Najuta kuacha kazi

Najuta kuacha kazi

Kwa hyo mm nitoe hela uwasomeshe wadogo zako! Unajisahau sana!!

Hv ingekuwa ni wadago zangu! Utawasomeshaa

Acha mawazo mgandooo
 
I wish ungenijua vizuri usingesema hayo yote..ndugu zangu nawasomesha japo kwa tabu sana na vicoba bado nipo ila hata ununuzi wangu wa hisa umekuwa wa kusua sana..japo ninapita kwenye magumu i can still smile and thank God hata kwa yale madogo ninayoyafanikisha

Am not blaming you zaidi ya kukushauri accordingly n magumu kila mtu anapitia sema tunatofautiana tafuta namna ya kuzungumza na mwenza wako kwa uwazi kama ulivyoandika hapa uone atareact vipi asipokuelewa vumilia wakati unajitafuta chakufanya kuongeza kipato


Cc Kingsmann
 
Kwa hyo mm nitoe hela uwasomeshe wadogo zako! Unajisahau sana!!

Hv ingekuwa ni wadago zangu! Utawasomeshaa

Acha mawazo mgandooo
Mimi nimewasaidia kwao mangapi?yanayohitaji pesa na yasiyo hitaji?you are so selfish...
 
My dear it's simple just tell him and give him a wk Kama hajafanyia kazi tell him ur starting again to look for a job uajiliwe Tena.
Ukiona anapuuzia Anza kuandaa application mbele yake aliona hivyo atajua uko seriously
 
Mkataba wangu wa kazi uliisha nikatafuta kazi sehemu nyingine nikapata,mme wangu akanishawishi kuwa mshahara ni mdogo kuliko Mwanzo halafu ni mbali na yeye so bora nijiajiri huku nikiangalia fam kwa ukaribu

Toka nimeacha kazi,nakosa hata pesa ya mahitaji yangu muhimu,mtaji nilioahidiwa siuoni,nna madeni chungu nzima coz nawasomesha wadogo zangu wawili walikoko college(jamaa hajawi hata kunisupport na anajua situation ya nyumbani kwetu) inaniuma sana pale mama yangu anaponiomba hata elfu 20 nakosa ya kumpa wakati nikiwa kazini nilikuwa nampa pesa nyingi na kuhudumia fam bila shida..

Roho inaniuma coz ninashuhudia jinsi mme wangu na wanafamilia wenzie wanavyopanga budget ya matumizi ya wazazi wao (kwa whattsapp family group na amount ili wawapelekee wazazi wao wakati mimi mama yangu hana kitu kabisa..kwa kweli nimekata tamaa na sijui hata nifanye ninikuna wakati natamani hata kurudi kwetu ili nikajipange upya na kuanza upya maisha yangu ila nafsi inakataa

Note:mme wangu hajawahi kunikosea ni mambo kama hayo tu ndo yanayoniumiza,halafu anapenda niende kwao tu,hataki niende kwetu na wakati njia ya kwenda kwao ni lazima upite mkoani kwetu na mara nyingi tunakuwa na private car but kupita anakuwa mgumu sana..hivi wanawake wenzangu mliopo kwenye ndoa situations kama hizi mnazihandle vipi?NISAIDIENI NAKUFA kwa MAWAZO

PS: NSSF nao wananizungusha kweli kunipa kapesa kangu kadogo,nina imani nikikapata katanisaidia kuinuka tena
Wewe si ulifanyiwa send off, ulisahau nn kwa wazaz wako.
 
Wewe kipindi unadanganyika kuacha kazi hukujua situation ya nyumbani kwenu?
Hiv unaanzaje kuacha kazi kisa mwanaume kakwambia acha?

Pambana uwe na kipato chako acha kubweteka na huo mtaji utaungoja sana.
Wanaume wanashindwaga kuwapa mitaji wake zao na kuwapa mahawara.
 
Kwa hiyo umepata muda mzuri wa kuangalia movie na tamthiliya.
 
kuna wakati natamani hata kurudi kwetu ili nikajipange upya na kuanza upya maisha yangu ila nafsi inakataa
Hii brain power unayoitumia kuwaza kurudi kwenu kwanini usiitumie kuwaza mbinu za kuingiza kipato, including kutafuta kazi? Kurudi kwenu sio suluhisho na unaweza "ukajipanga upya" ukiwa hapo hapo. Hujachelewa, anza sasa.
 
Pole sana dada ninanadhani unapitia wakati mgumu kidogo kwa sasa, ila kuhusiana na hili ninadhani mumeo hajakurupuka kufanya maamuzi hayo, hii mara nyingi husababishwa na akina mama wakisha kua na kipato familia nyingi huwa na migogoro isiyoisha sanasana dharau, hutawala. Sasa kuhandle hili wanaume huamua kuwaachisha kazi wake zao ili kurudisha heshima ndani ya familia. Sasa unaweza kukuta hali kama hii imechangia. Ushauri

Lamsingi umeishagundua yakua unapitia wakati mgumu, panga siku mukalishe chini kwa unyenyekuvu muambie hali uliyonayo ikiwezekana muombe akuambie alimanisha nn kukuachisha kazi bila kujali matakwa yako. Musihi yakua utamuheshimu hata kama utakua kazin au hata ukiwa na kipato ninauhakika mume wako ni msikivu atakuelewa,. Hakikisha wanawake munapopata kipato mnabakia kwenye mipaka yenu kwenye familia ninauhakika kwakilio hiki umeishajifunza kitu hata akikupa hamsin elfu tu utaieshimu naye pia utamuheshimu na kumuona wa maana tofauti na awali. Ni hayo tu. ....
 
Mkataba wangu wa kazi uliisha nikatafuta kazi sehemu nyingine nikapata,mme wangu akanishawishi kuwa mshahara ni mdogo kuliko Mwanzo halafu ni mbali na yeye so bora nijiajiri huku nikiangalia fam kwa ukaribu

Toka nimeacha kazi,nakosa hata pesa ya mahitaji yangu muhimu,mtaji nilioahidiwa siuoni,nna madeni chungu nzima coz nawasomesha wadogo zangu wawili walikoko college(jamaa hajawi hata kunisupport na anajua situation ya nyumbani kwetu) inaniuma sana pale mama yangu anaponiomba hata elfu 20 nakosa ya kumpa wakati nikiwa kazini nilikuwa nampa pesa nyingi na kuhudumia fam bila shida..

Roho inaniuma coz ninashuhudia jinsi mme wangu na wanafamilia wenzie wanavyopanga budget ya matumizi ya wazazi wao (kwa whattsapp family group na amount ili wawapelekee wazazi wao wakati mimi mama yangu hana kitu kabisa..kwa kweli nimekata tamaa na sijui hata nifanye ninikuna wakati natamani hata kurudi kwetu ili nikajipange upya na kuanza upya maisha yangu ila nafsi inakataa

Note:mme wangu hajawahi kunikosea ni mambo kama hayo tu ndo yanayoniumiza,halafu anapenda niende kwao tu,hataki niende kwetu na wakati njia ya kwenda kwao ni lazima upite mkoani kwetu na mara nyingi tunakuwa na private car but kupita anakuwa mgumu sana..hivi wanawake wenzangu mliopo kwenye ndoa situations kama hizi mnazihandle vipi?NISAIDIENI NAKUFA kwa MAWAZO

PS: NSSF nao wananizungusha kweli kunipa kapesa kangu kadogo,nina imani nikikapata katanisaidia kuinuka tena

Pole sana mpendwa. Ngoja nikwambie, umefanya kosa kubwa sana kuacha Kazi kwasababu mume kasema. Ndio ni vizuri kumuheshimu mume wako ila maisha yamebadilika sana, lolote linaweza tokea. Ulitakiwa ukae nae chini na kumueleza vizuri sababu za wewe kutokuacha Kazi.

Haujachelewa, dawa hapo ni kurudi kazini tu au akupe mtaji wa biashara mara moja. Umeshajionea yaliyokukuta, kukaa na kuongea nae akuhudumie wewe na familia yako sio jawabu la tatizo lako. Anaweza akakuhudumia leo, kesho akachoka na pia kumbuka maisha ni mapito, ikitokea hana kazi lazima wewe uwe Backup. Get a job ASAP, Mimi sikushauri ukae uombe kuhudumiwa. Kaa nae mwambie I am going back to work na reasons ni ABC....

Imeandikwa katika Bible amtegemeaye mwanadamu kalaaniwa. Mwanaume lazima akuhudumie ila na wewe lazima uwe na chako.

All the best .
 
Wanawake akili zao wanazijua wenyewe.. Wa kwangu kila siku alikuwa ananiimbiwa story za kurudi kwao, this time nimempa nauli aende akaanza kudata.
Hii brain power unayoitumia kuwaza kurudi kwenu kwanini usiitumie kuwaza mbinu za kuingiza kipato, including kutafuta kazi? Kurudi kwenu sio suluhisho na unaweza "ukajipanga upya" ukiwa hapo hapo. Hujachelewa, anza sasa.
 
Duuh kwaio kwanini wazazi wako wasiwasomeshe hao wadogo zako? Hadi uwasomeshe wewe? Ni jukumu la mzazi kusomesha mtoto wake, ila kwa ushuhuda tu mimi nilishawahi kuacha kazi sehemu ili nijiajiri sikua na back up plan nilitaka nimgeze mzee wangu aisee nilipitia waya mkali sana siwezi kusahau 2016 ilikua ngumu sana sema sababu CV ilikua inaeleweka nikaanza omba kazi tena Mungu si athumani wala abdallah nikapata lazi kufanya kazi miezi minne ikafungwa ofisini nikasota miezi kama 11 nikaja pata sehemu..ambayo kimsingi si haba maisha yanaendam.cha msingi omba kazi upya utapata tu
 
Wanawake akili zao wanazijua wenyewe.. Wa kwangu kila siku alikuwa ananiimbiwa story za kurudi kwao, this time nimempa nauli aende akaanza kudata.
Shemeji mke wa bwana mdogo alileta hizo na jamaa akamwambia nenda. 5 months down the line mwanamke anataka kurudi na jamaa akagoma kabisa. Ilibidi mwanamke akalilie ukweni na mama mtu kumrudisha kwa nguvu mguu kwa mguu. Kuondoka home kwa hasira in most case inaharibu badala ya kujenga
 
Tafuta kazi, ukipata tulia ufanye kazi achana na ahadi zisizo timia, me anakishauri uache kazi unakubali! Kweli? Pole sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom