Najuta kuacha kazi

Najuta kuacha kazi

Doh!. Pole sana. Utakua kiaina unamuogopa mmeo. Means sio rafikiako kiviiile..
Me siko kune ndoa. Ushauri wangu unaweza kua ni wa ki-wapenzi zaidi.. ila pole sana
Mkuu, pamoja na kwamba haupo kwenye ndoa na labda umejiona umesema kitu ndogo sana.... Lakini nikuhakikishie tu kwamba umenena jambo kubwa na lenye maana sana.
Wana ndoa wakiwa marafiki (hawaogopani), watapata fursa ya kujadili kila jambo linalo jiri ndani ya familia yao, tena pasipo mmoja kuwa na maumivu kwasababu ya mwingine
 
He is selfish, tupo kwenye ndoa lakini huyo wako ni mbinafsi na roho mbaya, atlist for now anajua situation ya kwako angekusapoti mpaka hapo utakaposimama tena

Kosa kubwa ulilofanya ni kuacha kazi, trust me, mambo mengi kwenye familia huwa yanasimamiwa na kina mama, na ili uweze kuyasimamia ipasavyo ni lazima iwe na kipato japo kidogo,

Unajua kumuomba mwanaume hela hadi ya kumtumia mama yako mzazi ni kitu kigumu sana, ila ukiwa na ya kwako wala humsumbui

All in all anakosea,

Je ulipokua unafanya kazi ulikua unaisapoti familia yao? Na je alikua anaijali familia yako?
Mkataba wangu wa kazi uliisha nikatafuta kazi sehemu nyingine nikapata,mme wangu akanishawishi kuwa mshahara ni mdogo kuliko Mwanzo halafu ni mbali na yeye so bora nijiajiri huku nikiangalia fam kwa ukaribu

Toka nimeacha kazi,nakosa hata pesa ya mahitaji yangu muhimu,mtaji nilioahidiwa siuoni,nna madeni chungu nzima coz nawasomesha wadogo zangu wawili walikoko college(jamaa hajawi hata kunisupport na anajua situation ya nyumbani kwetu) inaniuma sana pale mama yangu anaponiomba hata elfu 20 nakosa ya kumpa wakati nikiwa kazini nilikuwa nampa pesa nyingi na kuhudumia fam bila shida..

Roho inaniuma coz ninashuhudia jinsi mme wangu na wanafamilia wenzie wanavyopanga budget ya matumizi ya wazazi wao (kwa whattsapp family group na amount ili wawapelekee wazazi wao wakati mimi mama yangu hana kitu kabisa..kwa kweli nimekata tamaa na sijui hata nifanye ninikuna wakati natamani hata kurudi kwetu ili nikajipange upya na kuanza upya maisha yangu ila nafsi inakataa

Note:mme wangu hajawahi kunikosea ni mambo kama hayo tu ndo yanayoniumiza,halafu anapenda niende kwao tu,hataki niende kwetu na wakati njia ya kwenda kwao ni lazima upite mkoani kwetu na mara nyingi tunakuwa na private car but kupita anakuwa mgumu sana..hivi wanawake wenzangu mliopo kwenye ndoa situations kama hizi mnazihandle vipi?NISAIDIENI NAKUFA kwa MAWAZO

PS: NSSF nao wananizungusha kweli kunipa kapesa kangu kadogo,nina imani nikikapata katanisaidia kuinuka tena
 
Mkataba wangu wa kazi uliisha nikatafuta kazi sehemu nyingine nikapata,mme wangu akanishawishi kuwa mshahara ni mdogo kuliko Mwanzo halafu ni mbali na yeye so bora nijiajiri huku nikiangalia fam kwa ukaribu

Toka nimeacha kazi,nakosa hata pesa ya mahitaji yangu muhimu,mtaji nilioahidiwa siuoni,nna madeni chungu nzima coz nawasomesha wadogo zangu wawili walikoko college(jamaa hajawi hata kunisupport na anajua situation ya nyumbani kwetu) inaniuma sana pale mama yangu anaponiomba hata elfu 20 nakosa ya kumpa wakati nikiwa kazini nilikuwa nampa pesa nyingi na kuhudumia fam bila shida..

Roho inaniuma coz ninashuhudia jinsi mme wangu na wanafamilia wenzie wanavyopanga budget ya matumizi ya wazazi wao (kwa whattsapp family group na amount ili wawapelekee wazazi wao wakati mimi mama yangu hana kitu kabisa..kwa kweli nimekata tamaa na sijui hata nifanye ninikuna wakati natamani hata kurudi kwetu ili nikajipange upya na kuanza upya maisha yangu ila nafsi inakataa

Note:mme wangu hajawahi kunikosea ni mambo kama hayo tu ndo yanayoniumiza,halafu anapenda niende kwao tu,hataki niende kwetu na wakati njia ya kwenda kwao ni lazima upite mkoani kwetu na mara nyingi tunakuwa na private car but kupita anakuwa mgumu sana..hivi wanawake wenzangu mliopo kwenye ndoa situations kama hizi mnazihandle vipi?NISAIDIENI NAKUFA kwa MAWAZO

PS: NSSF nao wananizungusha kweli kunipa kapesa kangu kadogo,nina imani nikikapata katanisaidia kuinuka tena
Hamishia wazazi wako hapo nyumbani unapoishi na mumeo. Hamishia ukoo mzima hapo kwenu
 
Ulikosea kabla ya kuacha kazi ilitakiwa ujue je hela huwa unapewa kiasi gani na huyo mumeo,pia ungeomba ushauri hata kwa watu kadhaa.

Mkuu ningumu kumtegemea mtu mmoja ktk familia atoe kila kitu,bora ungekuwa umejiandaa hata kwa biashara.

Huyo mmeo atakuwa na wivu sana na unapenda kunyenyekewa sana ndiyo maana alijua ukiacha kazi utakuwa unabembeleza,baby naomba,baby naomba.........kakukosea sana na nyie mkiolewa Dada zetu bakisheni akili kidogo mapenzi yapo tu
 
Natumai u mzima wa afya njema, nimesoma ujumbe wako nimesikia kuumia sana moyoni,!

La Princesa,najaribu kuitazama hali ya mama yangu kule kijijini,halafu akose mtu wa kumsaidia ilhali yeye hana uwezo wa kujitafutia pesa ya kujikimu,roho inauma sana

Lakini vipi shemeji umejaribu kuongea naye juu ya jambo hilo? Na kwanini akuwekee mazingira magumu wewe kwenda kumuona mama? Kwa vyovyote vile,huyo ni mzazi wako na kama hana msaada mwingine zaidi ya wewe,usikubali kumuacha mama akateseka,(ni mama kama alivyo mama wa mumeo)

Sikushauri kuvunja ndoa yako hata kidogo,lakini ni muhimu kutafuta namna zozote zinazowezekana kuhakikisha mama anapata angalau kiasi kidogo cha kumuwezesha kupata mahitaji yake

Dada,mimi ni mwanaume,najua wakati fulani si rahisi sana kushauriwa na mwanaume namna ninavyokushauri

Kwanza ukiona hali imekuwa ngumu sana kupata pesa,bana hata ya matumizi ya nyumbani,mtumie mama,(mf kama anakupa bajeti ya sh.15000 kwa siku,hakikisha hapo angalau 7000 unaiweka pembeni,kwa wiki nzima mtumie mama) maisha yaendelee

Ukweli kuacha kazi haukuwa uamuzi mzuri,hasa ukizingatia nature ya mume wako,lakini haupaswi kujutia tu,ni lazima uchukue hatua,bora ukala maharage,dagaa kwa angalau wiki moja,umsapoti mama!

Pole sana,kwa mapito hayo magumu..

Asante,mkuu nakwambia hivi pesa ya kujikimu mahitaji yangu mwenyewe nakosa kwa mfano wakati nipo kazini nilikuwa naenda saloon nasuka,nafanya pedicure now siwezi coz nakosa hiyo pesa

Sokoni huwa naenda naye tunanunua vitu yeye analipa hapo ndo ilipo changamoto,pesa yake kuishika ni mpaka awe amesafiri na hapo vitu vinakuwepo ndani so ndo anaweza akaacha pesa kiasi ya emergency
 
Yeu
Ulikosea kabla ya kuacha kazi ilitakiwa ujue je hela huwa unapewa kiasi gani na huyo mumeo,pia ungeomba ushauri hata kwa watu kadhaa.

Mkuu ningumu kumtegemea mtu mmoja ktk familia atoe kila kitu,bora ungekuwa umejiandaa hata kwa biashara.

Huyo mmeo atakuwa na wivu sana na unapenda kunyenyekewa sana ndiyo maana alijua ukiacha kazi utakuwa unabembeleza,baby naomba,baby naomba.........kakukosea sana na nyie mkiolewa Dada zetu bakisheni akili kidogo mapenzi yapo tu

Yeye ndo alinishawishi niache,nimeshindwa kwenda in details sana ili wanaotufahamu wasije wakaunga dots...asante kwa ushauri though
 
Yeu


Yeye ndo alinishawishi niache,nimeshindwa kwenda in details sana ili wanaotufahamu wasije wakaunga dots...asante kwa ushauri though
Ila ulikosea kuacha bila kujua nini kitakuwa chanzo chako cha mapato,pole sana,Mungu ni mwema atakuinua
 
Kuna kitu nimekutumia PM, ingawa naona kama umeifunga PM yako.
Mkuu, nakushauri ungefunguwa PM yako ili upate msaada kwa hali hii yenye unaipitia. Na ikiwa utaona kama panatokea mtu mwenye kukuletea yasio kupendeza huko PM, basi nivyema ukam-block.
sawa muhenga nilikuona ile siku ya Jumanne
 
Ila ulikosea kuacha bila kujua nini kitakuwa chanzo chako cha mapato,pole sana
Nakiri kosa..ila kama nilivyosema alisema kituo nilichopangwa ni mbali na salary ni ndogo so atanipa mtaji nifanye biashara nnayoipenda nikiwa karibu na nyumbani,so nikaona ni vyema ila changamoto ndo ikawa hiyo mtaji sijapewa mwezi wa 9 huu toka niache kazi
 
Asante,mkuu nakwambia hivi pesa ya kujikimu mahitaji yangu mwenyewe nakosa kwa mfano wakati nipo kazini nilikuwa naenda saloon nasuka,nafanya pedicure now siwezi coz nakosa hiyo pesa

Sokoni huwa naenda naye tunanunua vitu yeye analipa hapo ndo ilipo changamoto,pesa yake kuishika ni mpaka awe amesafiri na hapo vitu vinakuwepo ndani so ndo anaweza akaacha pesa kiasi ya emergency
Duuh,huyo jamaa ni hatari...
Ni mchaga nini??
 
Nakiri kosa..ila kama nilivyosema alisema kituo nilichopangwa ni mbali na salary ni ndogo so atanipa mtaji nifanye biashara nnayoipenda nikiwa karibu na nyumbani,so nikaona ni vyema ila changamoto ndo ikawa hiyo mtaji sijapewa mwezi wa 9 huu toka niache kazi
Pole Dada Mungu ni mwema hata kuacha,atakuinua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom