Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,921
- 30,267
"Hadi asuswe na Waislamu wenzake, wana TANU na wananchi wote, bali lilikuwapo tatizo kubwa.
Hii haiwezekani ikatokea tu kama bahati mbaya, hapana."
(Kaniuliza Muulizaji)
MOHAMED SAID ANAJIBU:
"Hakika lilikuwapo tatizo kubwa
Katika mkutano uliofanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio Ukerewe Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe walipokwenda kumtaka ushauri kuhusu kumwingiza Nyerere kwenye uongozi wa juu wa TAA Hamza alishauri kuwa Nyerere achaguliwe kuwa rais na mwaka unaofuatia 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.
Historia hii nimeieleza mara nyingi naamini wengi wanaijua.
Nafasi ile ilitakiwa ishikwe na Mkristo ili upatikane umoja wa wananchi wote.
Harakati za siasa zilitawaliwa na Waislam na hofu ilikuwa ikiwa TANU itaundwa na kiongozi ni Muislam sura iliyokuwa imejengeka itadhihirisha kuwa harakati zile ni za Waislam.
Waingereza watatia fitna kuwashawishi Wakristo na wao wawe na chama cha siasa.
TANU walijifunza lililowafika Mohamed Ali Jinnah na Nehru kudai uhuru vyama vyao viwili vimejishikiza kwenye dini zao - Uislam na Uhindu.
Leo usiku wanapewa uhuru.
Asubuhi vita vya wenyewe kwa wenyewe vinalipuka.
TANU ilitaka kujiepusha na balaa hili.
Hili lingefanyika Tanganyika ingeingia katika kudai uhuru imegawanyika katika misingi ya dini.
Baada ya uchaguzi wa Arnautoglo baina ya Abdul Sykes na Nyerere 1953 na TANU kuundwa 1954 Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na Baraza la Wazee wa TANU chini ya uongozi wa Sheikh Suleiman Takadir wakafanya juhudi kubwa kujenga umoja wa wananchi chini ya Julius Nyerere.
Kuna historia ya kusisimua jinsi Bantu Group nayo kwa upande wake ilivyohamasisha wananchi kuwa wamoja kwa kufuta, "Salaam Aleikum Warahmatullah Wabarakatuh," kuwa mamkizi ya wanachama wa TANU.
Bantu Group akina Juma Selemani na Rashid Sisso wakaja na Salaam mpya, "Ahlan Tabu."
Hii Ahlan Tabu mimi niliiwahi na kuisikia kwa masikio yangu nikiwa na kama miaka mitano hivi.
Kibwagizo cha "Uhuru na Umoja" kilipokuja ndiyo Ahlan Tabu ikafa.
Yapo mengi na yote nimeyaeleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Sasa baada ya shutuma zile za Sheikh Suleiman Takadir dhidi ya Nyerere Waislam wote walimghadhibikia Sheikh Takadir wakamuona anasaliti msimamo uliowekwa na waasisi wenyewe wa TANU.
Hii ilikuwa 1958 na ilikuwa wazi kabisa kuwa uhuru unakaribia.
Hili ndilo tatizo kubwa lililokuwapo.
Bahati mbaya historia hii ya TANU ilifutwa na hii ndiyo sababu leo naulizwa nini lilikuwa tatizo kubwa kiasi Sheikh Suleiman Takadir apigwe pande hata na nduguze Waislam?"
Hii haiwezekani ikatokea tu kama bahati mbaya, hapana."
(Kaniuliza Muulizaji)
MOHAMED SAID ANAJIBU:
"Hakika lilikuwapo tatizo kubwa
Katika mkutano uliofanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio Ukerewe Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe walipokwenda kumtaka ushauri kuhusu kumwingiza Nyerere kwenye uongozi wa juu wa TAA Hamza alishauri kuwa Nyerere achaguliwe kuwa rais na mwaka unaofuatia 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.
Historia hii nimeieleza mara nyingi naamini wengi wanaijua.
Nafasi ile ilitakiwa ishikwe na Mkristo ili upatikane umoja wa wananchi wote.
Harakati za siasa zilitawaliwa na Waislam na hofu ilikuwa ikiwa TANU itaundwa na kiongozi ni Muislam sura iliyokuwa imejengeka itadhihirisha kuwa harakati zile ni za Waislam.
Waingereza watatia fitna kuwashawishi Wakristo na wao wawe na chama cha siasa.
TANU walijifunza lililowafika Mohamed Ali Jinnah na Nehru kudai uhuru vyama vyao viwili vimejishikiza kwenye dini zao - Uislam na Uhindu.
Leo usiku wanapewa uhuru.
Asubuhi vita vya wenyewe kwa wenyewe vinalipuka.
TANU ilitaka kujiepusha na balaa hili.
Hili lingefanyika Tanganyika ingeingia katika kudai uhuru imegawanyika katika misingi ya dini.
Baada ya uchaguzi wa Arnautoglo baina ya Abdul Sykes na Nyerere 1953 na TANU kuundwa 1954 Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na Baraza la Wazee wa TANU chini ya uongozi wa Sheikh Suleiman Takadir wakafanya juhudi kubwa kujenga umoja wa wananchi chini ya Julius Nyerere.
Kuna historia ya kusisimua jinsi Bantu Group nayo kwa upande wake ilivyohamasisha wananchi kuwa wamoja kwa kufuta, "Salaam Aleikum Warahmatullah Wabarakatuh," kuwa mamkizi ya wanachama wa TANU.
Bantu Group akina Juma Selemani na Rashid Sisso wakaja na Salaam mpya, "Ahlan Tabu."
Hii Ahlan Tabu mimi niliiwahi na kuisikia kwa masikio yangu nikiwa na kama miaka mitano hivi.
Kibwagizo cha "Uhuru na Umoja" kilipokuja ndiyo Ahlan Tabu ikafa.
Yapo mengi na yote nimeyaeleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Sasa baada ya shutuma zile za Sheikh Suleiman Takadir dhidi ya Nyerere Waislam wote walimghadhibikia Sheikh Takadir wakamuona anasaliti msimamo uliowekwa na waasisi wenyewe wa TANU.
Hii ilikuwa 1958 na ilikuwa wazi kabisa kuwa uhuru unakaribia.
Hili ndilo tatizo kubwa lililokuwapo.
Bahati mbaya historia hii ya TANU ilifutwa na hii ndiyo sababu leo naulizwa nini lilikuwa tatizo kubwa kiasi Sheikh Suleiman Takadir apigwe pande hata na nduguze Waislam?"