanamke mwenye mtoto

Magonjwa mengine tunayatafuta wenyewe. Haya maumivu YA kichwa huanza pole pole .
 
Ni baadhi Mkuu si wote wako hivyo, kwa mfano unaweza kujenga penzi zito na dada ambaye yule aliyezaa naye hayuko tena duniani, ila ni mtihani mgumu kusema kweli kwa sababu baadhi ya wanaume hawapendi kumuona mzazi mwenzao akiishi katika raha na starehe hivyo watata futa sababu za kuanzisha tafrani ambazo bila shaka zitakugusa wewe kama mume na kuiona ndoa yote chungu.




mwanaume wakuingilia penzi langu jipya bado hajazaliwa. yaani tuachane eti nimeolewa utaanzaje kunifwatafwata nigombane na mume wangu? hainiingii akilini kitendo cjakuachana na mawasiliano yameisha ada ya mtoto atawasiliana na waalimu wa mtoto.

huyo mkewe ni tabia yake tu aisee na maharage alokula cjui ni ya wapi
 
Nilichoona umenogewa na vitatu
1) lift ya gari
2) penzi la huyo dada
3) Kusaidiwa matumizi

Hebu fanya kazi kwa juhudi acha kupenda miteremko kijana maana umeanza kujitetea kwenye mshahara

Utapata Mimba isiyo kuwa na Baba, Acha kukurupuka.
 
T
Waheshimiwa habari za mida
Mimi ni IT specialist kwenye shirika moja lisilo la kiserikali mshahara wangu ni Wa kati si mkubwa sana wala si mdogo sana

Lakini pia Mimi ni lecturer part time nafundisha jioni wafanyakazi katika chuo kimoja hapa DSM

Nimeoa na Nina watoto wawili
Huyu mke wangu ni chotara Wa kiarabu
Wakati tumeanza tumeanza kudate hakuniambia kama ana mtoto na kwa kweli alivyo mzuri sikutilia shaka kama ana mtoto maana hata nyonyo zake zilikuaa zimesimama kama mtoto anaebalehe

Baadae mapenzi yaliponoga ndipo akaniambia kuwa ana mtoto alie darasa la kwanza yupo kwa mama mzazi yaani bibi Wa mtoto

Kwa kuwa nilikua tayari nimezama kwenye mahaba mazito ikabidi nikubali tu maana by that time nilishatangaza ndoa ilikua ni point of no return

Ila mchumba alianihakikishia kuwa mtoto wake hatakua kikwazo kwenye ndoa yetu na kwamba huduma zote za malezi ikiwa ni pamoja na shule, malazi,maradhi na mengineyo yatakua chini ya baba Wa mtoto
Huo ndio ukawa mkataba wetu na kwamba mtoto ataishi kwa bibi na baadae atahamia kwa baba mzazi ambae ni Mwarabu mwenzie

Akabadli dini kuja ukristo tukafunga ndoa haikua shida maana mama ake pia ni mkristo baba ndio muislam na aliwatelekeza siku nyingi

Miezi sita baada ya ndoa akamleta mtoto kwetu kuishi permanent kinyume na mkataba wetu, anyway nikawa na roho ya utu nikasema haina shida kuepusha Shari

Mtoto wake alipofika darasa LA NNE wakampeleka boarding sisi hapo tuna watoto wawili mapacha Wa miaka minne kasoro nadhani
Mimi ndie nililipa ada ya boarding

Siku moja katikati ya wiki nilibeba mahitaji kadhaa nikampelekea yule mtoto shuleni niliomba wakaniruhusu kuingia pale
Surprisingly matron akaniambia huyo mtoto mbona ana vitu vya kutosha mama ake na baba ake walikua hapa juzi siku tano hivi zimepita.
Akaniuliza kwan we nani Wa mtoto nikamweleza

Akashangaa akaniambia mbona walikua wamekaa na mtoto kama ni familia inayoishi pamoja akanipa kama umbea flani hivi
Nilishangaa kwa kuwa mke wangu hakuniambia kama alienda kwa mtoto na mzazi mwenzie alikuwepo

Visiting day moja nikaenda na watoto wangu kumuona mwenzao, mke wangu aliondoka mapema akatangulia tulipofika pale tukakuta jamaa nae yupo wamekaa na mtoto na wife, Mshikaji akaaga bila kunisalimia akaondoka zake
Nilishindwa kumwelewa nikazuga tukaendelea na mengine

Hatimae yule mtoto akamaliza LA saba, Mama ake akamtafutia shule nzuri sana yenye matokeo mazuri kila mwaka
Kimbembe kikaja kwenye ada, Mimi nikamwambia mwisho wangu ilikua ni LA saba sasa walipe wenyewe maana watoto wangu pia wameanza shule ya ma padre Lieberman ada wote wawili ni million sita kwa mwaka
Bado Nina mdogo wangu Wa kike anasoma chuo nalipa Mimi ingawa ana mkopo asilimia ishirini
Bado gharama za uendeshaji familia za kila siku, hivyo nikamwambia sitaweza kulipa, ni vema babaake ajipange kulipa

Wakuu kwa kauli yangu hiyo ulizuka mgogoro mkubwa Huduma zote muhimu nilisitishiwa pamoja na za chumbani

Akaondoka akarudi kwao kwa mwezi mzima baada ya kusuluhishwa akarudi mm nikashikilia msimamo kuwa silipi ada
Hivi karibuni wakati hayupo nimeingia kwenye mapenzi na mdada Jirani yangu amepanga upande anaish na ndugu
Wife amerudi sina hamu nae tena, huyu demu Jirani nimekua nikimpa lift asubuhi kwa muda mrefu sasa na ndipo tukaelewana na anajua matatizo yetu
Alikua akitusaidia sana nyumbani wakati wife ameondoka

Nimedhamiria kumuacha wife mazima nimeshachoka
Juzi baba amekuja akaniambia nilikushangaa ulipojifanya mjuaji kuoa mwanamke mwenye mtoto tukakuzuia ukalazimisha sasa umeyaona?

Wakuu nipo njia panda ?
Nifanyeje?

Umeyataka mwenyewe tukushauri nini sasa.Usiufuate moyo kila wakati ruhusu na akili yako ifanye kazi.Unachanganywa na uchotara mkuu kuoa aliyezaa ni tatizo kubwa sana na hapo jamaa atakuwa anamla kisirisiri.
Ulitakiwa uachane nae mapema sana kabla ya hata kufunga ndoa.
 
Huwa najiuliza Mara kumi kumi, Kijana itakuwaje uoe dem mwenye mtoto. Wakati wapo mabint kibao warembo wanatafuta Ndoa na hawana watoto. Hapo mkuu unapigiwa kila jamaa atakapo taka.
My take; Muache huyo mmanga wako, Tafuta kigori. Siku hatuoi uchafu huo.
 
Ni kweli kabisa wengi wanakosea kuhukumu watu wote kwa kosa la mtu mmoja huyu jamaa alipagawishwa na mvuto wa binti na kwa kweli hakufanya maamuzi ya busara na hakuwa na msimamo alipaswa achunguze mahusiano ya huyo mwanamke na ex wake....na mipaka ilitakiwa iwekwe tangia mwanzo sasa hivi naona mambo yamekuwa msawajiko na yeye anaharibu zaidi kucheat!!

To be honest kuishi na mwanamke mwenye mtoto au alishampenda mtu fulani walioachana nae ni shida asikwambie mtu,...
 
Hamna mke.

1. Alikosa transparency wakati mnaanza mahusiano. Hapo ndipo ulipotakiwa kuact kwa kusitisha ndoa na kuchunguza mienendo yake. Alikuwa amekuweka kwenye mtego. In the name of 'love', ukanasa.


2. Alikiuka makubaliano mliyowekeana kuhusu malezi ya mtoto, akijua hutokuwa na la kufanya. She was right. She got you cornered.

3. Alikuwa na ni msiri kuhusu mienendo yake na baba wa mtoto. Hichi kipengele ni maarufu sana nadhani.

4. Anakulazimisha uchukue jukumu la huyo mtoto, kimabavu (mabavu ya kike haya). Mkeo akitumia mabavu dhidi yako ujue umemshindwa mkuu.

Kwa maoni yangu, umefanya la maana sana kukataa kumsomesha huyo mtoto. Shikilia huo msimamo.

Kuhusu hiyo ndoa....mimi naona hamna mke hapo. Na akirudi, atakuja na mpangokazi mwingine aliouandaa na mpenzi wake - nao ni kukugeuza kitega uchumi kama hajafanya hivyo tayari. Hamna miradi au mali ulizoacha chini ya usimamizi wake kweli?

Worst case scenario....watakutoa duniani uwapishe na mambo yao.
 
Ni baadhi Mkuu si wote wako hivyo, kwa mfano unaweza kujenga penzi zito na dada ambaye yule aliyezaa naye hayuko tena duniani, ila ni mtihani mgumu kusema kweli kwa sababu baadhi ya wanaume hawapendi kumuona mzazi mwenzao akiishi katika raha na starehe hivyo watata futa sababu za kuanzisha tafrani ambazo bila shaka zitakugusa wewe kama mume na kuiona ndoa yote chungu.




mwanaume wakuingilia penzi langu jipya bado hajazaliwa. yaani tuachane eti nimeolewa utaanzaje kunifwatafwata nigombane na mume wangu? hainiingii akilini kitendo cjakuachana na mawasiliano yameisha ada ya mtoto atawasiliana na waalimu wa mtoto.

huyo mkewe ni tabia yake tu aisee na maharage alokula cjui ni ya wapi
 
To be honest kuishi na mwanamke mwenye mtoto au alishampenda mtu fulani walioachana nae ni shida asikwambie mtu,...
Inategemea na mtu mkuu na makubaliano au maelewano ya watu wawili binafsi!!Mimi nina mfano hai wa watu wanaoishi na walodumu miaka mingi lkn misimamo ni muhimu tena sana ukiwa legelege tu inakula kwako!Na kwann umebase kwa wanawake tu?na wanaume waliozalisha je?
 
Pole sana kaka, hawa wadada wenye watoto iwe aliolewa akaachika ama amejifungulia angali bado yupo nyumbani hawana msimamo kabisa. Mwanzoni atakupa simulizi nyingi za maisha yake hadi kufikia alipo, na atakushukuru sana kwa kuridhia kuwa naye kumbe anakupaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Ukishamweka ndani tu, kimbembe kinaanza. Sio kwamba nawachukia hawa viumbe, ila tabia zao ndio zinakatisha watu tamaa.
 
mabinti almost wote siku hizi ni wazazi, iwe kwa kuzaa au kwa kuzicholopoa mimba kibao.

Kigezo cha mwanamke kuwa na mtoto kisiwe sababu ya wao kutokuolewa maana sisi wanaume kumekuwa wakwepa majukumu sana inapotokea demu wako kanasa mimba, pia wapo wanaobakwa na kuzaa n.k

Tukirudi kwenye hoja nakushauri mkuu uachane tu na huyo mwarabu inaonyesha hana mapenzi ya kweli juu yako.
 
Hilo ni kweli kwa wanawake na wanaume wenye kujitambua, wengine huwa ni tamaa tu lakini ukweli ni kwamba wapo wengi ambao hawajitambui kama huyu dada ambaye pamoja na jamaa kuwa mstaarabu mpaka kufikia kumlipia mtoto asiyemhusu ada lakini huyu dada akamgusa mkono kipofu sasa machale yamemcheza hataki tena ndoa.

mwanaume wakuingilia penzi langu jipya bado hajazaliwa. yaani tuachane eti nimeolewa utaanzaje kunifwatafwata nigombane na mume wangu? hainiingii akilini kitendo cjakuachana na mawasiliano yameisha ada ya mtoto atawasiliana na waalimu wa mtoto.

huyo mkewe ni tabia yake tu aisee na maharage alokula cjui ni ya wapi
 
shida hapo naona unachokataa ndio unataka kumpatia mwenzako maana wewe tayari una watoto. Anyway huyo mke hakufai
 
Daaah...duniani kuna watu wana mioyo migumu!!!alafu bado unamuita ni mke!!na jinsi waarabu walivyo washenzi utakuta anatumia hadi 0713..,shauri yako wewe endelea kumchekea kama hatujakuzika faster.
 
Inategemea na mtu mkuu na makubaliano au maelewano ya watu wawili binafsi!!Mimi nina mfano hai wa watu wanaoishi na walodumu miaka mingi lkn misimamo ni muhimu tena sana ukiwa legelege tu inakula kwako!Na kwann umebase kwa wanawake tu?na wanaume waliozalisha je?

Psychologically mwanamke ni emotional zaid so huwa anaongozwa na hisia,..huwezi kumbadilisha akiwa na emotional feeling juu ya mtu au kitu fulani.
 
Back
Top Bottom