Historia Fupi ya Bibi Titi Niliyozungumza Uwanja wa Ujanaa Ikwiriri Kilele Cha Bibi Titi Festival

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,918
30,259
HISTORIA FUPI YA BIBI TITI NILIYOZUNGUMZA UWANJA WA UJAMAA KATIKA KILELE CHA BIBI TITI FESTIVAL

Nilifungua kwa kusema kuwa Bibi Titi hana mfanowe.

Rufiji ina historia ya pekee katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

TANU ilipoundwa kazi ya usajili walipewa Mwalimu Julius Nyerere, TANU Territorial President, Kadi ya TANU No. 1, Abdul Sykes Kadi No. 3 na Ally Sykes Kadi No. 2.

Msajili Mwingereza akakataa kuisajili TANU kwa kuwa Nyerere hakuwa na orodha ya wanachama wala kadi za TANU.

Alipofikisha taarifa hii kwa wenzake, Abdul akasema aitwe Said Chamwenyewe.

Said Chamwenyewe akakabidhiwa rejesta na kadi za TANU aende Rufiji akalete wanachama wa TANU.

Hivi ndivyo TANU ilivyosajiliwa November 1954.

TANU ilikuwa na wazungumzaji hodari watatu: Julius Nyerere, Sheikh Suleiman Takadir na Bibi Titi.

Bibi Titi amehutubia mikutano miwili Viwanja Vya Mnazi Mmoja hajapata kumuona Nyerere.

Siwezi kukuambieni kati ya Nyerere nani kamzidi mwengine kwa kuwa nyie hapa mmemsikia Nyerere hamjapata kumsikia Bibi Titi.

Lakini kwa kuwa inajengwa Maktaba ya Bibi Titi Dodoma, pale zitawekwa hotuba za Bibi Titi na mtamsikia Bibi Titi na mtaamua wenyewe nani kamzidi mwenzie.

Lakini Abbas Sykes amepata kuniambia kuwa kulikuwa na wakati Nyerere anaishiwa na la kusema na akimuomba Bibi Titi azungumze.

Kutoka hotuba ya Bibi Titi Mwalimu Nyerere atapata maneno ya kusema.

Bibi Titi hakunyanyua kalamu kuandika maisha yake lakini kabla ya kufariki kwake alimweleza Leila Sheikh historia yote ya maisha yake.

Leila kafariki hakujaaliwa kuandika historia ya Bibi Titi.

Zifanyike juhudi historia ya Bibi Titi iandikwe ili kitabu kiwepo katika Maktaba ya Bibi Titi itakapofunguliwa.
 
Tunakushukuru sana mzee Mohamed Said kwa kuendelea kutuletea taarifa mbalimbali za kihistoria. Kwa kweli zinasaidia sana kutufungua macho. Watu kama wewe mngeteuliwa na Rais kuwa washauri wa masuala ya histroria, tungekuwa hatufichwi mambo mengi ya kihistoria.

Kwa mfano, historia ya mapinduzi ya zanzibar imebagua kwa makusudi John Okello aliyehusika kwa kiasi kikubwa kufanikisha mapinduzi. Inauma sana.
 
HISTORIA FUPI YA BIBI TITI NILIYOZUNGUMZA UWANJA WA UJAMAA KATIKA KILELE CHA BIBI TITI FESTIVAL

Nilifungua kwa kusema kuwa Bibi Titi hana mfanowe.

Rufiji ina historia ya pekee katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

TANU ilipoundwa kazi ya usajili walipewa Mwalimu Julius Nyerere, TANU Territorial President, Kadi ya TANU No. 1, Abdul Sykes Kadi No. 3 na Ally Sykes Kadi No. 2.

Msajili Mwingereza akakataa kuisajili TANU kwa kuwa Nyerere hakuwa na orodha ya wanachama wala kadi za TANU.

Alipofikisha taarifa hii kwa wenzake, Abdul akasema aitwe Said Chamwenyewe.

Said Chamwenyewe akakabidhiwa rejesta na kadi za TANU aende Rufiji akalete wanachama wa TANU.

Hivi ndivyo TANU ilivyosajiliwa November 1954.

TANU ilikuwa na wazungumzaji hodari watatu: Julius Nyerere, Sheikh Suleiman Takadir na Bibi Titi.

Bibi Titi amehutubia mikutano miwili Viwanja Vya Mnazi Mmoja hajapata kumuona Nyerere.

Siwezi kukuambieni kati ya Nyerere nani kamzidi mwengine kwa kuwa nyie hapa mmemsikia Nyerere hamjapata kumsikia Bibi Titi.

Lakini kwa kuwa inajengwa Maktaba ya Bibi Titi Dodoma, pale zitawekwa hotuba za Bibi Titi na mtamsikia Bibi Titi na mtaamua wenyewe nani kamzidi mwenzie.

Lakini Abbas Sykes amepata kuniambia kuwa kulikuwa na wakati Nyerere anaishiwa na la kusema na akimuomba Bibi Titi azungumze.

Kutoka hotuba ya Bibi Titi Mwalimu Nyerere atapata maneno ya kusema.

Bibi Titi hakunyanyua kalamu kuandika maisha yake lakini kabla ya kufariki kwake alimweleza Leila Sheikh historia yote ya maisha yake.

Leila kafariki hakujaaliwa kuandika historia ya Bibi Titi.

Zifanyike juhudi historia ya Bibi Titi iandikwe ili kitabu kiwepo katika Maktaba ya Bibi Titi itakapofunguliwa.
Tunamshukuru sana kutuhabarisha mambo hadimu kama hayo Mungu akujalie maisha marefu, ila nina suali moja kwanini sehemu zulio lea Tanu na kutoa watu mashuhuri wa TANU, hazikuendelezwa na TANU au CCM, baada ya kupata uhuru kwa mfano Rufiji Kilwa Tanga Ikwiriri Tabora, lakini sehemu zisio kua na historia yoyote zikaendelezwa baada ya uhuru kama Arusha, Dodoma nk........
 
Back
Top Bottom