Nimetokea kumpenda sanaaaa kaka mmoja hapa jamiiforums!
Kusema kweli tulikuwa marafiki mwanzo ila yeye akasema ametokea kuvutiwa na maongezi yetu na ananipenda and blah blah blah..nikawa nasita sana kwasababu najua niko mbali nae na mambo ya long distance ni matatizo (kama walivyosema wahenga fimbo ya mbali haiuwi nyoka) lakini kwasababu alisisitiza sana anahitaji kuwa na mm nikaona kwanini nisijaribu kumpa nafasi japo nilishaumziwa sana mwanzo..
Huyo mtu kwa maelezo yake ni mjane na ana watoto wawili...Mwanzoni kila kitu kilikuwa shwari maongezi saa zote..tukaplan mpaka kuonana..kusema kweli nilikuwa na matumaini sana na furaha nimeshapata mwenza...
Ikatokea ishu kwamba alikuwa na matatizo ya network ya sim kitu ambacho kinaeleweka mawasiliano yakaanza kuyumba ila net alikuwa nayo lakini hakuona kama njia ya mawasiliano...Sasa kinachoendelea ni kwamba tangia tarehe 4 mwezi huu kapotea...namuona watsapp na naona anapata ujumbe wangu lakini hanijibu..na pia nilimuona facebook minamo tar 6...lakini mimi mawasiliano nae sina kwasababu hapokei simu zangu,hajibu sms zangu na sijui pakumpata..na ameniblock watsapp leo hii coz nimeshafanya uchunguzi na nimegundua kwamba ameniblock! Nakaa nikijiuliza nimemkosea nini kustahiki kutendewa hivi sielewi!kama hawezi kuwa na mimi kwanini haniambii kwamba hanitaki?kama hana mawasiliano mbona namuona online?
Sikujua kama watu wengine wamenyimwa ustaarabu kiasi hiki! Sio siri nimempenda na kumuamini sana huyu mkaka lakini naona kaniachia donda kubwa sana moyoni mwangu maana hata sielewi nimuweke fungu gani najiona -------- nilopindukia kujirahisisha na kumuamini mtu nisomjua! Au sijui ni mimi ndio na overreact na kumfatilia sana?
Nisaidieni jamani nahisi kuchanganyikiwa si ndo wendawazim huu mungu wangu!