Kila website ina IP address yake.
Hosts file ni text file ambayo kazi yake ni ku-redirect websites fulani kwenda IP addresses fulani (kwa lugha nyepesi).
Mfano:-
104.25.213.115 jamiiforums.com
Hivyo,
Kwenye hosts file uki-redirect Jamiiforums.com kwenda 185.60.219.35 instead of IP yake i.e 104.25.213.115, basi kila uandikapo Jamiiforums.com kwenye browser na ku-bofya "ENTER" utajikuta unapelekwa Fesibuku!
Mfano:-
185.60.219.35 jamiiforums.com
Tukija kwenye ku-block matangazo/ads, kwenye hosts file huwa tuna-redirect list ya websites ambazo ndizo zenye kuleta hayo matangazo kwenda IP address "0.0.0.0".
0.0.0.0 itaifanya hiyo website ya matangazo isipatikane/isiji-load pindi ukiperuzi websites mbalimbali.
Umenisoma, Mkuu?