Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,988
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini, akisalimiana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita ACP Safia Jongo, wakati alipotembelea na kukagua Kituo kidogo cha Polisi Bwanga Wilayani Chato katika Mkoa wa Geita Septemba 20, 2023.
Waziri Sagini ametoa maagizo hayo alipotembelea na kukagua Kituo kidogo cha Polisi Bwanga Wilayani Chato katika Mkoa wa Geita ambapo alipokelewa na Mwenyeji wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, ACP Safia Jongo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini (Mb), akipokea taarifa ya kituo na hali ya Askari toka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita ACP Safia Jongo, wakati alipotembelea na kukagua Kituo kidogo cha Polisi Bwanga Wilayani Chato katika Mkoa wa Geita, Septemba 20, 2023.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini, akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea na kukagua Kituo kidogo cha Polisi Bwanga Wilayani Chato katika Mkoa wa Geita, Septemba 20, 2023.
Naibu Waziri Sagini amelipongeza Jeshi la Polisi Mkoani Geita kwa kufanikiwa kudhibiti vurugu zilizoanzishwa na vijana dhidi ya Jeshi hilo kufuatia kuingilia kati kuokoa maisha ya raia aliyekuwa anashambuliwa na Wananchi kwa kutuhumiwa kuiba vifaa vya mziki msibani katika eneo la Bwanga Mkoani humo.
Pia ametoa rai kwa Wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi kwa kudhuru maisha ya wenzao kwani kufanya hivyo ni kosa la jinai na kuwataka kuimarisha shughuli za polisi jamii kwa lengo la kuimarisha usalama, kudhibiti uhalifu na kuepuka kujichukulia sheria mkononi.
Sehemu ya Askari wa Kituo kidogo cha Polisi Bwanga Wilayani Chato katika Mkoa wa Geita, wakisikiliza kwa makini maelekezo ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini, wakati alipotembelea na kukagua Kituo hicho Septemba 20, 2023.
Naye, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita ACP Safia Jongo, amemshukuru Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kufika kituoni hapo huku akimuhakikishia kuwa hali ya usalama mkoani humo ni shwari na wale wote wenye kuleta viashiria vya uvunjifu wa amani watashughulikiwa.
Askari wa Kituo kidogo cha Polisi Bwanga Wilayani Chato katika Mkoa wa Geita, wakionesha ukakamavu mbele ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini, wakati alipotembelea na kukagua Kituo hicho Septemba 20, 2023.